Hifadhi ya Selous ina utajiri wa madini unaoweza kuwaondoa Watanzania kwenye ufukara na umaskini

Kiboko ya Jiwe

JF-Expert Member
Apr 7, 2020
12,698
36,099
Habarini wakuu!
Leo ngoja niandike kitu ambacho huenda kitaamsha ari ya viongozi wetu.

Binafsi mimi ni mwenyeji wa mkoa wa Ruvuma(Myao) ila nimekulia na kuzaliwa Liwale (Lindi).

Ulinzi wa hifadhi ile hasa kipindi cha masika ulikuwa duni. Hii ilisababishwa na poor infrastructure (barabara). Hivyo wakazi wa vijiji vya Mlembwe, Barikiwa, Ndapata, Mpengere, Mkundi n.k walikuwa wakiingia bila hofu na kuwinda wanyama au kuvua Samaki.

Sema tu ufahamu wa wananchi juu ya utajiri wa madini ulikuwa duni , nakumbuka mwaka 2004 Mzee mmoja aliokota mawe ya thamani 3 kwenye kijito kidogo. Baadaye akayatupa 2 na kubakiwa na moja.

Aliporudi nalo kijijini ili ampe mtoto wake achezee mtu mmoja akamwambia kuwa ile ni Mali.

Wakaenda kuliuza Mtwara kwa walanguzi wakapata hela ya kujenga nyumba na kubadili mboga.

Wakarudi porini 2015 ili wakayaokote mengine wakajaza mfuko wa Rambo wakayaleta Dar , wakatapeliwa.

Imagine waliyaokota tu juu juu.
Mzee alipobembelezwa awapeleke mabrother wanaoijua pesa alikataa akikumbuka machungu ya matapeli wa Dar.

Jamaa wakaenda kwa kubahatisha mmoja aliokota jiwe ambalo aliliuza Tunduru zaidi ya milioni 100.
Sijajua siku hizi kukoje maana nilishahama huko kusini miaka zaidi ya kumi imepita.

Hizi fedha za kizamani za Wajerumani huko ukifika kwenye zile kota za Wajerumani za zamani huko porini utaziokota mpaka uchoke.

Ma skaveta yao baada ya kupigwa kwenye First World War wameyachimbia kwenye mahandaki huko.
Huenda na Dhahabu wamezichimbia huko pia.

Serikali kupitia shirika la madini ikachunguze deeply utajiri uliojichimbia ardhini huko.

Mjerumani anaipenda Selous kuliko sehemu yoyote ile duniani.
 
Habarini wakuu!
Leo ngoja niandike kitu ambacho huenda kitaamsha ari ya viongozi wetu.
Binafsi mimi ni mwenyeji wa mkoa wa Ruvuma(Myao) ila nimekulia na kuzaliwa Liwale (Lindi).
Ulinzi wa hifadhi ile hasa kipindi cha masika ulikuwa duni. Hii ilisababishwa na poor infrastructure (barabara). Hivyo wakazi wa vijiji vya Mlembwe, Barikiwa, Ndapata, Mpengere, Mkundi n.k walikuwa wakiingia bila hofu na kuwinda wanyama au kuvua Samaki. Sema tu ufahamu wa wananchi juu ya utajiri wa madini ulikuwa duni , nakumbuka mwaka 2004 Mzee mmoja aliokota mawe ya thamani 3 kwenye kijito kidogo. Baadaye akayatupa 2 na kubakiwa na moja. Aliporudi nalo kijijini ili ampe mtoto wake achezee mtu mmoja akamwambia kuwa ile ni Mali. Wakaenda kuliuza Mtwara kwa walanguzi wakapata hela ya kujenga nyumba na kubadili mboga. Wakarudi porini 2015 ili wakayaokote mengine wakajaza mfuko wa Rambo wakayaleta Dar , wakatapeliwa.
Imagine waliyaokota tu juu juu.
Mzee alipobembelezwa awapeleke mabrother wanaoijua pesa alikataa akikumbuka machungu ya matapeli wa Dar.
Jamaa wakaenda kwa kubahatisha mmoja aliokota jiwe ambalo aliliuza Tunduru zaidi ya milioni 100.
Sijajua siku hizi kukoje maana nilishahama huko kusini miaka zaidi ya kumi imepita.
Hizi fedha za kizamani za Wajerumani huko ukifika kwenye zile kota za Wajerumani za zamani huko porini utaziokota mpaka uchoke.
Ma skaveta yao baada ya kupigwa kwenye First World War wameyachimbia kwenye mahandaki huko.
Huenda na Dhahabu wamezichimbia huko pia.
Serikali kupitia shirika la madini ikachunguze deeply utajiri uliojichimbia ardhini huko.
Mjerumani anaipenda Selous kuliko sehemu yoyote ile duniani.
Mkuu karibu sana Liwale nipo hapa Mpiga miti..uliyoyasema hapo yote ni kweli
 
Hawa vijana wa 98 hawawezi kiamini haya tuyasemayo
Wasikuumize kichwa, Selous kuna sehemu ni kama Kilometers 30 kutokea barikiwa kijijini ile sehemu ukubwa wake sawa na uwanja wa ndege hapaoti nyasi wala mmea wowote hauwezi kuota pale mjerumani alichimbia chini makontena na baadhi ya Mali zake pale Ukiwa na Gps pale haiacsess chochote
 
Ndio maana anamuandaa Lissu awe rais ili waje wajibebee mali kirahisi!
Mungu hamtupi mja wake Wanawake 19 wameiua chadema kama maandiko yasemavyo.
Wewe ni kiazi kwa taarifa yako Hifadhi zote nchini asilimia 70 ya uendeshaji zinafadhiliwa na mjerumani huyo unayemtukana, Hiyo Selous yenyewe baada ya kugawanywa kuwa nyerere National Park saivi imebaki na kanda tatu za kiindeshaji zenye ukubwa wa kilomita za mraba elfu ishirini ambazo ni kanda ya liwale, kingupira na miguruwe kanda zote hizo kila kanda ina gari zaidi ya sita za askari kufanyia doria magari yote hayo hamna gari hata moja ya serikali zote ni ufadhili wa mjerumani na ndie anazifanyia hadi service kila MWezi huo ni mfano tu nimekupa wa Selous bado Serengeti, Gombe, Mahale na hifadhi zingine Serikali ikiachiwa iendeshe hayo mapori haiwezi hata siku moja
 
Hao wafanyakazi wa hiyo hifadhi wao ni vipofu?

Wao ndiyo wangekuwa wa kwanza kutajirika na hii habari isingekuwa ngeni.

Labda unazungumzia hadithi za Selous ya kabla ya ukoloni,hakuna mahali mzungu aliacha mali ya kuokota juu tu kote alikopita.

Too good to be true!
 
Hizi story za Mali za wajerumani naona zimekuwa habari kubwa hapa JF cha kushangaza hakuna aliyefanikiwa kupata mali hizo
Mali zipo mkuu kuna sehemu Selous mjerumani kaacha masanduku ya mali sehemu za maficho ambapo ukifika sanduku la Mali unaliona lakini huwezi kulibeba kutokana na uchawi aliotumia mjerumani kuuficha
 
Wasikuumize kichwa, Selous kuna sehemu ni kama Kilometers 30 kutokea barikiwa kijijini ile sehemu ukubwa wake sawa na uwanja wa ndege hapaoti nyasi wala mmea wowote hauwezi kuota pale mjerumani alichimbia chini makontena na baadhi ya Mali zake pale Ukiwa na Gps pale haiacsess chochote
Mjerumani aliondolewa nchi kabla ya uwepo wa shipping containers, 1950s.
1950s aliyekuwepo nchini alikuwa Mwingereza.

Sasa huyu mjerumani alifukia containers lini?? 🤣 🤣
Hapa wapo wanaotafutwa, mie simoo!

Ndukiiii🏃‍♂️🏃‍♂️🏃‍♂️🏃‍♂️🏃‍♂️🏃‍♂️🏃‍♂️🏃‍♂️🏃‍♂️🏃‍♂️

Everyday is Saturday...............................😎
 
Hao wafanyakazi wa hiyo hifadhi wao ni vipofu?

Wao ndiyo wangekuwa wa kwanza kutajirika na hii habari isingekuwa ngeni.

Labda unazungumzia hadithi za Selous ya kabla ya ukoloni,hakuna mahali mzungu aliacha mali ya kuokota juu tu kote alikopita.

Too good to be true!
Shahidi za Mali kuwepo zipo mkuu sema hatuwezi kufunguka sana, kuhusu wafanyakazi kuwa vipofu utasema hadi kwamba kwanini Maaskari wanakubali kuwalinda tembo na faru ilhali akimuua moja tu akauza meno tayari ametoka kimaisha
 
Hutu tuvijana tukishakula tukashiba basi tunaaanza kuanzisha stories za paukwa pakawa. Yaani kajamaa kanaandika utadhani kanaandikia darasa wenzie. Kanazungumzia aliokota mawe....akaenda uza....just like that. Mjerumani alifukia makontena ...just like that. Nyie darasa la saba hamjaanza kuwa busy? Siku mkila wali nyama mnashusha nyuzi nyingi sana humu.
 
Back
Top Bottom