Heko TLS kwa kutoa tamko la Covid 19, Aibu yenu Chama cha madaktari MAT.

Fundi Madirisha

Senior Member
Jun 30, 2020
184
986
Umuofia wanajukwaa!

Kwanza kabisa nitoe masikitiko yangu makubwa sana kwa chama cha madaktari Tanzania MAT, sikutegemea kuona kua hiki ni taasisi iliyojaa unafki mwingi na kujipendekeza. Haina msaada wowote katika wala katika taaluma ya tiba nchini. Ninashangaa na kushtuka mpaka sasa MAT hawajaweka wazi kua Tanzania tuna wimbi la pili la ugonjwa wa COVID-19 kama ambavyo TLS wamesema bayana na pia baadhi ya viongozi wa dini wamesema.

Hongereni sana chama cha wanasheria Tanganyika TLS kwa kuweka msimamo wenu juu ya hali inayoendelea na kuweka wazi kabisa umma kua tuko katika kipindi kigumu cha Wimbi la pili la ugonjwa wa COVID-19. Mmetimiza wajibu wenu kama alivyotakiwa katika vifungu vya sheria za kuanzishwa kwenu. Hakika ninyi si wanafiki ni wakweli na kweli mnasimsmia haki za watanzania ikiwemo ya kuishi.

Yaani chama cha Madaktari ambacho wataalam wake 24hrs wanashinda na wagonjwa na wanaidhinisha vifo vyao washikwe kigugumizi kusema tatizo nini? Wameamua kuiweka taaluma yao mifukoni na kuamua kufanya siasa?
Hiki chama hakifai, wakitaka kujua ni kwanini hakifai watazame michango ya vyama vya Madaktari toka kwa majirani zetu wa Uganda, Kenya, Rwanda na hata mataifa makubwa ya Marekani,Canada,Australia,Uingereza nk. Kivunjwe mara moja hiki chama hakina tija kwa taifa.

Mwisho lakini kwa umuhimu sana, tunawashukuru sana viongozi wetu wa madhehebu baadhi ya dini waliojitokeza wazi wazi kusema kua tunasumbuliwa na tatizo hili la wimbi la pili la homa ya mapafu. Hongereni sana mmeikwepa dhambi ya uongo na hata siku ya hukumu mtalipwa wema wenu.

Ni muhimu kuendelea kuchukua tahadhari, tatizo lipo na linatisha wala hakuna unafki katika hili.
1613808379898.png
1613808396580.png
1613808414947.png
1613808431277.png
1613808443804.png
1613808458622.png
1613808472970.png
 

Attachments

  • Tamko la TLS juu ya Wimbi la Pili la Mlipuko wa Ugonjwa wa Korona 2021.pdf
    434.1 KB · Views: 10
Watu wengine buana?,yaani mbele yako unaona kuna moto kuuepuka mpaka serikali ikuambie?,wenzako tuneshaanza kuchukua tahadhali mydamrefu sana,jilinde wewe na jamii yako
#VaaBarakoaCoronaIpo
 
Mpaka leo, sjaskia tamko lolote la Serikali linalozuia watu kujikinga na Corona
Na mpaka leo hatujasikia kauli ya serikali inayosema kuna korona au kuwapa wamanchi wake updates za korona.

Yani serikali imeamua nchi ijiongoze kama vile rubani anavyo set "auto pilot" then analala ndege ijiongoze yenyewe!!

A shithole gavamenti.
 
Na mpaka leo hatujasikia kauli ya serikali inayosema kuna korona au kuwapa wamanchi wake updates za korona.

Yani serikali imeamua nchi ijiongoze kama vile rubani anavyo set "auto pilot" then analala ndege ijiongoze yenyewe!!

A shithole gavamenti.
Kauli hio unataka uisikie kwa kuunganisha herufi ? mbona hata Mheshimiwa anasema kuwa corona ipo,au unahitaji aende TBC upigwe wimbo wa Taifa kisha atoe ilani rasmi,aliposema WaTz tutumie tiba asilia aka nyungu ,mnahisi alikusudia nyungunyungu ?
 
Madaktari wameidhalilisha taaluma ya udaktari na kuofanya ionekane taaluma iliyoshikiliwa na watu wa ajabu, watu wanafiki, waoga na wababaishaji.

Hongereni wanasheria. Ole wenu chama cha madaktari kwa unafiki wenu. Mnajenga mazingira ya kuwaua wanachama wenu kwa unafiki wenu.
 
Viongozi wa afya wanaidhalilisha taaluma yao kuanzi waziri wa afya na naibu wake mpaka hao viongozi wa Jumuia ya Afya
Wameamua kuweka taaluma yao pembeni na kukumbatia "utaalamu" wa mkemia wa juisi ya korosho
 
Na mpaka leo hatujasikia kauli ya serikali inayosema kuna korona au kuwapa wamanchi wake updates za korona.

Yani serikali imeamua nchi ijiongoze kama vile rubani anavyo set "auto pilot" then analala ndege ijiongoze yenyewe!!

A shithole gavamenti.

Halafu wanachukulia Watanzania wote ni kama sisi wachache tunaosaka taarifa mitandaoni na kwenye vyombo vya kimataifa huku wao kwenye majukwaa yao ya kisiasa wakiwaaminisha wananchi kuwa corona imemalizwa kwa maombi. Kwamba wanaovaa barakoa “wanaamini matambara kuliko kumpa Mungu utukufu”! Na kusisitiza nyungu na mitishamba.

Mitaani unakutana na watu kibao wanaishi carelessly; hakuna kujilinda. Ukiwauliza, wanakwambia serikali imesema hakuna corona; ni njama za mabeberu na biashara yao ya chanjo. Kama serikali imeamua kutokuwa wazi kwa wananchi ili kila mtu ajijue mwenyewe - sawa. Kazi kwao wanyonge.
 
Umuofia wanajukwaa!

Kwanza kabisa nitoe masikitiko yangu makubwa sana kwa chama cha madaktari Tanzania MAT, sikutegemea kuona kua hiki ni taasisi iliyojaa unafki mwingi na kujipendekeza. Haina msaada wowote katika wala katika taaluma ya tiba nchini. Ninashangaa na kushtuka mpaka sasa MAT hawajaweka wazi kua Tanzania tuna wimbi la pili la ugonjwa wa COVID-19 kama ambavyo TLS wamesema bayana na pia baadhi ya viongozi wa dini wamesema.

Hongereni sana chama cha wanasheria Tanganyika TLS kwa kuweka msimamo wenu juu ya hali inayoendelea na kuweka wazi kabisa umma kua tuko katika kipindi kigumu cha Wimbi la pili la ugonjwa wa COVID-19. Mmetimiza wajibu wenu kama alivyotakiwa katika vifungu vya sheria za kuanzishwa kwenu. Hakika ninyi si wanafiki ni wakweli na kweli mnasimsmia haki za watanzania ikiwemo ya kuishi.

Yaani chama cha Madaktari ambacho wataalam wake 24hrs wanashinda na wagonjwa na wanaidhinisha vifo vyao washikwe kigugumizi kusema tatizo nini? Wameamua kuiweka taaluma yao mifukoni na kuamua kufanya siasa?
Hiki chama hakifai, wakitaka kujua ni kwanini hakifai watazame michango ya vyama vya Madaktari toka kwa majirani zetu wa Uganda, Kenya, Rwanda na hata mataifa makubwa ya Marekani,Canada,Australia,Uingereza nk. Kivunjwe mara moja hiki chama hakina tija kwa taifa.

Mwisho lakini kwa umuhimu sana, tunawashukuru sana viongozi wetu wa madhehebu baadhi ya dini waliojitokeza wazi wazi kusema kua tunasumbuliwa na tatizo hili la wimbi la pili la homa ya mapafu. Hongereni sana mmeikwepa dhambi ya uongo na hata siku ya hukumu mtalipwa wema wenu.

Ni muhimu kuendelea kuchukua tahadhari, tatizo lipo na linatisha wala hakuna unafki katika hili.
View attachment 1707098View attachment 1707099View attachment 1707100View attachment 1707101View attachment 1707102View attachment 1707103View attachment 1707104
Uongozi wa MAT uliosheheni maafisa vipenywa, ni aibu kwa nchi hii na taaluma nzima ya udaktari wa binadamu hapa nchini.

Madaktari wazalendo rekebisheni hali hii mapema iwezekanavyo.

Siasa na taaluma vinatangamana.

Au nasema uongo ndugu zangu?
 
Hili sasa ndio tamko.Unaliona kabisa lina usomi ndani yake sio kile kipeperushi cha wale vilaza wa MAT.
Inatia aibu yaani watu walio nje ya taaluma yako wanaweza kutoa kitu kama hiki kilicho na mantiki.
Madaktari wengi wa siku hizi ni vilaza hasa.
Dunia ina advocate matumizi ya science nyie mnatetea kula ndimu.
 
Sidhani kama ni kutetea mkuu, nikweli Serikali inatakiwa itoe neno kuhusu kujikinga lakini kwa vile hakuna dalili za hilo tamko ndio maana mdau anashauri kuwa tusisubiri tamko, ni muda wa kuchukua hatua bila hata tmko.

Kwa maoni haya nadhani unashauri tumtake huyu serikali ajiuzuru tu kwani ameshindwa kutekeleza wajibu wakr.

Serikali wana wajibu mkubwa wa kuwalinda, kuwahami na kuwakinga watu wake ikiwamo kuwapa taarifa sahihi na kwa wakati yakiwamo juu ya magonjwa kama haya ya Corona.

Je serikali hii wanafanya hayo?

Wamemwachia nani majukumu hayo?

Kama jibu ni la! Basi watu hawa ni wa kazi gani?
 
MAT wameandika utumbo hata kuandika neno Corona wanaogopa, umuhimu wa serikali kutamka ugonjwa upo na kusisitiza ugonjwa upo ni vema sana, maana kuna raia ukiwaambia wajilinde watakuambia serikali inasema hamna ugonjwa
 
9 Reactions
Reply
Back
Top Bottom