General mex
Senior Member
- May 1, 2011
- 158
- 185
Wadau mimi ni mmojawapo kati ya wale tuliokua wizara ya elimu kulalamika kuhusu kunyimwa mkopo na heslb. Kwa taarifa mpaka tulivyoondoka pale wizarani saa 12 jioni, bodi ya mikopo ilikiri kua kuna matatizo mengi yaliyojitokeza kwenye ugawaji wa mikopo. Ila kilichoamuliwa ni kwamba, wata review yale majina ya wote waliokosa mikopo ambao walikua na vigezo wapate mikopo. Ila walichoongelea sana ni kwamba watatoa taarifa kwa kila aliekosa mkopo ili ajue ni kwa nini amekosa. Kwa hyo wataongezea pale kwenye matokeo ya chuo maelezo kuonesha sababu. Baada ya hapo xaxa 2tajua cha kufanya kwa maana wamedai kuna watu form zao hazikufika ilhali kumbe wana hadi risiti za Ems! Ila suala la kwamba, mikopo itatolewa tena ama la? Wamedai ni mpaka waziri atoe tamko. Watafanya mkutano hivi karibuni. Lets hope that they will not cheat us. Amen. Nawasilisha kwenu wana jf..