FairPlayer
JF-Expert Member
- Feb 27, 2006
- 4,145
- 716
Jamani nimeona hii habari wala sijaielewa:
Gazeti ‘The Biggest IQ' Ijumaa Wikienda, halina cha kupoteza kwa kuthubutu kuondoa wingu hilo na kueleza kinagaubaga kuhusu tukio zima kwa kuweka hadharani maelezo ya pande zote mbili na jinsi Jeshi la Polisi Kanda ya Dar chini ya Kamanda Suleiman Kova, lilivyo hoi kiasi cha kuchelewa kupata hatma.
Gazeti ndugu na hili la Ijumaa lilikuwa la kwanza kuripoti habari ya Miss Tanzania Top 10 mwaka 2008 – 09 (jina linaendelea kuhifadhiwa kwa sababu za kimaadili) kubakwa baada ya kuleweshwa na Patrick.
Ijumaa Wikienda linakwenda mbele zaidi kwa kuchambua utata mkubwa ambao unalizingira tukio zima kiasi cha kulipa msukosuko Jeshi la Polisi ambalo mpaka leo limeshindwa kuchukua uamuzi wa kuifikisha kesi hiyo kwa Pilato a.k.a mahakamani.
Tukio hilo la Miss kubakwa, linadaiwa kuchukua nafasi Machi 13, 2010 (Jumapili) lakini mpaka leo Machi 22, 2010 ikiwa ni siku tisa baadaye, kesi hiyo haijafikishwa mahakamani na inaendelea kuzungushwa polisi.
Kitendo cha kuzungushwa polisi bila kufikishwa mahakamani, kumekuwa na taswira yenye shaka kwamba huenda zinafanyika jitihada za kulimaliza shauri hilo kabla ya kufika mahakamani.
Endapo hilo litafanikiwa, bila shaka Jeshi la Polisi litakuwa limetenda dhambi kwa sababu sheria inakataza kwa kesi za ubakaji na mauaji kuzungumzwa achilia mbali kumalizwa nje ya Mahakama.
Uchunguzi wa Ijumaa Wikienda umebaini kauli tata zinazopishana kutoka pande mbili yaani kwa mlalamikaji na mtuhumiwa, pia mazingira ya kitendawili kigumu kuteguka yanayoelezwa na mlalamikaji ambaye ni Miss Tz.
MAELEZO KUTOKA KWA MISS TZ
Kauli za Miss Tz kama alivyosimulia na maelezo yake kuhifadhiwa kwenye kitabu cha Ripoti za Polisi (Report Book au kwa kifupi RB) na katika faili la mpelelezi wa kesi ni kwamba mrembo huyo alibakwa baada ya kuleweshwa.
Mrembo huyo ambaye alipitia kitongoji cha Dar City Centre na Kanda ya Ilala, akiwa na kampani ya ‘mashosti' zake watatu, siku ya tukio, walikuwa ‘wakipombeka' kwa vileo vya bei mbaya ndani ya Hoteli ya Sea Cliff, Oysterbay, Dar es Salaam.
Wakiwa wanapombeka, Patrick aliungana nao huku naye akiwa ameshika pombe yake na baada ya muda, mrembo mwingine mwenye asili ya Bara la Ulaya alijumuika nao, hivyo kutimiza timu ya watu sita.
Baada ya kugida kinywaji huku wakiongea stori za hapa na pale, likaja wazo la wao kwenda Club Bilicanas ‘Billz' ambapo wote waliingia kwenye gari la Patrick na safari ya kuelekea klabu hiyo iliyopo Posta Mpya, Dar ikaanza.
Alieleza kwamba walipofika Billz, warembo hao walishuka na kuingia klabu huku Patrick akibaki kwenye gari lakini baada ya muda naye aliteremka, akafunga ‘motokaa' lake na kuingia ‘mjengoni'.
Miss huyo alieleza polisi kuwa baada ya Patrick kuingia ndani ya klabu, aliwafuata na kuwauliza kama wapo tayari kwa ofa yake ya vinywaji lakini warembo hao wakadai bado wanayo ‘stoko' waliyotoka nayo Sea Cliff, hivyo zikiisha ataruhusiwa kuwanunulia.
Inaelezwa kuwa baada ya kauli hiyo, Patrick aliondoka lakini aliporudi alikuwa na kinywaji kingine kinachoingiza kilevi mwilini (jina tunaliminya) kikiwa ndani ya glasi ambacho alimkabidhi mrembo huyo ambapo baada ya kupiga funda kadhaa alianza kulegea.
Mrembo huyo alieleza kuwa palipopambazuka, alijikuta akiwa amelala kitandani kwenye chumba asichokijua kabla ya kukutanisha macho na Patrick ambaye bila kuficha alijisifu kwamba alimuingilia kimapenzi tena akishirikiana na vijana wengine watatu.
Miss Tz huyo ambaye yupo ‘sexy' kimuonekano, alisema kuwa baada ya majibu hayo ya Patrick, ilibidi amlaghai kwa maelezo kuwa amemkubalia waendelee kuwa wapenzi kwa dhati badala ya kubakana, hivyo akamuomba waongozane hadi nyumbani kwao, Upanga, akamtambulishe kwa wazazi wake.
Aliongeza, nyumba aliyobakwa ipo Mbezi Beach, hivyo walisafiri hadi Upanga ambako alimkaribisha Patrick sebuleni, kisha yeye akaenda kuteta na ndugu zake kuhusu unyama aliotendewa.
Alisema, baada ya kuwaeleza ndugu zake, walimkamata Patrick hadi Kituo Kidogo cha Polisi Upanga kabla ya kurushwa Kituo cha Selander Bridge ambako kesi hiyo ilipokelewa na kupewa nambari SBR/RB/470/2010 KUBAKWA.
Baada ya kufika Selander Bridge, mrembo huyo alitoa maelezo kwamba alitendewa ubakaji Mbezi Beach, hivyo kesi hiyo ilihamishiwa Kituo cha Polisi Kawe na kuripotiwa kwa nambari KW/RB/2325/2010.
MAELEZO YA PATRICK
Katika kufuatilia mbivu na mbichi, gazeti hili lilizungumza na Patrick ambaye alisema kuwa yeye hakumbaka mrembo huyo, isipokuwa kesi imetengenezwa kwa lengo la kujinufaisha kimaslahi.
Patrick alisema: "Stori ipo hivi, nilikutana na … (anamtaja jina mrembo huyo) Sea Cliff Hotel baadaye tukaenda Bilicanas. Mimi nafahamiana naye kwa muda na nimekuwa nikimsaidia mambo mengi kwa sababu sisi wote ni wanamitindo.
"Tuliachana Bills mimi nikarudi nyumbani kwangu, asubuhi kwenye saa tano nilipokea simu ya … (anataja tena jina la mrembo) akiniomba niende nyumbani kwao kwa sababu ana shida na mimi.
"Kwa sababu tunafahamiana sikuwa na tatizo, nilikwenda na nilipofika nyumbani kwao ilikuwa ni majira ya saa saba mchana. Alinikaribisha vizuri nikaketi lakini nikiwa sebuleni aliingia mwanamke mmoja ambaye nilikuja kugundua ni mama yake.
"Yule mwanamke aliniambia kuwa yeye ni mwanamke wa kirashia, kwahiyo ni lazima atanionesha kazi kwa kitendo cha mimi kumbaka mwanaye, nikashangaa, nikauliza kumbaka nani? Akaniambia nimembaka … (anataja tena jina la mrembo).
"Hapo hapo … (jina la miss) akanigeuka, wakaingia watu wengine, wanawake wawili na mabaunsa wawili ambao walianza kunipiga na kunilazimisha nikubali kuwa nimembaka … (jina), vinginevyo wangeniua.
"Kutokana na ukweli kwamba walikuwa wamenipiga sana ilibidi nikubali, baada ya hapo wakaniambia ni lazima niandike maelezo ya kukiri na ni lazima nitoe faini.
"Waliniambia nikubali kulipa dola 5,000 (kama shilingi 6,700,000) lakini mimi nikasema naweza kulipa 1,000,000. Wakasema nilipe pale pale ‘keshi', mimi nikawaambia kwa pale pesa niliyokuwa nayo ni shilingi 500,000, wakachukua.
"Huku wakinipiga, walinilazimisha nisaini kwamba nitalipa hizo pesa kwa kosa la kumbaka … (jina), kwahiyo nilisaini kwa kuona hiyo ndiyo njia pekee ya kujiokoa na kipigo.
"Hata hivyo haikusaidia, wakaendelea kunipiga mpaka jioni, fikiria tangu saa saba mpaka saa moja jioni napigwa, wakatishia kunifanyia kitu kibaya zaidi, hapo nikapiga kelele nyingi za kuomba msaada.
"Unajua mazingira ya Upanga na ile nyumba, ilikuwa ngumu kwa majirani kusikia lakini baadaye walisikia, hivyo wakatoa taarifa polisi ambapo askari walifika, wakaingia ndani na kunibeba hadi kituoni.
"Pale Selander nilieleza kila kitu lakini nashangaa polisi walinigeuka, mara tukapelekwa Kawe. Tangu wakati huo nimekuwa nikiomba kesi hii iende mahakamani ili ukweli ujulikane kwa sababu mimi sijambaka… (jina).
"Na hizo picha za … (jina), walimpiga ndugu zake pale pale nyumbani kwao ili kutengeneza mazingira ili ionekane nilimpiga baada ya kumbaka. Walivunja simu zangu, wakachukua laptop kwenye gari.
"Nashangaa tangu tufike polisi, ndugu zake wamekuwa waking'ang'ania niwalipe shilingi 500,000 ili kesi iishe, hawataki iende mahakamani. Mimi nataka kesi iende mahakamani ili ukweli ujulikane. Nimenyanyswa sana, nimepigwa na nimedhalilishwa.
"Badala ya kupelekwa mahakamani, kesi yetu imepelekwa Oysterbay Polisi huko nako tumeambiwa kuna watu wawili waliwahi kupelekwa na … (jina) kwa nyakati tofauti kwa madai kwamba walimbaka lakini badala ya kwenda mahakamani, akaomba alipwe fidia, wakamalizana. Hii ni kutengeneza, sijabaka na wala sina sababu ya kubaka."
MASWALI TATA
Kwanini mrembo huyo atake fidia ya pesa kwa kubakwa? Je, kitendo cha yeye kubakwa anakilinganisha na shilingi 1,000,000 ndiyo maana ‘anakomalia' shilingi 500,000 iliyobaki?
Ndugu wa mrembo huyo walimsainisha Patrick kama ushahidi, je, ushahidi wa Kipolisi na Kimahakama, unaweza kuthibitisha tendo la ubakaji kwa sahihi badala ya vipimo vya daktari?
HEKA HEKA POLISI
Kwa ufuatiliaji wa tukio hilo wiki iliyopita, tuliweza kugundua kwamba shauri hilo limekuwa likihamishwa vituo mara kwa mara.
Lilianzia Kituo kidogo cha Polisi, Upanga, likapelekwa Selander, baadaye Kawe, likahamishiwa Oysterbay na Ijumaa iliyopita lilipelekwa Kituo cha Wazo Hill lakini baadaye Patrick na Mrembo waliitwa Kituo Kikuu cha Dar (Central).
Central, kikao kikuu kilifanyika kwa vigogo wenye nyota zao kuzungumza na mrembo huyo pamoja na Patrick hasa baada ya gazeti ndugu na hili la Ijumaa, kuripoti habari hii kwa mara ya kwanza.
Kikao kilichukua muda mrefu na ilipofika machweo, Patrick alibanwa nyuma ya nondo (mahabusu) ili kurahisisha upelelezi wa kesi kuchukua nafasi ya mafanikio.
KUTOKA IJUMAA WIKIENDA
Hapa kuna utata na ili haki itendeke, shauri hili ni vema likafika mahakamani. Kama mrembo huyo katendwa basi Patrick ashughulikiwe kulingana na sheria za nchi zinavyoongoza.
Ikiwa mrembo huyo na familia yake walifanya mtego kwa lengo la kujipatia fedha, basi naye alipie gharama ya kitendo alichofanya mbele sheria. Ieleweke kuwa hii ni Dar yenye mambo na hila nyingi. MHARIRI.
Source:http://www.globalpublisherstz.com/ijumaawikienda
Gazeti ‘The Biggest IQ' Ijumaa Wikienda, halina cha kupoteza kwa kuthubutu kuondoa wingu hilo na kueleza kinagaubaga kuhusu tukio zima kwa kuweka hadharani maelezo ya pande zote mbili na jinsi Jeshi la Polisi Kanda ya Dar chini ya Kamanda Suleiman Kova, lilivyo hoi kiasi cha kuchelewa kupata hatma.
Gazeti ndugu na hili la Ijumaa lilikuwa la kwanza kuripoti habari ya Miss Tanzania Top 10 mwaka 2008 – 09 (jina linaendelea kuhifadhiwa kwa sababu za kimaadili) kubakwa baada ya kuleweshwa na Patrick.
Ijumaa Wikienda linakwenda mbele zaidi kwa kuchambua utata mkubwa ambao unalizingira tukio zima kiasi cha kulipa msukosuko Jeshi la Polisi ambalo mpaka leo limeshindwa kuchukua uamuzi wa kuifikisha kesi hiyo kwa Pilato a.k.a mahakamani.
Tukio hilo la Miss kubakwa, linadaiwa kuchukua nafasi Machi 13, 2010 (Jumapili) lakini mpaka leo Machi 22, 2010 ikiwa ni siku tisa baadaye, kesi hiyo haijafikishwa mahakamani na inaendelea kuzungushwa polisi.
Kitendo cha kuzungushwa polisi bila kufikishwa mahakamani, kumekuwa na taswira yenye shaka kwamba huenda zinafanyika jitihada za kulimaliza shauri hilo kabla ya kufika mahakamani.
Endapo hilo litafanikiwa, bila shaka Jeshi la Polisi litakuwa limetenda dhambi kwa sababu sheria inakataza kwa kesi za ubakaji na mauaji kuzungumzwa achilia mbali kumalizwa nje ya Mahakama.
Uchunguzi wa Ijumaa Wikienda umebaini kauli tata zinazopishana kutoka pande mbili yaani kwa mlalamikaji na mtuhumiwa, pia mazingira ya kitendawili kigumu kuteguka yanayoelezwa na mlalamikaji ambaye ni Miss Tz.
MAELEZO KUTOKA KWA MISS TZ
Kauli za Miss Tz kama alivyosimulia na maelezo yake kuhifadhiwa kwenye kitabu cha Ripoti za Polisi (Report Book au kwa kifupi RB) na katika faili la mpelelezi wa kesi ni kwamba mrembo huyo alibakwa baada ya kuleweshwa.
Mrembo huyo ambaye alipitia kitongoji cha Dar City Centre na Kanda ya Ilala, akiwa na kampani ya ‘mashosti' zake watatu, siku ya tukio, walikuwa ‘wakipombeka' kwa vileo vya bei mbaya ndani ya Hoteli ya Sea Cliff, Oysterbay, Dar es Salaam.
Wakiwa wanapombeka, Patrick aliungana nao huku naye akiwa ameshika pombe yake na baada ya muda, mrembo mwingine mwenye asili ya Bara la Ulaya alijumuika nao, hivyo kutimiza timu ya watu sita.
Baada ya kugida kinywaji huku wakiongea stori za hapa na pale, likaja wazo la wao kwenda Club Bilicanas ‘Billz' ambapo wote waliingia kwenye gari la Patrick na safari ya kuelekea klabu hiyo iliyopo Posta Mpya, Dar ikaanza.
Alieleza kwamba walipofika Billz, warembo hao walishuka na kuingia klabu huku Patrick akibaki kwenye gari lakini baada ya muda naye aliteremka, akafunga ‘motokaa' lake na kuingia ‘mjengoni'.
Miss huyo alieleza polisi kuwa baada ya Patrick kuingia ndani ya klabu, aliwafuata na kuwauliza kama wapo tayari kwa ofa yake ya vinywaji lakini warembo hao wakadai bado wanayo ‘stoko' waliyotoka nayo Sea Cliff, hivyo zikiisha ataruhusiwa kuwanunulia.
Inaelezwa kuwa baada ya kauli hiyo, Patrick aliondoka lakini aliporudi alikuwa na kinywaji kingine kinachoingiza kilevi mwilini (jina tunaliminya) kikiwa ndani ya glasi ambacho alimkabidhi mrembo huyo ambapo baada ya kupiga funda kadhaa alianza kulegea.
Mrembo huyo alieleza kuwa palipopambazuka, alijikuta akiwa amelala kitandani kwenye chumba asichokijua kabla ya kukutanisha macho na Patrick ambaye bila kuficha alijisifu kwamba alimuingilia kimapenzi tena akishirikiana na vijana wengine watatu.
Miss Tz huyo ambaye yupo ‘sexy' kimuonekano, alisema kuwa baada ya majibu hayo ya Patrick, ilibidi amlaghai kwa maelezo kuwa amemkubalia waendelee kuwa wapenzi kwa dhati badala ya kubakana, hivyo akamuomba waongozane hadi nyumbani kwao, Upanga, akamtambulishe kwa wazazi wake.
Aliongeza, nyumba aliyobakwa ipo Mbezi Beach, hivyo walisafiri hadi Upanga ambako alimkaribisha Patrick sebuleni, kisha yeye akaenda kuteta na ndugu zake kuhusu unyama aliotendewa.
Alisema, baada ya kuwaeleza ndugu zake, walimkamata Patrick hadi Kituo Kidogo cha Polisi Upanga kabla ya kurushwa Kituo cha Selander Bridge ambako kesi hiyo ilipokelewa na kupewa nambari SBR/RB/470/2010 KUBAKWA.
Baada ya kufika Selander Bridge, mrembo huyo alitoa maelezo kwamba alitendewa ubakaji Mbezi Beach, hivyo kesi hiyo ilihamishiwa Kituo cha Polisi Kawe na kuripotiwa kwa nambari KW/RB/2325/2010.
MAELEZO YA PATRICK
Katika kufuatilia mbivu na mbichi, gazeti hili lilizungumza na Patrick ambaye alisema kuwa yeye hakumbaka mrembo huyo, isipokuwa kesi imetengenezwa kwa lengo la kujinufaisha kimaslahi.
Patrick alisema: "Stori ipo hivi, nilikutana na … (anamtaja jina mrembo huyo) Sea Cliff Hotel baadaye tukaenda Bilicanas. Mimi nafahamiana naye kwa muda na nimekuwa nikimsaidia mambo mengi kwa sababu sisi wote ni wanamitindo.
"Tuliachana Bills mimi nikarudi nyumbani kwangu, asubuhi kwenye saa tano nilipokea simu ya … (anataja tena jina la mrembo) akiniomba niende nyumbani kwao kwa sababu ana shida na mimi.
"Kwa sababu tunafahamiana sikuwa na tatizo, nilikwenda na nilipofika nyumbani kwao ilikuwa ni majira ya saa saba mchana. Alinikaribisha vizuri nikaketi lakini nikiwa sebuleni aliingia mwanamke mmoja ambaye nilikuja kugundua ni mama yake.
"Yule mwanamke aliniambia kuwa yeye ni mwanamke wa kirashia, kwahiyo ni lazima atanionesha kazi kwa kitendo cha mimi kumbaka mwanaye, nikashangaa, nikauliza kumbaka nani? Akaniambia nimembaka … (anataja tena jina la mrembo).
"Hapo hapo … (jina la miss) akanigeuka, wakaingia watu wengine, wanawake wawili na mabaunsa wawili ambao walianza kunipiga na kunilazimisha nikubali kuwa nimembaka … (jina), vinginevyo wangeniua.
"Kutokana na ukweli kwamba walikuwa wamenipiga sana ilibidi nikubali, baada ya hapo wakaniambia ni lazima niandike maelezo ya kukiri na ni lazima nitoe faini.
"Waliniambia nikubali kulipa dola 5,000 (kama shilingi 6,700,000) lakini mimi nikasema naweza kulipa 1,000,000. Wakasema nilipe pale pale ‘keshi', mimi nikawaambia kwa pale pesa niliyokuwa nayo ni shilingi 500,000, wakachukua.
"Huku wakinipiga, walinilazimisha nisaini kwamba nitalipa hizo pesa kwa kosa la kumbaka … (jina), kwahiyo nilisaini kwa kuona hiyo ndiyo njia pekee ya kujiokoa na kipigo.
"Hata hivyo haikusaidia, wakaendelea kunipiga mpaka jioni, fikiria tangu saa saba mpaka saa moja jioni napigwa, wakatishia kunifanyia kitu kibaya zaidi, hapo nikapiga kelele nyingi za kuomba msaada.
"Unajua mazingira ya Upanga na ile nyumba, ilikuwa ngumu kwa majirani kusikia lakini baadaye walisikia, hivyo wakatoa taarifa polisi ambapo askari walifika, wakaingia ndani na kunibeba hadi kituoni.
"Pale Selander nilieleza kila kitu lakini nashangaa polisi walinigeuka, mara tukapelekwa Kawe. Tangu wakati huo nimekuwa nikiomba kesi hii iende mahakamani ili ukweli ujulikane kwa sababu mimi sijambaka… (jina).
"Na hizo picha za … (jina), walimpiga ndugu zake pale pale nyumbani kwao ili kutengeneza mazingira ili ionekane nilimpiga baada ya kumbaka. Walivunja simu zangu, wakachukua laptop kwenye gari.
"Nashangaa tangu tufike polisi, ndugu zake wamekuwa waking'ang'ania niwalipe shilingi 500,000 ili kesi iishe, hawataki iende mahakamani. Mimi nataka kesi iende mahakamani ili ukweli ujulikane. Nimenyanyswa sana, nimepigwa na nimedhalilishwa.
"Badala ya kupelekwa mahakamani, kesi yetu imepelekwa Oysterbay Polisi huko nako tumeambiwa kuna watu wawili waliwahi kupelekwa na … (jina) kwa nyakati tofauti kwa madai kwamba walimbaka lakini badala ya kwenda mahakamani, akaomba alipwe fidia, wakamalizana. Hii ni kutengeneza, sijabaka na wala sina sababu ya kubaka."
MASWALI TATA
Kwanini mrembo huyo atake fidia ya pesa kwa kubakwa? Je, kitendo cha yeye kubakwa anakilinganisha na shilingi 1,000,000 ndiyo maana ‘anakomalia' shilingi 500,000 iliyobaki?
Ndugu wa mrembo huyo walimsainisha Patrick kama ushahidi, je, ushahidi wa Kipolisi na Kimahakama, unaweza kuthibitisha tendo la ubakaji kwa sahihi badala ya vipimo vya daktari?
HEKA HEKA POLISI
Kwa ufuatiliaji wa tukio hilo wiki iliyopita, tuliweza kugundua kwamba shauri hilo limekuwa likihamishwa vituo mara kwa mara.
Lilianzia Kituo kidogo cha Polisi, Upanga, likapelekwa Selander, baadaye Kawe, likahamishiwa Oysterbay na Ijumaa iliyopita lilipelekwa Kituo cha Wazo Hill lakini baadaye Patrick na Mrembo waliitwa Kituo Kikuu cha Dar (Central).
Central, kikao kikuu kilifanyika kwa vigogo wenye nyota zao kuzungumza na mrembo huyo pamoja na Patrick hasa baada ya gazeti ndugu na hili la Ijumaa, kuripoti habari hii kwa mara ya kwanza.
Kikao kilichukua muda mrefu na ilipofika machweo, Patrick alibanwa nyuma ya nondo (mahabusu) ili kurahisisha upelelezi wa kesi kuchukua nafasi ya mafanikio.
KUTOKA IJUMAA WIKIENDA
Hapa kuna utata na ili haki itendeke, shauri hili ni vema likafika mahakamani. Kama mrembo huyo katendwa basi Patrick ashughulikiwe kulingana na sheria za nchi zinavyoongoza.
Ikiwa mrembo huyo na familia yake walifanya mtego kwa lengo la kujipatia fedha, basi naye alipie gharama ya kitendo alichofanya mbele sheria. Ieleweke kuwa hii ni Dar yenye mambo na hila nyingi. MHARIRI.
Source:http://www.globalpublisherstz.com/ijumaawikienda