High BP iliyosbabaishwa na Cholesterol nyingi

Carina

Senior Member
Jan 4, 2011
190
65
Wana jamvi,

Kuna mgonjwa kaanzishiwa dosage ya Amlodipne kwa muda wa siku 14 baada ya kuonekana pressure yake iko juu sana (178/109) wakati akisubiria vipimo vya damu ambavyo vingetoka siku 3 baadaye. Baada ya hizo siku 3, majibu yametoka na kuonekana kama mtawanyo wa mafuta (yaani cholesterol) hauko vizuri yaani HDL iko chini sana na LDL iko juu sana (samahani technical terms kidogo). Inaonekana Cholesterol kwenye kipimo cha HDL iko chini sana, dokta akamuanzishia dosage ya kupunguza mafuta kwa muda wa siku 30.

Swali ni kwamba jee akimaliza hiyo dosage ya Amlodipine (kupunguza pressure) ana haja tena ya kuendelea na hiyo dosage ya Amlodipine? kwani inavyosemekana ukishaanza dosage ya kupunguza pressure ni kwa maisha yako yote yaliyobaki ikiwa kama pressure haijulikani chanzo chake ni nini,
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom