Ndugu Watanzania Mimi siyo Mwandishi sana humu. Ila huwa napitaga na kusoma mijadara yenu. Ninawapongeza wote mnaotufungua akili kupitia mijadala ya humu Ndani ambayo hakika hutufanya kujua mambo mengi hasa yahusuyo Taifa .
Leo nataka kushare nanyi juu ya hili jambo la Bodi ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu. Hivi ukimya wa humu JF kukaa kimya bila kutoa tamko kwa serikali kuwanyima wadogo zetu mkopo hamjaliona? Kwa mjibu wa maelezo ya bodi yanayokinzana na ya Mh Ndalichako, waombaji walikuwa elfu 88, waliopata mkopo ni 20000.
Hebu angalia mtoto amesoma shule ya kata yenye Ada ya 20000, akaenda kidato Cha tano na 6 alikuwa analipa Ada kwa kuunga unga, yaani kuuza ndizi na viazi. Leo huyo mtoto anapelekwa Nyerere Memorial Academy Ada shilingi 1115000 unamwambia Huna mkopo unauwezo wa kujilipia. Hivi tunapeleka wapi Taifa? Ni ni Dhamira ya Ndalichako? Ni kwamba ma into zetu waende kufanya biashara ya mwili ili waishi au?
Leo nataka kushare nanyi juu ya hili jambo la Bodi ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu. Hivi ukimya wa humu JF kukaa kimya bila kutoa tamko kwa serikali kuwanyima wadogo zetu mkopo hamjaliona? Kwa mjibu wa maelezo ya bodi yanayokinzana na ya Mh Ndalichako, waombaji walikuwa elfu 88, waliopata mkopo ni 20000.
Hebu angalia mtoto amesoma shule ya kata yenye Ada ya 20000, akaenda kidato Cha tano na 6 alikuwa analipa Ada kwa kuunga unga, yaani kuuza ndizi na viazi. Leo huyo mtoto anapelekwa Nyerere Memorial Academy Ada shilingi 1115000 unamwambia Huna mkopo unauwezo wa kujilipia. Hivi tunapeleka wapi Taifa? Ni ni Dhamira ya Ndalichako? Ni kwamba ma into zetu waende kufanya biashara ya mwili ili waishi au?