Heko Lema kwa Ujenzi wa Barabara hadi za mitaa

bushland

JF-Expert Member
Mar 6, 2015
7,016
4,961
Tunakupongeza Mbunge wetu Lema pamoja na meya WA jiji la Arusha Calisty Lazaro kwa maendeleo ya mkoa huu.

Tunaona ujenzi WA Bara bara hadi za mitaani ukiendelea kwa mwendo WA changarawe na zile kuu kwa kiwango cha Lami., tunashukuru Sana sasahivi hata vumbi hamna huku mtaani,

Naamini hizi mlizoweka changarawe huku mtaani baada ya miaka 2,itakuwa full lami.
 
Kwani km usemavyo unadhani kwa kukaa pale Kisongo ndo ulikuwa ni mwisho wa ukombozi?

Yote hayo ndo chachu ya kujua kipi mchele na kipi chuya.
 
Hakika wana arusha mmepata mbuge anayejua thamani yenu!
Hongereni pamoja na mstahiki meya pamoja na madiwani wa chadema

Hiyo kazi iliwashinda ccm zaidi ya miaka 40
Kweli Mkuu, viongozi WA CHADEMA pamoja na Wananchi wake Ni wachapakazi hakuna Mfano
 
Mkumbusheni na Mdee pia, mahandaki jimbo ya Kawe imekuwa kama kitu cha kawaida, gharama ya kununua vipuri vya magari inasikitisha,wasipoweka lami basi wapitishe hata greda baada ya mvua.
 
Acheni hadaa za ajabu ajabu...ujenzi wa barabara ni program maalumu kwa majiji yote nchini
Ngoja wajitekenye na kucheka wenyewe!ukweli unajulikana....alichofanya lema kama anavyodai mwenyewe ni
1. kuwatia ujasiri watu wa arusha....nadhani walikuwa waoga kama kuku!
2. aligeuza hiace kuwa ambulance (alilibandika mataa mekundu&kulipaka rangi)
Zaidi ya hayo pumba tupu!
 
ARUSHA kwa sasa inapendeza, lami kila kona ( Makao mapya, Kaloleni,Levolosi,ungalimited,Fire,Nk) huku kote kipindi cha ccm ili kuwa ni mashimo ila sasa ni lami.
Raskazoni via Mianzini mpaka Tengeu sasa ni Gari 4 kwenda na 4 kurudi (4roads).

Mrisho Gambo anapita kwa raha zake kwenye Barabara zilizotengenezwa chini ya usimamizi wa Chadema.

Asante Chadema
Asante Lema
 
Back
Top Bottom