Herufi R na L ni tatizo kwa Rais wetu, tumsaidie

Hayo ni mengine ya kwako Bro, Mimi nazungumzia hizi herufi mbili, L na R. Naomba wahusika wafanye juu chini wahakikishe anaondokana na hili tatizo kwa manufaa na heshima kwa Nchi yetu.
Kwani magogoni hupajui ukawaambie?
 
Wabongo kuja na vihoja Kama Hivi hatutapiga hatua kwani hata wenye lugha yao hawaongee grammar fasaha au Wabongo mnavutia na silang za akina Obama kweli hamnazo kabisa
 
mkuu hayo mambo ya kawaida sana, usukumani hizo herufi zinatamkwa the same, kwa maana nyingne msukuma aloiva hatumii kabisa R bali L na pia usukumani kwa kufata mila za kisukuma hakuna majina yenye herufi ya R bali majina yote yenye mlengo huo yanapoandika kisukuma huwa ni L tu...mfano Mayala, Malando, Kabula, Milembe, Magufuli nk, so kwa kisukuma hakuna R bali kuna L..
"mwabheja bhagosha"
Mleta mada kasema Rais anabalidisha herufi R kuwa L na L kuwa R, ila wewe unadai wasukuma hawana herufi R kwenye maneno yao! Ina maana Magufuli siyo msukuma au una maana gani? Kama wasukuma hawatumii herefi R kwenye maneno yao, hizi R yeye anazitoa wapi? Mfano "sorution", "wewe ni mzarendo kweri kweri",
 
Wasukuma na watu wa kanda ya ziwa wote hawajui matumizi sahihi ya R na L katika misamiati fasaha ya kiswahili,jiwe bhana anazidi kutuhaibisha waTanganyika
 
Usukuma usitumike kama excuse. Akina Pascal Mayalla ni wasukuma humu mbona wanaandika vizuri?
Lugha ya kuandika ni tofauti na kuongea, hata Ph.D ya Kemia, alifanya thesis yake kwa Kiingereza cha kuandika, na akaidefend kwenye jopo la wabobezi na ikapita, lakini mwambie akahutubie kwa Kiingereza...

Hili la viongozi kuchanganya R na L, niliwahi kulizungumzia humu
P
P
 
Back
Top Bottom