Hii habari ya Jumatano ya Majivu asili yake ni nini!?

Niseme tu ukweli kwamba kiasi fulani nakereka na hii imani ya kuchorana chorana na majivu kwa hii siku inaitwa Jumatano ya majivu.

Hebu nieleweshwe labda nikielewa ntaiona sawa..

=======

UPDATES:

IFAHAMU JUMATANO YA MAJIVU

UTANGULIZI
Jumatano ya majivu ni mwanzo wa kipindi cha kwaresima katika kanisa. Ni ishara ya kuanza kwa siku arobaini za kutafakari kwa undani fumbo kuu la upendo wa Mungu linalofunuliwa kwa kujitoa kwake na kufa msalabani, kifo cha aibu ili kuichukua aibu yetu. Mama kanisa anatupatia kipindi hiki ili tuweze kutafakari njia na mienendo yetu.


KWA NINI TUNAPAKWA MAJIVU?
Majivu ni ishara ya majuto, nayo hufanywa visakramenti kwa kubarikiwa na kanisa. Tunapopakwa majivu katika paji la uso hutusaidia kutafakari na kutukumbusha kuwa wanadamu sisi tu mavumbi na mavumbini tutarudi. Hutukumbusha zaidi kuwa maisha ya hapa duniani tunapita na safari yetu itakamilika pale tutakapoungana na Bwana na mwokozi wetu katika ufalme wako.
Angalia; Isaya 61:3, Ester 4:1-3, Yeremia 6:26, Ezekieli 27:30, Mathayo 11:21 na Luka 10:13


KWA NINI MAJIVU YAPAKWE KATIKA PAJI LA USO NA SI PENGINEPO?
Ishara yoyote iwekwayo katika paji la uso huonesha umiliki (soma Ufunuo 7:3, Ufunuo 9:4, Ufunuo 14:1, Ezekieli 9:4-6, ). Tunapochorwa ishara ya msalaba katika paji la uso ni ishara kwamba sisi tupo chini yake yeye aliyekufa msalabani kwa ajili yetu.
Hali kadhalika hutukumbusha ishara ya msalaba tuliyochorwa na mafuta matakatifu siku ya ubatizo wetu, hutukumbusha ahadi tuliyoiweka siku hiyo ya ubatizo na kutuita tuishi maisha ya utakatifu


MANENO ANAYOTAMKA PADRE YANA MAANA GANI?
Tunapopakwa majivu Padre husema; Mwanadamu kumbuka u mavumbi na mavumbini utarudi AU Tubuni na kuiamini Injili.
Maneno haya kwa upande mmoja hutukumbusha tunapoelekea, tusisikitike kwamba siku moja tutarudi mavumbini bali tuwe na furaha kwani wakati miili yetu unarudi mavumbini roho zetu zitakwenda kuungana na Mungu Baba mbinguni.
Hivyo maandalizi tunayoalikwa kuyafanaya si maandalizi ya kuelekea mavumbini bali maandalizi ya kuelekeza roho zetu mbinguni. Ndio maana pia twaambiwa tubuni na kuiamini Injili.


MAJIVU HUTOKA WAPI?
Majivu tunayopakwa hutoka katika matawi yaliyotumika katika jumapili ya matawi ya mwaka jana. Majivu haya hubarikiwa na kuwa visakramenti. Hivyo majivu yanapoashiria toba na majuto pia hutukumbusha wema wa Mungu na utayari wake wa kutusamehe.


KWA NINI TUNATUMIA MATAWI YA JUMAPILI YA MATAWI?
Matawi haya yalimkaribisha Yesu Yerusalemu akiwa tayari kufa kwa ajili ya dhambi zetu, yalimpokea mfalme kwa furaha na shangwe kuu. Matawi haya yanapochomwa na sisi kupakwa majivu yetu yanatukumbusha kuwa ni kwa ajili ya dhambi zetu Mungu alimtoa mwanae wa pekee kufa msalabani kwa ajili ya dhambi zetu sisi wanaadamu. Hivyo hututafakarisha kuacha dhambi.

KANISA LIMEKATAZA NINI SIKU YA JUMATANO YA MAJIVU?
Tumekatazwa kula chakula siku ya Jumatano ya Majivu na kula nyama siku ya Ijumaa Kuu katika Amri ya Pili ya Kanisa.

NANI ANALAZIMA KUFUNGA SIKU YA JUMATANO YA MAJIVU NA KWARESMA?
Kila Mkristo aliyetimiza miaka 14 na zaidi anapaswa kufunga kula nyama (Ijumaa kuu) na mwenye miaka zaidi ya 21 kufunga chakula Jumatano ya Majivu

TUNAPOSEMA KUJINYIMA WAKATI WA KWARESMA TUNAMAANA GANI?
Kujinyima ni kujikatalia kitu ukipendacho mfano nyama, pombe, sigara, muziki, safari, maongezi n.k.

MWISHO
Wakati wa Kwaresma Waamini wanapaswa kujitakasa zaidi kwa kusali, kufunga, toba na matendo mema

Kipindi cha Kwaresima ni fursa makini ya kumkimbilia Mwenyezi Mungu, kwani kwa njia ya dhambi wamejikuta wakiwa mbali na Uso wa huruma ya Mungu, kiasi hata cha kupoteza imani na matumaini kwa Mwenyezi Mungu. Hii ni changamoto ya kumpenda Mungu na jirani badala ya kukumbatia malimwengu yanayoendelea kuwatumbukiza katika utupu wa maisha ya kiroho. Kwaresima ni kipindi cha waamini kukimbilia na kuambata huruma ya Mungu inayoganga na kuponya dhambi. Ni wakati wa sala, upendo na kufunga.
Wasabato mna tabu sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakristo hawana uvumilivu kabisa kwenye kuuulizwa swali, huishiwaga hoja mapema mno na kukimbikia matusi, yaaan ni jins gani inavyojidhihilisha kwamba ndugu zetu wako weupe kwenye hii dini.
Ni wachache sana wanauelewa, lakini waliobakia empty
Kwani ninyi mnavyoulizwa kwamba mtume wenu kitendo alichokifanya cha kuoa katoto kadogo(bi aisha) kakiwa na miaka 6 kwa Sheria za Tanzania mtume wenu angekumbwa na kosa gani mahakamani, huwa mnasema nini?
 
Huu ni ibabaishajiii ndugu zangu maana ukiangalia hata huyo Yesu maana wa mariam mnasema kafa msalabani sijui nn lakin ni uzushi tuuu ukiangalia kwanza huyo Yesu mwana aa Maria hakuwahi kuingia kanisan hata siku moja pili hakuna kwenye biblia hakuna dini Ukristo wala wakiristo sasa kama Yesu hakuwahi kuingia kanisan kipindi yupo je nyie mnaingia kanisan kwa mfano wa mtume gani kuwahi makin wazee wangu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wazee tuwekane wazii wazee mbona kwenye hiii biblia hakuna sehem ambayo Yesu ameingia kanisani na je kama lipo hilo andiko aliingia dheheb ganiii wazee na pili dini ya Ukristo ipo sehem kwenye biblia

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimesoma heading na conclusion, ushauri wangu bila kujali umeandika nini kwenye body ni kwamba kama unakubaliana na mambo ya kwaresma inabidi ukubali kupakwa majivu, hauwezi kuzitenganisha practices hizi mbili.

Au la ukendelea mbele zaidi, kama haukubaliani na kupakana majivu, utaishia kutupilia mbali kwaresma ambayo tayari naona unaquestion qualities zake.
 
Niseme tu ukweli kwamba kiasi fulani nakereka na hii imani ya kuchorana chorana na majivu kwa hii siku inaitwa Jumatano ya majivu.

Hebu nieleweshwe labda nikielewa ntaiona sawa..

=======

UPDATES:

IFAHAMU JUMATANO YA MAJIVU

UTANGULIZI
Jumatano ya majivu ni mwanzo wa kipindi cha kwaresima katika kanisa. Ni ishara ya kuanza kwa siku arobaini za kutafakari kwa undani fumbo kuu la upendo wa Mungu linalofunuliwa kwa kujitoa kwake na kufa msalabani, kifo cha aibu ili kuichukua aibu yetu. Mama kanisa anatupatia kipindi hiki ili tuweze kutafakari njia na mienendo yetu.


KWA NINI TUNAPAKWA MAJIVU?
Majivu ni ishara ya majuto, nayo hufanywa visakramenti kwa kubarikiwa na kanisa. Tunapopakwa majivu katika paji la uso hutusaidia kutafakari na kutukumbusha kuwa wanadamu sisi tu mavumbi na mavumbini tutarudi. Hutukumbusha zaidi kuwa maisha ya hapa duniani tunapita na safari yetu itakamilika pale tutakapoungana na Bwana na mwokozi wetu katika ufalme wako.
Angalia; Isaya 61:3, Ester 4:1-3, Yeremia 6:26, Ezekieli 27:30, Mathayo 11:21 na Luka 10:13


KWA NINI MAJIVU YAPAKWE KATIKA PAJI LA USO NA SI PENGINEPO?
Ishara yoyote iwekwayo katika paji la uso huonesha umiliki (soma Ufunuo 7:3, Ufunuo 9:4, Ufunuo 14:1, Ezekieli 9:4-6, ). Tunapochorwa ishara ya msalaba katika paji la uso ni ishara kwamba sisi tupo chini yake yeye aliyekufa msalabani kwa ajili yetu.
Hali kadhalika hutukumbusha ishara ya msalaba tuliyochorwa na mafuta matakatifu siku ya ubatizo wetu, hutukumbusha ahadi tuliyoiweka siku hiyo ya ubatizo na kutuita tuishi maisha ya utakatifu


MANENO ANAYOTAMKA PADRE YANA MAANA GANI?
Tunapopakwa majivu Padre husema; Mwanadamu kumbuka u mavumbi na mavumbini utarudi AU Tubuni na kuiamini Injili.
Maneno haya kwa upande mmoja hutukumbusha tunapoelekea, tusisikitike kwamba siku moja tutarudi mavumbini bali tuwe na furaha kwani wakati miili yetu unarudi mavumbini roho zetu zitakwenda kuungana na Mungu Baba mbinguni.
Hivyo maandalizi tunayoalikwa kuyafanaya si maandalizi ya kuelekea mavumbini bali maandalizi ya kuelekeza roho zetu mbinguni. Ndio maana pia twaambiwa tubuni na kuiamini Injili.


MAJIVU HUTOKA WAPI?
Majivu tunayopakwa hutoka katika matawi yaliyotumika katika jumapili ya matawi ya mwaka jana. Majivu haya hubarikiwa na kuwa visakramenti. Hivyo majivu yanapoashiria toba na majuto pia hutukumbusha wema wa Mungu na utayari wake wa kutusamehe.


KWA NINI TUNATUMIA MATAWI YA JUMAPILI YA MATAWI?
Matawi haya yalimkaribisha Yesu Yerusalemu akiwa tayari kufa kwa ajili ya dhambi zetu, yalimpokea mfalme kwa furaha na shangwe kuu. Matawi haya yanapochomwa na sisi kupakwa majivu yetu yanatukumbusha kuwa ni kwa ajili ya dhambi zetu Mungu alimtoa mwanae wa pekee kufa msalabani kwa ajili ya dhambi zetu sisi wanaadamu. Hivyo hututafakarisha kuacha dhambi.

KANISA LIMEKATAZA NINI SIKU YA JUMATANO YA MAJIVU?
Tumekatazwa kula chakula siku ya Jumatano ya Majivu na kula nyama siku ya Ijumaa Kuu katika Amri ya Pili ya Kanisa.

NANI ANALAZIMA KUFUNGA SIKU YA JUMATANO YA MAJIVU NA KWARESMA?
Kila Mkristo aliyetimiza miaka 14 na zaidi anapaswa kufunga kula nyama (Ijumaa kuu) na mwenye miaka zaidi ya 21 kufunga chakula Jumatano ya Majivu

TUNAPOSEMA KUJINYIMA WAKATI WA KWARESMA TUNAMAANA GANI?
Kujinyima ni kujikatalia kitu ukipendacho mfano nyama, pombe, sigara, muziki, safari, maongezi n.k.

MWISHO
Wakati wa Kwaresma Waamini wanapaswa kujitakasa zaidi kwa kusali, kufunga, toba na matendo mema

Kipindi cha Kwaresima ni fursa makini ya kumkimbilia Mwenyezi Mungu, kwani kwa njia ya dhambi wamejikuta wakiwa mbali na Uso wa huruma ya Mungu, kiasi hata cha kupoteza imani na matumaini kwa Mwenyezi Mungu. Hii ni changamoto ya kumpenda Mungu na jirani badala ya kukumbatia malimwengu yanayoendelea kuwatumbukiza katika utupu wa maisha ya kiroho. Kwaresima ni kipindi cha waamini kukimbilia na kuambata huruma ya Mungu inayoganga na kuponya dhambi. Ni wakati wa sala, upendo na kufunga.
Jamani mbona wazungu hawapakai majivu, hata kanisani hawaendi!!! Yaani kabisa kabisa hawana time na kanisa!

Siku ya Jumapili kengele ikilia unaweza kuwaona watu labda wawili au wanne kibibi na kibabu pair mke na mume wake either 1 pair or 2 pairs! kanisa zima watu wawili au watu wanne na padri basi! Kanisa lote tupu hakuna watu! Wazungu hawaendi kanisani. Siku utakayowakuta kanisani ni siku atakayokufa mtu familia na watu wa karibu wachache sana wanakwenda na marehemu kanisani wamevaa nguo nyeusi wote wanaume wanawake All black top to toe!

Makanisa mengi sana yanapigwa mnada yanauzwa Inageuka kuwa Bar and Club! sehemu ya starehe, watu wanaingia kunywa, kucheza n.k...

Ibada ya wazungu ni Bars, Clubs, na Mpira! huko hata kama ni usiku kucha au mchana kutwa watakuwepo utawakuta! ni kama Ibada jinsi wanavyousudu!

Huwa najiuliza hivi hawa wazungu kwa nini wao hawafanyi Ibada hawaendi kanisani? na wao ndio walituletea Dini Africa?
 
Mungu yupi atakaemuadhibu?? Mungu wa Papa as naeongoza makasisi wanaowaingilia watoto na kusabisha Pope kuomba msamaha kila mara??
Yaaniii nililia sana Ipo siku niliona kwenye Tv Roma Italy Ipo sehemu kuna uwanja mkubwa na kuna kanisa kubwa sana na ndani ya hilo kanisa ulifunguliwa mlango mkubwa akatoka Pop akasalimia watu waliokuwa nje kwenye uwanja mkubwa. Ndani ya kanisa walikuwepo Watoto wadogo wa kiume wengi rika lao baina ya miaka tuseme 9-12 hivi.... wapo kwa ndani kwenye hilo kanisa kubwa halafu Pop alipomaliza kusalimia watu akafunga mlango na watoto wapo ndani! watu waliokuwepo nje kwenye hilo eneo la Kanisa wote walishangaa kwa sauti! Nilijiuliza sana kuhusu watoto wale wa Kiume
 
Namuunga mkono aliyesema ukristu utaisha. Ukristu umesukwa kiujanjaujanja na wazungu, wakatuletea waafrika eti tufunge Macho kwa kusali ili watunyonye. Maadamu siamini katika ufufuko nipo huru kukiamini ninachokijua kwa roho yangu. Kama imani yangu ni mlima Kilimanjaro basi nitafika kwa muumba kwa imani yangu. Ole wao waliozoea kula kwa kutumia ukristu kwani nyakati za ukristu zinakaribia ukingoni
Hivi unajua hata hao Wazungu hawaendi kanisani? Yaani hawaendi jamani.... hawana time kabisa na kanisa na cha kushangaza zaidi wengi wao hata hawaamini MUNGU! wanasema hii yote ni NATURE tu! Hakuna MUNGU!

Kingine cha kushangaza Ikikaribia mwisho wa mwaka kuanzia mapema sana mwezi wa 9 shangwe za Chrismas na shamra shamra zake sijawahi kuona! kila mahali kunapambwa kwa mataa, Father Xmas na Santa kila mmoja anajitahidi awe nae nyumbani kwake pirikapirika za shopping ndio usiseme! n.k...
Swali hawa hata kanisani hawataki kwenda, MUNGU wengi wao hawaamini Lakini mbona wanashangwe hivi tena mapema sana?
 
Yesu hakuacha kanisa wala hakuwahi kuanzisha kanisa, hivyo ni uwongo uliokithiri kudai kwamba Roma ndio kanisa mama aliloacha Yesu, in short Waroma/Wakatoliki ni mwendelezo wa dini ya Mafalsayo na masadukayo ,dini zile za mapokeo ya asili ambayo ndio waliokuwa wakimpinga saana Yesu hadi wakamuua na wakatunga uwongo kwamba hakufufuka bali aliibiwa mwili wake kabirini. Ukatoliki ni ka mfumo tu kaliko kinyume na Yesu / Mungu Ila kamejificha ficha ktk baadhi ya maandiko
Ni kweli kabisa! Yesu ni Myahudi kwao Israel, na Wayahudi Wanasali kwenye Sinagogi, Kanisani akatafute nini? hakuwahi kuacha kanisa wala hakuwahi kuanzisha kanisa.

Wayahudi hawaitambui hata hiyo Christmas!
Hawaitambui 25.12 ya kila mwaka ni sikukuu ya kuzaliwa Yesu! Huwa hawasherehekei jamani nyie chunguzeni Ikiwezekana muwaulize mtapata ukweli wote!

Yesu sio mzungu! wala hakutoka Italy/Ulaya.

Yesu asili yake ni Myahudi/Jewish kutoka Israel.
 
Back
Top Bottom