HESLB yatoa siku tano zaidi kuomba mkopo

robbinhood

JF-Expert Member
Apr 19, 2020
524
1,521
HESLB YATOA SIKU TANO (05) ZAIDI KUOMBA MKOPO

Ni kuanzia Oktoba 1 hadi 5, 2020

Lengo ni kuwapa fursa vijana waliokuwa JKT kuomba

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) inawajulisha wanafunzi waliomaliza mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) hivi karibuni kuwa mfumo wa kuomba mkopo kwa njia ya mtandao utafunguliwa kwa siku tano (05)kuanzia kesho, Ijumaa, Oktoba 1, 2020 ili kuwawezesha kuomba mkopo.

Uamuzi huu unatokana na maombi ya wanafunzi, wazazi na walezi wa wanafunzi wahitaji ambao hawakuweza kuomba au kukamilisha maombi yao kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kujiunga na mafunzo katika kambi mbalimbali za JKT kwa mujibu wa sheria.

Aidha, katika muda huo wa siku tano, mfumo pia utakuwa wazi ili kuwawezesha waombaji ambao maombi yao yana upungufu kurekebisha kwa kuweka nyaraka sahihi ili kuiwezesha HESLB kuendelea na hatua nyingine.

“Kwa wanaorekebisha taarifa, wanapaswa kuingia katika akaunti zao walizofungua kuombea mkopo na watapata ujumbe kuhusu maeneo ya kurekebisha. Tunawasihi watumie muda huu wa siku tano kurekebisha na kukamilisha maombi yao ili kutuwezesha kuendelea na hatua inayofuata ili hatimaye wenye sifa wawezeshwe kutimiza ndoto zao,” amesema Mkurugenzai Mtendaji wa HESLB Abdul-Razaq Badru.
 
HESLB YATOA SIKU TANO (05) ZAIDI KUOMBA MKOPO

Ni kuanzia Oktoba 1 hadi 5, 2020

Lengo ni kuwapa fursa vijana waliokuwa JKT kuomba

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) inawajulisha wanafunzi waliomaliza mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) hivi karibuni kuwa mfumo wa kuomba mkopo kwa njia ya mtandao utafunguliwa kwa siku tano (05)kuanzia kesho, Ijumaa, Oktoba 1, 2020 ili kuwawezesha kuomba mkopo.

Uamuzi huu unatokana na maombi ya wanafunzi, wazazi na walezi wa wanafunzi wahitaji ambao hawakuweza kuomba au kukamilisha maombi yao kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kujiunga na mafunzo katika kambi mbalimbali za JKT kwa mujibu wa sheria.

Aidha, katika muda huo wa siku tano, mfumo pia utakuwa wazi ili kuwawezesha waombaji ambao maombi yao yana upungufu kurekebisha kwa kuweka nyaraka sahihi ili kuiwezesha HESLB kuendelea na hatua nyingine.

“Kwa wanaorekebisha taarifa, wanapaswa kuingia katika akaunti zao walizofungua kuombea mkopo na watapata ujumbe kuhusu maeneo ya kurekebisha. Tunawasihi watumie muda huu wa siku tano kurekebisha na kukamilisha maombi yao ili kutuwezesha kuendelea na hatua inayofuata ili hatimaye wenye sifa wawezeshwe kutimiza ndoto zao,” amesema Mkurugenzai Mtendaji wa HESLB Abdul-Razaq Badru.


source:
HESLB | Web
Hivi kuappeal kutaanza lini?
 
HESLB YATOA SIKU TANO (05) ZAIDI KUOMBA MKOPO

Ni kuanzia Oktoba 1 hadi 5, 2020

Lengo ni kuwapa fursa vijana waliokuwa JKT kuomba

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) inawajulisha wanafunzi waliomaliza mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) hivi karibuni kuwa mfumo wa kuomba mkopo kwa njia ya mtandao utafunguliwa kwa siku tano (05)kuanzia kesho, Ijumaa, Oktoba 1, 2020 ili kuwawezesha kuomba mkopo.

Uamuzi huu unatokana na maombi ya wanafunzi, wazazi na walezi wa wanafunzi wahitaji ambao hawakuweza kuomba au kukamilisha maombi yao kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kujiunga na mafunzo katika kambi mbalimbali za JKT kwa mujibu wa sheria.

Aidha, katika muda huo wa siku tano, mfumo pia utakuwa wazi ili kuwawezesha waombaji ambao maombi yao yana upungufu kurekebisha kwa kuweka nyaraka sahihi ili kuiwezesha HESLB kuendelea na hatua nyingine.

“Kwa wanaorekebisha taarifa, wanapaswa kuingia katika akaunti zao walizofungua kuombea mkopo na watapata ujumbe kuhusu maeneo ya kurekebisha. Tunawasihi watumie muda huu wa siku tano kurekebisha na kukamilisha maombi yao ili kutuwezesha kuendelea na hatua inayofuata ili hatimaye wenye sifa wawezeshwe kutimiza ndoto zao,” amesema Mkurugenzai Mtendaji wa HESLB Abdul-Razaq Badru.


source:
HESLB | Web
Kwani tar 1 Oct itakuwa kesho kutwa Ijumaa..?,mbona wananichanganya hawa.
Maana Leo ni Wed tar 30 sept INA maana kesho ni Thur tar 1 Oct na zoezi litabidi lianze, sasa hiyo Ijumaa niajeh..!!!
 
.
Screenshot_20201001-175233.jpg
 
Habari wana JF, naombeni kuuliza., Ivi kama kwenye application ya mkopo na mahali nilikosea na ni ya muhimu sana na nikaprint ile document kana kwamba sina uwezo wa ku-Edit tena, je nitafanyaje ili niweze kutatua ilo tatizo, au nikifika kwenye ofisi zao wataweza kunitatulia, Naombeni msaada wenu wa mawazo
 
Habari wana JF, naombeni kuuliza., Ivi kama kwenye application ya mkopo na mahali nilikosea na ni ya muhimu sana na nikaprint ile document kana kwamba sina uwezo wa ku-Edit tena, je nitafanyaje ili niweze kutatua ilo tatizo, au nikifika kwenye ofisi zao wataweza kunitatulia, Naombeni msaada wenu wa mawazo
ujumbe waliokuletea ni upi?
 
Husika na tittle, uniambie inatakiwa iweje hiyo sponsorship maana ya kwangu wameikataa.
 
Wakubwa..

Katika akaunti ya bodi ya mkopo verification result ikionyesha kwamba cheti cha kifo ni INVALID yani majina yametofautiana na ni kweli kwasababu cheti icho kilikosewa Herufi kwenye majina..

Nifanyaje kusolve tatizo
 
Back
Top Bottom