Cheef Baroka
JF-Expert Member
- Apr 28, 2019
- 491
- 1,000
Wana MMU mlio wengi mnapenda thread za kulana matunda kimasihara, kuchakatana yani Ngono na bata kwa ujumla. Leo naomba tujadili mambo yakifamilia zaidi hasa zile za kiswahili. niwakumbushe wale tulopita kwenye familia za mlundikano wa ndugu, je, tunawakumbuka wale wake za kaka zetu, na mama zetu wakambo tulokuwa tunaishi nao kwenye mfumo huu wa maisha usoisha, masengenyo, magomvi, umbea, majungu na wengine huingiza hadi imani za kishirikina?. Unamchukuliaje mdada huyu anaeolewa hapa anazaa watoto wake kadhaa au wote hapa, anaanza toka binti hadi mtu mzima katika maisha haya?. Hebu tuvute kumbu kumbu hata kama si kwetu hata kwa Jirani mambo yalikuaje?
Nakuheshim sana we dada unayeishi na mawifi zaidi ya wa3, mashemeji 7, Watoto wa mawifi na mashemeji (kama krinik), baba mkwe na MAMA mkwe, shangazi/ mjomba. Nikivuta hisia nikajaribu kuvaa uhalisia wako , Sina Maneno yakukwambia ila kama umeweza kuishi katika hali hiyo nahisi hata motoni hapatakupa tabu ( natania) UBARIKIWE KULIKO WANAWAKE WOTE DUNIANI.
Afu unakuta lijanaume limeshiba ugoro na bangi linalopoka tu "Wanawake wote ni M mbwa " . Mmbwa mwenyewe kenge wewe
Nakuheshim sana we dada unayeishi na mawifi zaidi ya wa3, mashemeji 7, Watoto wa mawifi na mashemeji (kama krinik), baba mkwe na MAMA mkwe, shangazi/ mjomba. Nikivuta hisia nikajaribu kuvaa uhalisia wako , Sina Maneno yakukwambia ila kama umeweza kuishi katika hali hiyo nahisi hata motoni hapatakupa tabu ( natania) UBARIKIWE KULIKO WANAWAKE WOTE DUNIANI.
Afu unakuta lijanaume limeshiba ugoro na bangi linalopoka tu "Wanawake wote ni M mbwa " . Mmbwa mwenyewe kenge wewe