Helikopta ya Barrick yapigwa jiwe

Maseke ya Meme

JF-Expert Member
Jul 11, 2007
693
905
•
Rubani apigwa jiwe jichoni akiwa angani


*Alishambuliwa kwa kombeo na wavamizi wa mgodi wa Barrick
*Alikuwa akipiga picha za eneo la mgodi kutoka juu

Na Joyce Magoti, Musoma


WATU wasiojulikana wamemjeruhi kwa kumpiga jiwe jichoni kwa kutumia kombeo rubani wa ndege iliyokuwa imekodiwa na mgodi wa Kampuni ya Barrick, North Mara, kwa ajili ya kukagua eneo la mgodi huo na kupiga picha ya eneo hilo.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Ofisa Habari wa Mgodi huo, Bw. Emmanuel Nyasigo, alisema tukio hilo lilitokea jana saa 4 asubuhi wakati ndege hiyo namba ZCHUC ikikagua na kupiga picha eneo la mgodi huo, katika kijiji cha Kewanja ikiwa kimo cha meta 50 kutoka ardhini.

Bw. Nyasigo alisema watu hao wanaodhaniwa kuwa wavamizi katika eneo hilo la mgodi walirusha jiwe kwa kombeo ambalo lilipasua kioo na kumpiga rubani na kumjeruhi jicho la kulia.

Alisema ndege hiyo iliyokuwa ikitoka Dar es Salaam ilikuwa na watu wawili ambao ni rubani, Bw. Charles Wanchira (52) raia wa Kenya na msaidizi wake, Bw. Lioly Ernest, raia wa Afrika Kusini na kuongeza kuwa majeruhi alipata huduma ya kwanza na kisha kupelekwa Dar es Salaam kwa ajili ya matibabu zaidi.

Bw. Nyasigo pia aliongeza kuwa yamekuwapo matukio mengi ya uhalifu na kwamba katika kipindi cha mwezi huu, kumekuwa na matukio matatu, ikiwa ni pamoja na tukio la kupigwa kwa mlinzi wa mgodi akiwa lindoni kwa kutumia kombeo na kumjeruhi jicho.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mara, Bw. David Saibulu, alithibitisha kuwapo kwa tukio hilo na kuongeza kuwa watu watatu wamekamatwa.

Kamanda Saibulu aliwataja waliokamatwa, kuwa ni Marwa Nyahiri (40), Ginki Shoma (24) na Nyangi Shongo (22).
 
lazima sheria ifuate mkondo wake ! washitakiwe extremely upuuzi mwingine can not be condonned !
 
Tajiri akikaa karibu na masikini akawa anachukua hata walichonacho bila kumwangalia masikini huyo ujue kuna siku yatakukuta.

Hii ni challenge kwa Barrick, itabidi wakati mwingine wagawane kinachopatikana na wanakijiji.

Halafu mambo kama haya hayawezi kukwepeka wakati huu ambao watu wanafikra kuwa labda Barrick wanatumia ujanja ujanja kuchuma mali ktk nchi ya Tanzania.

Pamoja na sheria kuchukua mkondo wake kwa wahusika pia kuna haja ya serikali kutopuuza malalamiko mbalimbali yanayotolewa. Hata wakati wa ukoloni mambo yalianza hivi hivi.
 
Kama ndio mambo yenyewe ndio hivi basi ingekuwa busara kwa haya makampuni ya madini kuomba kufuta mikataba yao mibovu na serikali na kuingia mipya ambayo wananchi watairidhia. Nasema makampuni ndiyo yawe na initiative hii maana serikali yetu sidhani kama wako tayari kufanya hivyo kirahisi, I could be wrong though...
 
lazima sheria ifuate mkondo wake ! washitakiwe extremely upuuzi mwingine can not be condonned !

Yameshakuwa haya tena
Icadon

Ama mlitegemea nini? wapinzani si mlisema haya wakati wa ziara zenu mkoani, sasa wananchi wanatekeleza mliyotaka!!!,,, na wakiendelea hivi msidhani hata nanyi mkipewa nchi mtaweza kuiongoza... not at all

Ikiendeleea hivi wawekezaji hata wale ambao wanapenda kutenda haki hawataona ulazima wa kuja kuwekeza Tanzania badaya ya Uganda, Kenya, Botswana, DRC etc...

Yangu macho, lakini kwa hakika hali hii ikiendelea sio nzuri kabisa kwenye nchi,,, baadaye itakuwa kila tajiri awe amepata kwa halali au la!!! mawe tu!!!

Ewe Mola wa Haki, tunaomba usifikishe taifa letu hili changa huko, wape wananchi subra ya kutafakari wanayoambia na viongozi wa siasa na wape subra kwa kuwahukumu viongozi kwa nchi ya sanduku ya kura na sio kujichukulia sheria mkononi!!!
 
Hawa wenyeji wa Kewanja na vijiji vyote vya Nyamongo walikuwa na hali nzuri ya maisha kutokana na shughuli za uchimbaji wa dhahabu kabla ya hao wazungu kupora maeneo yao. Leo hii hali zao ni duni sana na si wajinga kujua kuwa uduni wa hali zao unasababishwa na nini. Leo wanawatungua kwa manati lakini siku inakuja watakapo watungua kwa machine gun.
 
Posted Date::10/13/2007
*Helikopta ya Barrick yapigwa jiwe angani

*Yatua kwa dharura, rubani ajeruhiwa

*FFU watumwa kumsaka aliyerusha jiwe



Na Mathias Marwa, Tarime
Mwananchi



HELIKOPTA ya mgodi wa North Mara imelazimika kutua kichakani katika Kijiji cha Kewanja, wilayani Tarime Mkoa wa Mara, baada ya kushambuliwa kwa mawe na watu wasiojulikana.

Helikopta hiyo mali ya mgodi huo unaomilikiwa na wawekezaji wa kampuni ya uchimbaji dhahabu ya Barrick Tanzania, ilishambuliwa juzi kwa kupigwa mawe na kupasuliwa kioo cha upande wa na kumjeruhi rubani jicho.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mara, David Saibullu, aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa tukio hilo lilitokea majira ya alasiri katika Kijiji cha Kewanja, Kata ya Kemambo, wilayani Tarime.

Helikopta hiyo ilikuwa ikiendeshwa na rubani Charles Wassira, mkazi wa Ukerewe Mkoa wa Mwanza.

Jiwe liliovunja kioo hicho na kumjeruhi rubani huyo, lilirushwa kwa kutumia kombeo na mtu ambaye hajafahamika, ikiwa umbali wa takriban mita 50 usawa wa bahari.

Baada ya rubani huyo kujeruhiwa jicho lake la kulia, alilazimika kutua na kupewa msaada wa kupata matibabu katika hospitali ya Nyamongo iliyopo katika Kijiji cha Nyangoto, wilayani humo.

Kufuatia huduma ya kwanza, rubani huyo akiwa na mwenzake mzungu waliyekuwa pamoja nwakati shambulio hilo likitokea, walifanya marekebisho ya kioo kilicho pasuliwa kisha kuondoka kurejea jijini Dar es Salaam.

Akizungumzia tukio hilo, Ofisa Mawasiliano wa Mgodi huo, Emmanuel Nyasigo, alisema tukio hilo lilitokea katika Uwanja wa Ndege wa Kijiji cha Kewanja Namongo wakati rubani akianza kurusha helikopta hiyo.

Nyasigo alisema kuwa helikopta hiyo ilishambuliwa wakati ikifanya doria katika eneo la mgodi huo na kudai kuwa aliyefanya kitendo ni miongoni mwa watu wanaodhaniwa kuwa wezi wa dhahabu na mafuta ambayo ni mali ya mgodi huo.

Alisema rubani huyo alitengeza kioo hicho kilichovunjwa kwa kutumia makaratasi meupe kuziba tundu na kurudi Dar es Salaam.

Kamanda Saibullu, alituma Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) Tarime, kikiongozwa na mkuu wake, Costantine Bandola kumsaka mtu huyo au watu waliohusika na tukio hilo ili kuwakamata ili wafikishwe katika vyombo vya sheria.

Hadi tunakwenda mitamboni hakuna mtu aliyekuwa amekwisha kukamatwa.

Katika eneo la mgodi huo wa Northen Mara kumekuwepo mgogoro kati ya kampuni ya Barrick na wananchi wa eneo hilo ambao wanadia fidia kwa maelezo kwamba kiasi walicholipwa hakilingani na thamani ya maeneo yao.

Kufuatia kutolidhika na malipo hayo baadhi ya waliokuwa wakazi wa eneo hilo waligoma kuchukua malipo hayo wakidai mikataba yao kurekebishwa kulingana na thamani ya maeneo yao.

Katika harakati za kudai haki zao waziri mkuu Edward Lowassa alipotembelea eneo hilo mwezi uliopita walimlalamikia na alipowaambia atamtuma Waziri wa Nishati na Madini, Naziri Karamagi kushguliki suala hilo, lakini walipinga kwa madai kwamba hawamtaki.


[
 
Gold-seekers stone helicopter, three arrested

2007-10-13 09:20:28
By George Marato, Musoma


Police in Musoma yesterday arrested three persons for allegedly stoning a patrol helicopter, property of Barrick Gold Mine, injuring both the pilot and co-pilot.

The incident occurred when a group of people was in the process of sneaking into North Mara gold mine the Mara, Regional Police Commander, David Ole Saibull, has said.

In an exclusive interview with The Guardian, Saibull said the incident occurred on Thursday evening at around 9.00 am, when the company`s helicopter was taking aerial photographs around the mine.

According to the RPC, suspected criminals, who numbered 15, stoned the aircraft, injuring the pilot, Charles Wanchira and his assistant, Lioly Ernest�who are Kenyan and South African nationals respectively.

The rest of the group vanished as the police made some arrests.

`The helicopter was hovering close to the ground in the course of patrolling the mine. One of the criminals threw a stone that damaged the screen,` said Saibull.

`The captain managed to fly the helicopter back into the mine, after which he was rushed to the Nyangoto Hospital for preliminary check-up before being shifted to Bugando Hospital in Mwanza,` said the RPC.

Barrick Gold Mine had hired the helicopter from South Africa for patrol purposes.

Saibull said those arrested were Marwa Nyairi (40), Ginki Shyoma (24) and Nyangi Shyongo (22)�all from Kewanja Village.


SOURCE: Guardian
 
Ni ccm ndio wametufikisha hapa tulipo,kwa kuwa na sera mbovu mbovu.

leo hii watu mnadiriki kusema ccm imewaweka hapa ? ama kweli kwa binadamu hakuna lililo jema, tanzania ingekuwa inaendeshwa na madikteta je ? au tz ingekuwa kama zimbabwe, we are really far ahead of many countries kama hamjui na tushukuru Mungu tuna amani ambayo ndio hiyo sasa inatibuliwa na wapinzani ! kuna sehemu nyingine afrika wananchi hawana sauti kabisa, not at all ! sie tushukuru wananchi wetu are some what free kufanya wanayotaka, kusema n.k sehemu nyingine unakuwa executed ! tatizo wengi wetu wanadhani wapinzani ndio wataleta maendeleo, kitu ambacho si kweli BALI mtu/chama chochote kile kinaweza kuleta maendeleo na kaa ukijua kwamba maendeleo ni process, milolongo lazima iwepo, shida, tabu ni yote matokeo ya maendeleo BUT NEVER TELL ME WAPINZANI LOVE THEIR COUNTRY MORE THAN ANY ONE, THATS A BIG BOLD FACE LIE ! wapinzani kama kweli wanataka kuleta maendeleo wakae meza moja na chama tawala na waongelee manufaa ya wananchi na sio kutembea mikoani kuambia wananchi wafanye fujo !
 
Mazuri ya CCM yalifanywa hadi pale walipoamua kujipatia mali kwa njia za KIFISADI na hatuwezi kukubali generation mbili/tatu za watanzania kuendelea kwa mtindo huu wa kutajirisha wageni ambao wanapora rasilimali kama vile hazina mwenyewe. Wale wanaopewa peremende waendelee na ushabiki wao lakini hivi sasa muda waja hizo pipi zitawatokea puani.
 
sasa kama suala la kufanya fujo, unadhani watakaokuwa affected na hizo fujo na ccm au wananchi wasio na hatia ? kumbuka kwamba fujo hazileti maendeleo bali mifarakano !
 
Kwani fujo ina maana gani? Unaposaini mkataba wa kuwaangamiza two/three generations ya WTZ (umasikini wa kutupwa) kwa njia ambazo wengine hawazioni ni fujo vile vile.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom