Heko nyingine ya Rais Magufuli kwenye kupigania maslahi ya Tanzania: Kisa cha bomba la mafuta kutoka Hoima, Uganda hadi Tanzania

JOYOPAPASI

JF-Expert Member
Jan 10, 2016
250
408
HEKO NYINGINE YA RAIS MAGUFULI KWENYE KUPIGANIA MASLAHI YA TANZANIA: KISA CHA BOMBA LA MAFUTA KUTOKA HOIMA, UGANDA HADI TANZANIA

Na Bwanku M Bwanku

Jumapili Septemba 13 mwaka huu tulishuhudia tukio kubwa la kihistoria la kiuchumi, ustawi wa watu, undugu na maendeleo ya nchi yetu kwa kushuhudia utiaji saini wa utekelezaji wa mradi mkubwa wa Bomba la mafuta lenye urefu wa takriban Km 1445 kutoka Hoima nchini Uganda mpaka Tanga Tanzania wenye gharama ya Trillion 7.8, tukio lililofanyika kule Chato mkoani Geita kati ya Rais wa Tanzania Mhe John Pombe Magufuli na Rais wa Uganda Yoweri Kaguta Museveni.

Mradi huo wa matrillion wa Bomba la mafuta refu kabisa duniani la kusafirisha mafuta ya moto Kutoka Hoima, Uganda mpaka Tanzania unakuja baada ya juhudi kubwa ya Rais Magufuli kumuomba Rais Museveni apitishe Bomba hilo nchini Tanzania hasa kwa kutambua jinsi mradi huo ulivyo na faida kubwa kwa nchi ya Tanzania na hasahasa kugeuka kuwa fursa kwa mikoa 8, wilaya 24, kata 132 na vijiji 186 utakakopita.

Chini ya mapambano ya Rais Magufuli kuomba mradi huo upite nchini kwetu, Tanzania itapata asilimia 60 ya faida itakayozalishwa kwenye mradi huo huku Uganda ikipata asilimia 40 na kuajiri kati ya Watanzania elfu 10 hadi elfu 15 kwa ajira za moja kwa moja kwenye mradi huo.

Zaidi kwenye mikoa 8 ya Kagera, Geita, Shinyanga, Tabora, Singida, Dodoma, Manyara na Tanga ambako mradi huo utapita, Watanzania zaidi ya 90 elfu watalipwa fidia inayofika takribani Billion 21 kwa wananchi wote watakaoguswa na kupitiwa na mradi huo.

Hapo hujaenda kwa mama nitilie, bodaboda na kundi kubwa la Watanzania ambao watafaidika na mradi huo kwa kuajiliwa kwa muda na wengine watakaotoa huduma mbalimbali ndani ya maeneo ya mradi huo. Zaidi utaendelea kuimarisha mahusiano mazuri ya nchi yetu na Uganda na kukomaza zaidi diplomasia yetu ya Afrika Mashariki.

Nani kama Magufuli? Nani anapinga haya? Huo ndio uongozi wa kujitoa kwa maarifa na nguvu zako zote ili kuwainua wananchi wako. Sasa Watanzania ni mwendo wa kuchangamkia fursa tu kwenye mradi huo mkubwa na mrefu kabisa wa kusafirisha mafuta kwenye Bomba hilo. Kura zote ni kwa Magufuli tu siku ya Jumatano, Oktoba 28.

0657475347
 
1.-1.jpg

Jumapili Septemba 13 mwaka huu tulishuhudia tukio kubwa la kihistoria la kiuchumi, ustawi wa watu, undugu na maendeleo ya nchi yetu kwa kushuhudia utiaji saini wa utekelezaji wa mradi mkubwa wa Bomba la mafuta lenye urefu wa takriban Km 1445 kutoka Hoima nchini Uganda mpaka Tanga Tanzania wenye gharama ya Trillion 7.8, tukio lililofanyika kule Chato mkoani Geita kati ya Rais wa Tanzania Mhe John Pombe Magufuli na Rais wa Uganda Yoweri Kaguta Museveni.

Mradi huo wa matrillion wa Bomba la mafuta refu kabisa duniani la kusafirisha mafuta ya moto Kutoka Hoima, Uganda mpaka Tanzania unakuja baada ya juhudi kubwa ya Rais Magufuli kumuomba Rais Museveni apitishe Bomba hilo nchini Tanzania hasa kwa kutambua jinsi mradi huo ulivyo na faida kubwa kwa nchi ya Tanzania na hasahasa kugeuka kuwa fursa kwa mikoa 8, wilaya 24, kata 132 na vijiji 186 utakakopita.

Chini ya mapambano ya Rais Magufuli kuomba mradi huo upite nchini kwetu, Tanzania itapata asilimia 60 ya faida itakayozalishwa kwenye mradi huo huku Uganda ikipata asilimia 40 na kuajiri kati ya Watanzania elfu 10 hadi elfu 15 kwa ajira za moja kwa moja kwenye mradi huo.

Zaidi kwenye mikoa 8 ya Kagera, Geita, Shinyanga, Tabora, Singida, Dodoma, Manyara na Tanga ambako mradi huo utapita, Watanzania zaidi ya 90 elfu watalipwa fidia inayofika takribani Billion 21 kwa wananchi wote watakaoguswa na kupitiwa na mradi huo.

Hapo hujaenda kwa mama nitilie, bodaboda na kundi kubwa la Watanzania ambao watafaidika na mradi huo kwa kuajiliwa kwa muda na wengine watakaotoa huduma mbalimbali ndani ya maeneo ya mradi huo. Zaidi utaendelea kuimarisha mahusiano mazuri ya nchi yetu na Uganda na kukomaza zaidi diplomasia yetu ya Afrika Mashariki.

Nani kama Magufuli? Nani anapinga haya? Huo ndio uongozi wa kujitoa kwa maarifa na nguvu zako zote ili kuwainua wananchi wako. Sasa Watanzania ni mwendo wa kuchangamkia fursa tu kwenye mradi huo mkubwa na mrefu kabisa wa kusafirisha mafuta kwenye Bomba hilo. Kura zote ni kwa Magufuli tu siku ya Jumatano, Oktoba 28.
 

Jumapili Septemba 13 mwaka huu tulishuhudia tukio kubwa la kihistoria la kiuchumi, ustawi wa watu, undugu na maendeleo ya nchi yetu kwa kushuhudia utiaji saini wa utekelezaji wa mradi mkubwa wa Bomba la mafuta lenye urefu wa takriban Km 1445 kutoka Hoima nchini Uganda mpaka Tanga Tanzania wenye gharama ya Trillion 7.8, tukio lililofanyika kule Chato mkoani Geita kati ya Rais wa Tanzania Mhe John Pombe Magufuli na Rais wa Uganda Yoweri Kaguta Museveni.

Mradi huo wa matrillion wa Bomba la mafuta refu kabisa duniani la kusafirisha mafuta ya moto Kutoka Hoima, Uganda mpaka Tanzania unakuja baada ya juhudi kubwa ya Rais Magufuli kumuomba Rais Museveni apitishe Bomba hilo nchini Tanzania hasa kwa kutambua jinsi mradi huo ulivyo na faida kubwa kwa nchi ya Tanzania na hasahasa kugeuka kuwa fursa kwa mikoa 8, wilaya 24, kata 132 na vijiji 186 utakakopita.

Chini ya mapambano ya Rais Magufuli kuomba mradi huo upite nchini kwetu, Tanzania itapata asilimia 60 ya faida itakayozalishwa kwenye mradi huo huku Uganda ikipata asilimia 40 na kuajiri kati ya Watanzania elfu 10 hadi elfu 15 kwa ajira za moja kwa moja kwenye mradi huo.

Zaidi kwenye mikoa 8 ya Kagera, Geita, Shinyanga, Tabora, Singida, Dodoma, Manyara na Tanga ambako mradi huo utapita, Watanzania zaidi ya 90 elfu watalipwa fidia inayofika takribani Billion 21 kwa wananchi wote watakaoguswa na kupitiwa na mradi huo.

Hapo hujaenda kwa mama nitilie, bodaboda na kundi kubwa la Watanzania ambao watafaidika na mradi huo kwa kuajiliwa kwa muda na wengine watakaotoa huduma mbalimbali ndani ya maeneo ya mradi huo. Zaidi utaendelea kuimarisha mahusiano mazuri ya nchi yetu na Uganda na kukomaza zaidi diplomasia yetu ya Afrika Mashariki.

Nani kama Magufuli? Nani anapinga haya? Huo ndio uongozi wa kujitoa kwa maarifa na nguvu zako zote ili kuwainua wananchi wako. Sasa Watanzania ni mwendo wa kuchangamkia fursa tu kwenye mradi huo mkubwa na mrefu kabisa wa kusafirisha mafuta kwenye Bomba hilo. Kura zote ni kwa Magufuli tu siku ya Jumatano, Oktoba 28.
Ni kweli Rais Magufuli kwa haya yote aliyoyafanya ni makubwa sana ajiandae kubeba kura nyingi sana za ushindi
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom