Anko Sam
JF-Expert Member
- Jun 30, 2010
- 3,200
- 820
Ndugu performance ya PM haiwezi kuwa determined na kelele. Shida mnataka Pinda awe anapiga kelele kama zile za magufuli ndo mjue ni mchapa kazi - Si kweli. Kuna mtu alikuwa anajua kukuru kakara kama Lowasa? Mbona amekuja akawasaliti watanzania kwa kupiga deal la Richimond. PM ana mengi ya kufanya katika uendeshaje wa shughuli za serikali and his main tools are hekima, busara na uelewa.
Lakini ukweli HERI FISADI LOWASSA kuliko MTOTO WA MKULIMA PINDA! Lowasa alikuwa akifanya ziara sehemu wakurugenzi wa halmashauri na wakuu wa wilaya wazembe walikuwa tumbo joto. Kama angeendelea utendaji wa viongozi wengi wa kimazoea mazoea ungekwisha. Tatizo lake lilikuwa "kusaka mahela" fasta fasta. Siyo huyu Pinda amekuwa mpole mno inatia aibu mpaka analia....aaaah noma!
Nchi hii sasa hivi inataka akina-Sokoine au Mrema. Kwa hivi sasa mtu aliyekuwa anafaa sana kuwa MP ni MAGUFULI, sema wanambania tu.