Herufi R na L ni tatizo kwa Rais wetu, tumsaidie

Major

JF-Expert Member
Dec 20, 2007
1,865
2,439
Ni dhahiri kabisa hizi herufi mbili za R na L zinamtatiza sana Raisi wetu, Mara nyingi ktk hotuba zake amekuwa akisikika kabisa kuzikosea yaani sehemu ambayo alitakiwa kutamka neno Reli, yeye atasema Leli, tena kwa kujiamini,. Ktk Msamiati wa kiswahili neno Leli Lina maana tofauti kabisa.

Ni Mara nyingi sana amekuwa akijichanganya kuhusu herufi hizi, kwa Sisi Watanzania tunamvumilia kwa sababu ni mtu wetu, lakini Tatizo linakuja pale tu anapokuwa nje ya Nchi ambapo inabidi aongee lugha ya Kimataifa, kwa English, penye Herufi R ukibadili na kuweka L, automatic huwa inabadili maana nzima ya unachozungumzia. Na wakati mwingine inaweza hata kuwa ni matusi makubwa. Niwaombe Tu Wahusika kwa Roho safi, Wajitahidi sana kumwelekeza namna nzuri ya kutumia hizi herufi ili Mara nyingine tusije kupata aibu Kama hii inayoendelea ktk mitandao huko Zimbabwe . Pls
 
Naunga mkono hoja.
Kwanza namuunga mkono rais Magufuli kutumia lugha ya Kiswahili kila mahali hadi UN mwezi October mwaka huu, ila Kiswahili hicho kiwe ni Kiswahili fasaha.

P
Rejea
 
kwani kuna R au L wapi kwenye Hostages?
Hayo ni mengine ya kwako Bro, Mimi nazungumzia hizi herufi mbili, L na R. Naomba wahusika wafanye juu chini wahakikishe anaondokana na hili tatizo kwa manufaa na heshima kwa Nchi yetu.
 
Mkuu hayo mambo ya kawaida sana, usukumani hizo herufi zinatamkwa the same, kwa maana nyingne msukuma aloiva hatumii kabisa R bali L na pia usukumani kwa kufata mila za kisukuma hakuna majina yenye herufi ya R bali majina yote yenye mlengo huo yanapoandika kisukuma huwa ni L tu...mfano Mayala, Malando, Kabula, Milembe, Magufuli nk, so kwa kisukuma hakuna R bali kuna L..
"mwabheja bhagosha"
 
Hayo ni mengine ya kwako Bro, Mimi nazungumzia hizi herufi mbili, L na R. Naomba wahusika wafanye juu chini wahakikishe anaondokana na hili tatizo kwa manufaa na heshima kwa Nchi yetu.
Kweli, ila baada ya kufanikiwa kwenye R na L pia na haya mengine yazingatiwe sababu nayo pia yanapotosha maana.
 
mkuu hayo mambo ya kawaida sana, usukumani hizo herufi zinatamkwa the same, kwa maana nyingne msukuma aloiva hatumii kabisa R bali L na pia usukumani kwa kufata mila za kisukuma hakuna majina yenye herufi ya R bali majina yote yenye mlengo huo yanapoandika kisukuma huwa ni L tu...mfano Mayala, Malando, Kabula, Milembe, Magufuli nk, so kwa kisukuma hakuna R bali kuna L..
"mwabheja bhagosha"
Sasa kunafaida gani ya kusoma? Msomi anatakiwa aongee lugha fasaha
 
Naunga mkono hoja.
Kwanza namuunga mkono rais Magufuli kutumia lugha ya Kiswahili kila mahali hadi UN mwezi October mwaka huu, ila Kiswahili hicho kiwe ni Kiswahili fasaha.
P
Rejea
Naunga mkono hoja.
Kwanza namuunga mkono rais Magufuli kutumia lugha ya Kiswahili kila mahali hadi UN mwezi October mwaka huu, ila Kiswahili hicho kiwe ni Kiswahili fasaha.

P
Rejea
Na ikiwezekana Kama ameamua kuzungumza Kiswahili basi asichanganye na Kiingereza, kwa sababu huwa inasababisaha matatizo makubwa, kumbuka kuna wakati alitaka kusema."We are on the rite truck" lakini akakosea kutamka akasema, "we are on ze lite tlack, Kwani akiongea tu kiswahili fasaha kuna ubaya gani? Mbona Raisi wa wa China huwezi kumkuta popote akitamka neno lolote la Kiingereza!
 
18 Reactions
Reply
Back
Top Bottom