HESLB wanatuibia tuliomaliza marejesho ya mkopo Elimu ya juu. Kwa kuendeleza makato licha ya kumaliza deni. Prof Mkenda Litazame.

Tozo

Member
Aug 23, 2021
76
154
Ukifika ofisi za Bodi ya Mkopo Elimu ya Juu unachokutana nacho ni foleni kubwa ya watu waliomaliza makato kusitisha mwezi mmoja au miwili na baada ya hapo ni kuanzia tena kukatwa kupitia mshahara. Ukifika kulalamika wanakupa fomu ujaze na baadae unapewa barua kwenda kwa mwajiri kusitisha. Maswali anayotakiwa Prof. Mkenda kuwauliza Hawa wapigaji. Kwanza, kwa nini tujaze formu na tupeleke barua ya kusitisha wakati Kila marejesho yanapofanyika kiasi Cha Salio la mkopo huonekana kwenye salary slip? Pili, Kwa nini hawatoi hundi ya kurejeshewa makato yaliyofanyika kimakosa papo hapo? Tatu, watarekebisha lini system yao ya kudai kurejeshewa malipo yaliyokatwa kimakosa?. Waziri wa Elimu , Mhe. Rais anaposema na hili nalo ukalitazame ulimuelewa anamaanisha nini? Hebu tembelea Bodi yako ya Mikopo Elimu ya Juu usiende kuishia kutazama tu.
 
Miezi mitatu iliyopita nilifika ofisi zao za Dodoma kulalamika. Wakaniambia niingie online kuomba refund. Nikazaja fomu. Mpaka leo hawaja verify madai yangu ya kurejeshewa 2.3M walizozidisha makato halisi. Wakati mwingine unatamani tu Mungu awapende zaidi maafisa wote wa Loan Board.
 
Wahuni tu !! Deni kweny salary slip tofauti na la kweny website nimechoka kabisa
 
Miezi mitatu iliyopita nilifika ofisi zao za Dodoma kulalamika. Wakaniambia niingie online kuomba refund. Nikazaja fomu. Mpaka leo hawaja verify madai yangu ya kurejeshewa 2.3M walizozidisha makato halisi. Wakati mwingine unatamani tu Mungu awapende zaidi maafisa wote wa Loan Board.
Hawa ni mbwa tena ni makalio kabisa. Salary slip inaonesha vizuri. Mtu ana mwaka tangu amalize wanaibuka wanaanza kukata tn. Ni wa kupiga shaba tu hawa!
 
Stupidity, kama wanajua where to start why wasijue namna ya kustopisha makato? Tunapoteza muda kufanya kazi za watu..si kuna officers wanao deal na hiyo kazi kwanini mtumishi uanze kuhangaika na makaratasi kwa muajiri badala ya ku focus na kazi wao wawasiliane na HR? Haya mambo ndio yanafanya wazungu watuchukulie poa!
 
Wanufaika wapya wa Mkopo zaidi ya elfu 20 HESLB 2022/2023 | Majina ya Waliopata Mkopo
Habari njema kwa waombaji wote wa mkopo wa HESLB, Allocation ya mkopo bechi ya kwanza sasa inapatikana mtandaoni kuangalia allocation ya mkopo Tembelea Tovuti ya HESLB ya Maombi ya Mikopo na Mfumo wa Usimamizi https://olas.heslb.go.tz/index.php/olas/Olas

Nifanye nini nikikosa mkopo kwenye bechi ya kwanza HESLB?
Kuwa mvumilivu na subiri kwa sababu bodi ya mkopo inatoa majina ya waombaji wa mkopo waliopata mkopo kwa Bechi. Bechi za majina ya waliopata mkopo ni nyingi wakati mwingine hufikia tano au sita

Je nikisubiri hadi bechi zote za majina zikatoka na ikiwa sioni jina langu, nifanye nini?
Bodi ya mikopo hufungua dirisha kwa waombaji kukata rufaa kwa hivyo ikiwa unajiona kuwa una hoja, unaweza kukata rufaa
Je, nifanye nini ikiwa sipati mkopo baada ya kukata rufaa?
  • Lipa ada ya masomo na chakula cha kujifadhili na gharama za malazi.
Naweza kuomba mkopo huku nikiendelea na masomo?

  • Ndio mwaka ujao bodi itafungua dirisha jipya la maombi
Maswali baadhi ambayo naweza kukupa msaada angalau wa majibu kuendena na uelewa wangu
Je, iwapo nilikatisha(disco) masomo nifanye nini ili niweze kupata mkopo Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu(HESLB) Soma hapa

Je, ni lazima nifuate taratibu gani ili nilipwe mkopo na Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu(HESLB)?

Ili bodi ifanye malipo, mnufaika lazima afuate taratibu hizi

1. Mfadhiliwa lazima ajiandikishe kikamilifu katika taasisi ya elimu ya Juu, vinginevyo itamfanya akose sifa ya kupokea fedha hizo.

2. Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu(HESLB) lazima ipokee maelezo ya ziada ya wanufaika. Jukumu la kutuma taarifa hizo ni la taasisi ambayo wamekubali Wanufaika na kuwasajili kikamilifu.

Nyongeza:

iwapo mnufaika wa mkopo atajiandikisha katika taasisi ya elimu ya juu ambayo ni tofauti na ile ambayo TCU ilipeleka Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu(HESLB), mnufaika hatapokea fedha za mkopo hadi aombe kupangiwa upya au Kuhamishiwa mkopo.

Ikiwa mnufaika atabadilisha programu yake aliyoichagua awali, kiasi cha mkopo wake hakitabadilika hadi aombe kutengewa tena.

Mwisho, bodi ya mikopo Huendelea kufuatilia maendeleo ya mnufaika katika Vyuo vya Elimu ya Juu mara kwa mara ili kufanya uamuzi wa malipo.

Recomended Posts

 
Back
Top Bottom