Helsinki Mdebwedo.....!

Kibunango

Platinum Member
Aug 29, 2006
8,416
2,263
Bongo FC timu machachari katika jiji la Helsinki jana walifundishwa jinsi ya kucheza soka na wabongo wa Tampere maarufu kwa jina TAS... Bongo FC ambayo inajiandaa na safari ya kwenda kucheza na Kilimanjaro FC ya Sweden, ilijikuta ikiwa na wakati mgumu pale ilipufungwa bao 3-1... Wabongo wa Tampere sasa wanatuma salaam kwa Wabongo wa Vaasa wajiandae kuja na vikapu vya magoli...

Image502.jpg
Baadhi ya wachezaji wa Bongo FC wakijiandaa na mpambano wa TAS....


Image509.jpg


Image510.jpg

Wachezaji wa Tampere(TAS) wakipanga mikakati ya kutoa dozi kwa Bongo FC


Image508.jpg

Benchi la TAS


Image504.jpg
Wapenzi wa TAS wakishangilia moja ya dozi kwa Bongo FC
 
Last edited:
Hongereni sana wana TAS lakini mhh! kama wachezaji wa TAS ndio hawa(wanywaji wakubwa vileo) hao waliofungwa sijui watakuwaje
 
Kamanda Yoyo...
Hongera zimefika ila kwa niaba ya TAS napenda kukufahamisha kuwa sio wanywaji wa vileo... wao ni kutoa dozi tu...
 
shukran Kibunango,

mambo sio mabaya huko. Mti mkubwa sijamuona hapo, hakuwepo japo kushangilia, au ndio umri tena?
 
Mti Mkubwa kwa sasa hayupo helsinki....Ila matokeo ya mechi hii aliyapata jana hiyo hiyo...
 
aaaaha kumbe mshambuliaji ... give us your records losses ngapi na goli ngapi ... you never know maximo may need these records
 
TAS watarudiana na Bongo FC jumamosi tarehe 23, saa tisa jioni mjini Tampere, wote mnakaribishwa
 
FC Bongo jana ilijikuta ikipata kipigo kitakatifu cha mabao 8-1 toka kwa timu machachari ya Kilimanjaro ya Sweden. Hii ni mara ya pili kwa FC Bongo kunywea mbele ya Kilimanjaro.
Fc Bongo ambayo ilikuwa inawania kutwaa kombe la Tanzania Cup toka kwa Kilimajaro, ilijikuta ikipokea kipigo kisicho na huruma toka kwa Kilimanjaro ambao walicheza mchezo huo huku wakiwa na uchovu wa safari ya usiku mzima baharini.

Jumamosi ijayo FC Bongo watakuwa na wakati mwingine mgumu, pale watakapo cheza na timu ngumu ya Waafrika waishio katika jiji la Tampere.
 
Wabongo wa Finland choka mbaya sana aisee...hamna hata mmoja aliyekwiva bana...aaah ovyo kabisa
 
Last edited:
teheteheteheeee! duu 8-1 ni zaidi ya mdebweno, ni mpira wa chandarua [netball) au wa miguu, na-imagine wao ndio wangekuwa wametoka safari
 
Wabongo wa Finland choka mbaya sana aisee...hamna hata mmoja aliyekwiva bana...aaah ovyo kabisa


Wafini wacha wewe !!!!wabongo wanaoishi FINLAND wanaiona joto ya jiwe inayotokana na wenyeji wao,wanawapeleka mchaka mchaka usiku na mchana.
 
TAS leo wanawatembelea Fc Bongo kuwafundisha jinsi ya kucheza soka.... Kumbuka kuwa FC Bongo hivi majuzi walipewa dozi kubwa ya kumaliza malaria walipo pachikwa bao 8 kwa 1 bila huruma na Kilimanjaro ya Sweden
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom