Huo utofauti ukoje?unajua Sisi wengine tupo mikoani kufika makao makuu ni mbali kidogo
Kumbuka sasa hivi VRF na penalty zimefutwa.
Hivyo, automatically kiwango cha pesa unachodaiwa kitabadilika. Hapo ndio inconsistency inapotokea. Kuna watu madeni yao ni makubwa lakini si kwa sababu ya riba au penalty bali uingizaji mbaya wa taarifa za madeni.
Verified loan statement inaonesha mchanganuo uliokamilika kama ifuatavyo
i) Ulikopeshwa shilingi ngapi.
Hapa utapewa taarifa kwa mchanganuo. Kwa mfano kiasi cha tuition fee, meals and accommodation, research fund, practical training n.k ulichokopeshwa.
ii) Umerejesha kiasi gani hadi sasa.
Hapa utaoneshwa marejesho yako ya kila mwezi. Kuna watu wanadaiwa pesa nyingi kumbe kosa ni la muajiri kuna miezi hakuwa anapeleka pesa.
Na hii inatokea hata kwa waajiriwa wa serikali pia. Kwa hiyo usijipe moyo wewe ni mwajiriwa wa serikali.
Wewe nenda tu kapate statement yako ujue hali ya mkopo wako.