Lizarazu
JF-Expert Member
- Aug 23, 2015
- 6,334
- 7,868
Umedadavua vizuri sana na nimekuelewa general perspective uliyonayo!Kwa kiasi kikubwa (not 100%) ni very right lakini umeshindwa kuki-transform ulichokieleza na kukileta kwenye mazingira ya Afrika.
Kabla sijaenda mbali, kwanza niweke jambo moja sawa nalo ni kuhusu Yen ya Japan na government intervention. Kwa kifupi, Japan huwa hawafanyi intervention (kushusha au kuongeza thamani) kwenye sarafu yake. Kwenye post moja nimeeleza kwa kirefu why YEN ipo chini sana.
Aidha, watu wanavyoona Yen ya Japan ni cheap wanadhani ipo weak... Yen ni one of the strongest currency duniani na pia ni Floating Currency.
Kwa China, upo sahihi kwamba, hawa jamaa huwa wanafanya intervention. Na ni kutokana na ukweli huo ndio maana huwezi kuikuta Yuan kuwa ni miongoni mwa major currency pair duniani kwenye masoko makubwa ya fedha!!
Tukirudi kwenye suala la sarafu ya Burundi na Shilling, nimeeleza kwa kirefu kwenye post yangu #65 nimesema wazi hili suala haliwezi kuwa lenye mbolea kwa uchumi wa Burundi.
Now, tukirudi kwenye hoja yako kwamba.... "kushuka/kupanda kwa shilingi ya tanzania sio kipimo cha ukuaji/kuzorota kwa uchumi huku ukitolea mfano China au Japan ni upotofu wa hali ya juu."
Kwanza kupanda na/au kushuka husika kutategemea forces behind kupanda au kushuka huko! Kama kuna government intervention, YES, kupanda kwa shilingi hakutakuwa na uhusiano wowote na ukuaji wa uchumi! Mara kwa mara hapa nimekuwa nikitolea mfano wa Tanzania ya Mwalimu Nyerere!
Ingawaje nchi ilikuwa haina inakosa hadi dawa za meno na sabuni lakini bado shilingi ya Tanzania ilikuwa very expensive!! Ilikuwa very expensive kutokana na government intervention na hakukuwa na correlation yoyote kati ya shilingi na uchumi wetu kwa sababu determinant ya shilling price haikuwa market force!!
Kwa sasa, bei ya shilling inakuwa determined na market force with rare government intervention. Inaposhuka thamani, especially relative to dollar, sie wengine hatusemi uchumi umeshuka bali tunasema hatutakiwi kulia lia kwa sababu, on the other way round, hiyo ni opportunity!
Inakuwa ni opportunity na dalili njema kwa uchumi at large kwa sababu inafanya value of imports kuwa expensive!! Value of imports inapokuwa expensive. So, in the beginning, sio suala la export peke yake kama ilivyo kwa Japan au Uchina bali kwa mazingira ya uchumi wetu, tutaanza kuangalia import kwa sababu ndiyo inaelemea mizania ya biashara zetu za nje.
So, first assumption, shilling ikishuka thamani itafanya value of imports kuwa very expensive na hivyo kuchochea uzalishaji wa ndani... hiyo ndiyo opportunity tunayoisema!!! Hii ni kwa sababu sio bidhaa zote tunazoagiza hatuwezi kuzalisha ndani bali tunaagiza kwa sababu it's cheap to import kuliko kuzalisha ndani!!!
Endapo tutaanza kuzalisha ndani, assumption ni kwamba, in the medium to long run, bidhaa, ama ziwe za kilimo au non agriculture, zitakuwa nyingi sana nchini na hivyo itachochea wazalishaji kutafuta masoko ya nje... exports. Hii export ikishakuwa kubwa, itaimarisha shilingi yetu ambayo hapo kabla ilikuwa very weak!!!
Hiyo ni kwa upande mmoja lakini kwa upande mwingine, hata huo mfano wa Japan uliotolea nao una-fit!! Lazima ukumbuke source kubwa ya forex yetu ni mazao ya kilimo!
Chukulia korosho kwa mfano ambayo kumekuwa na price boom misimu miwili mfululizo. Kutokana na thamani ya shilingi yetu, ingawaje mkulima anashangilia bei kubwa ya korosho lakini kimsingi Traders wamenunua korosho for ONLY USD 2/kg. Hapa, mosi mkulima amefurahia bei kubwa ya korosho na ndio maana mwaka huu Wamakonde walihamasika sana kwenye kuongeza uzalishaji lakini pili, kwa upande wa Traders, USD2/Kilo ni bei shindani sana kwenye soko la dunia!!!
Now assume Dollar 1 ingekuwa inabadilishwa kwa Sh. 1000. This means, kama bei ingebaki vile vile, ina maana Cashew Traders wangekuwa wamenunua korosho kwa USD 4 kwa kilo na hivyo kuifanya korosho ya Tanzania kuwa more expensive soko la dunia!!!
Na kama bei ya maslahi kwa Traders ingekuwa ni ile ile USD 2 ya hapo juu, ina maana mkulima asingelipwa tena Sh. 4000 bali angelipwa Shilingi 2000!!
Again, thamani ndogo ya shilingi imekuwa neema kwa cashew producers!! Hali hii inaweza isiwe na maana yoyote endapo tu sehemu kubwa ya matumizi ya kila siku ya mwananchi wa kawaida yanatokana na imported goods!
I know mafuta ni moja ya hizo bidhaa lakini linapokuja suala la mafuta ni universal issue!!!!
Na ilimradi hatutegemei mchele, unga, mkate, maharage and the like kutoka nje, then net outcome mzunguko mzima unakuwa ni wa manufaa zaidi kwa mkulima kuliko kama bei ya shilingi ingekuwa expensive!
Lakini naona umetembea na assumptions sana kiasi kwamba napata ugumu kuamini kama ulichokielezea kina uhalisia wowote na mazingira yetu hasa kwa Tanzania. hapo unaposema kuwa imported products zikipanda thamani zitachochea uzalishaji wa ndani na hatimae mwisho wa siku production yetu itakuwa kubwa na kuanza kufanya exportation kitu ambacho kitaimarisha sarafu yetu..
Sasa wewe unaliona hili likifanyika tanzania kweli, kama waziri mkuu na boss wake wanazuia usafirishaji wa mazao ya chakula(tena ndio yanazalishwa kwa wingi nchini) kwenda nje ya nchi kwa muda wa zaidi ya miezi 9? Na muda huo huo sisi tunapokea yaliyozalishwa na wenzetu!?