bahati93
JF-Expert Member
- Aug 6, 2015
- 1,049
- 1,906
Hapa kwetu bongo kuna vimbwanga vya kila aina ila mbali ya yote kumekuwa na tabia ya watu kuzarauliana kutokana na vipawa mbalimbali ambavyo watu wanavyo kama ulevi wa wastani na uliopindukia. Nasikitika jamii yetu imekuwa kipofu kuona mchango wa walevi kuwaona kama kwamba hawana akili na hawajui matumizi mazuri ya pesa. Wengine wanaenda mbali na kudiriki kuwaza kwamba eti bar zote zifunguliwe tu wikiendi.
Mbali na yote haya yatupasa tuwaombe walevi wanywe Zaidi kutokana na ukweli kuwa serikali inategemea kodi nyingi kutoka kwa bia na pombe sasa ukiwasumbua walevi wakagoma kunywa hio kodi uliopigia maesabu lukuki utaipata wapi au unafikiri madeski yatajijenga yenyewe.
Sasa endapo utamwona mlevi anayumba yumba usifikiri anayumba kwamba kilevi kimemkolea hapana anayumba Amani na faraja anapojua kwamba amechangia bila shurutu kodi ya taifa na hivyo kudhibitisha tz ndani ya bongo inaenda mbele kwa mbele.
Ata mimi mwenyewe nataka nianze kuwa mlevi nichangie pato la taifa haswa.
Mbali na yote haya yatupasa tuwaombe walevi wanywe Zaidi kutokana na ukweli kuwa serikali inategemea kodi nyingi kutoka kwa bia na pombe sasa ukiwasumbua walevi wakagoma kunywa hio kodi uliopigia maesabu lukuki utaipata wapi au unafikiri madeski yatajijenga yenyewe.
Sasa endapo utamwona mlevi anayumba yumba usifikiri anayumba kwamba kilevi kimemkolea hapana anayumba Amani na faraja anapojua kwamba amechangia bila shurutu kodi ya taifa na hivyo kudhibitisha tz ndani ya bongo inaenda mbele kwa mbele.
Ata mimi mwenyewe nataka nianze kuwa mlevi nichangie pato la taifa haswa.