Helikopta ya Polisi!!

kadata

Member
Nov 22, 2008
7
0
hivi kweli jeshi letu la polisi limeshindwa kuweka vijana wake maeneo muhimu ya jiji badala ya kuendelea kuichosha hii helikopta yake ambayo hata asiye na uelewa mkubwa wa vyombo vya anga anajua imeshazeeka? Si afadhali waepushe disaster kwa kununua mafuta kwa ajili ya pikipiki na gari zao badala ya huu utani wanaouendeleza!! Mtu yeyote atembelee eneo la Ubungo Stand ya mabasi madogo, na maeneo ya jirani kuanzia saa moja jioni,atashuhudia jinsi wezi wababe na wasioogopa chochote wanvyosumbua raia, lakini hakuna hata polisi mmoja!!? Tafadhali mkuu Kova, jaribu kuangalia suala hili, mambo mengine mnafanya utani mtupu!!
 
..true police wamebakiwa na helicopter moja tu nzima..walikuwaga wanategemea kuazima za jwtz ..ambao wanazo nne hati ya sita walizonunuliwa na serikali mwaka 2004[only four choppers have been delivered todate].......ambazo mbili zimeanguka[moja ilianguka wakati wajumbe wa wizara ya mazingira walipoenda kukagua ziwa natron,na nyingine wakati ikitokea doria suliavan]....zimebaki mbili ambazo zimesimamisha urukaji kwa ajili ya uchunguzi.....

ukweli ni kuwa hilo eneo unalotaja ubungo na maeneo yote ya traffic lights ..kuna uporaji wa kutisha wakti magari yanaposimama ....[simu ,side mirrors ..ets ni halali yao]
 
Ni kweli kabisa kadata! mimi nilikua nadhani jeshi letu la polisi libadilishe mfumo wa kufanya kazi kwa Kudessa!yaani kuona baadhi ya nchi zinatumia Helikopta kupambana na waharifu basi nao wanakurupuka tu, bila ya kujua gharama zinazotumika kurun operation hizo za kutumia helikopta ni kubwa kuliko uharifu wanaouzuia! maana sijaona kitu kikubwa kilichofanyika na jeshi hilo kutumia Helikopta zaidi ya kukamata watengeneza gongo na wakulima wa mashamba ya bangi wakati kuna majambazi wakubwa wanaotumia mabomu huko kagera. Pia wangeweza kutumia pikipiki na magari yao na kukomesha uharifu kwa gharama ndogo.Natunachosubiria sasa ni kutokea maafa kwa vijana wetu wa jeshi hilo wanaolazimishwa kufanya kazi kwa kutumia helikopta bila kua na uzoefu wa kutosha na uchakavu wa chombo hicho.NAOMBA WALIOPO KARIBU NA IGP MWEMA WAMSHAURI KUHUSU HILO!
 
Back
Top Bottom