Von Bismarck
JF-Expert Member
- Jul 11, 2018
- 3,073
- 6,251
Kwanza nianze kwa kuwapongeza askari wa hifadhi za wanyamapoli walio waadilifu, kwa kuendelea kusimamia kulinda urithi wa maliasili tulizo nazo ikiwemo hifadhi ya Taifa ya rubondo.
Kwa wasio ifahamu rubondo ni kisiwa kinachopatikana ndani ya ziwa Victoria. wilayani chato, Mkoani Geita.
Naweza kusema kwa ushahindi ni moja ya hifadhi ambayo imepoteza watanzania wengi sana kuanzia maeneo ya kasenda, muganza, kibehe, nyamilembe, Nkome na maeneo mengine ndani ya mwambao wa ziwa hasa mkoa wa geita.
Vija wengi wameuwa kwa mateso ya kupigwa risasi, kuangikwa kwenye miti, kufungwa mawe na kuzamishwa ziwani na hao wanaojiita askari gemu.
Familia nyingi zimewapoteza Baba zao, kaka zao , waume zao ( maeneo hayo niliyoyataja yanaongoza kwa wanawake waliopoteza waume zao)..kweli Magufuli Mungu anakuona huko uliko
Kwa kipindi hiki hali ipo hivi.
Unapokamatwa ndani ya ziwa maeneo ya rubondo hasa wavuvi unapewa mateso makali kama kuvunjwa miguu na badae wanaakupiga faini ya 500,000 -600,000 au zaidi ili uachiwe na mateso umepata.
Hali yaa ukaamataji imekuwa ni kero kipindi hichi cha mwezi wa December
Wavuvi wanafatwa uraini (nje kabisa ya mipaka ya hifadhi) wanachukuliwa kama majangili.
nimeshuhudia leo magemu wakiwakata watu waliokuwa wanaendelea na uvuvi nje ya mipaka ya hifadhi, majira ya asubhi nikiwa eneo la mwembeni- kasenda.
Rai yangu kwa mkuu wa hifadhi Rubondo.
Ukamataji wa majangili uzingatie taratibu naa sheria zinazohusika.
Waliokamatwa leo maeneo ya kasenda hao watu wachiwe, askari wako wamekuwa kero kuwavutia wavuvi ndani ya eneo ya hifadhi wakati wa doria
Kwa wasio ifahamu rubondo ni kisiwa kinachopatikana ndani ya ziwa Victoria. wilayani chato, Mkoani Geita.
Wavuvi(majangili) wazidi kuuawa hifadhi ya kisiwa cha Rubondo
Hili si jambo la kuficha. Yapata aidha kipindi cha miezi minne sasa wavuvi wanaoingia kwenye hifadhi ya Rubondo kwa kujipatia kitoweo wanapigwa risasi na kupoteza maisha kila kukicha. Sehemu hizi zinazokizunguka kisiwa hiki cha Rubondo ambazo ni: Izumacheli, Maisome, Ikuza na Mganza, Sasa...
www.jamiiforums.com
Naweza kusema kwa ushahindi ni moja ya hifadhi ambayo imepoteza watanzania wengi sana kuanzia maeneo ya kasenda, muganza, kibehe, nyamilembe, Nkome na maeneo mengine ndani ya mwambao wa ziwa hasa mkoa wa geita.
Vija wengi wameuwa kwa mateso ya kupigwa risasi, kuangikwa kwenye miti, kufungwa mawe na kuzamishwa ziwani na hao wanaojiita askari gemu.
Familia nyingi zimewapoteza Baba zao, kaka zao , waume zao ( maeneo hayo niliyoyataja yanaongoza kwa wanawake waliopoteza waume zao)..kweli Magufuli Mungu anakuona huko uliko
Kwa kipindi hiki hali ipo hivi.
Unapokamatwa ndani ya ziwa maeneo ya rubondo hasa wavuvi unapewa mateso makali kama kuvunjwa miguu na badae wanaakupiga faini ya 500,000 -600,000 au zaidi ili uachiwe na mateso umepata.
Hali yaa ukaamataji imekuwa ni kero kipindi hichi cha mwezi wa December
Wavuvi wanafatwa uraini (nje kabisa ya mipaka ya hifadhi) wanachukuliwa kama majangili.
nimeshuhudia leo magemu wakiwakata watu waliokuwa wanaendelea na uvuvi nje ya mipaka ya hifadhi, majira ya asubhi nikiwa eneo la mwembeni- kasenda.
Rai yangu kwa mkuu wa hifadhi Rubondo.
Ukamataji wa majangili uzingatie taratibu naa sheria zinazohusika.
Waliokamatwa leo maeneo ya kasenda hao watu wachiwe, askari wako wamekuwa kero kuwavutia wavuvi ndani ya eneo ya hifadhi wakati wa doria