Heko gazeti la Mwananchi

Sanda Matuta

JF-Expert Member
May 9, 2007
949
134
nimekuwa nikisoma gazeti hili mara kwa mara,ingawa muda mwingine limekuwa likilalia upand e mmoja katika utoaje wake wa habari kiasi cha kuwapa usumbufu waandishi wake kutoka kwa wale wanaoguswa na habari husika hasa za kisiasa.
Lakini,napenda kuchukua fursa hii kumpongeza muhariri na waandishi wake wale wa "kijarida" kile cha ndani ya gazeti (miaka 50 ya uhuru) .Wamefanya kazi ya ziada ya kuchunguza na kuhakikki taarifa na historia ya taifa hili ambazo nyingi zilikua hazifahamiki au kufichwa na baadhi ya watu kwa malengo yao binafsi.
Hii,ni fursa tosha kwa sisi wasomaji na familia zetu hasa watoto wetu ambao hawajui historia ya nchi hii (yao),tuchukue fursa hii kuwashauri na wasisitiza katika kusoma magazeti na vitabu ili kujua historia yao,pia na wale vijana wenzangu ambao kwa njia moja ama nyingine wamekosa kujua yale yalio jiri kabla na baada ya uhuru wetu.

Hongera sana gazeti la MWANANCHI
 
NIMEKUELEWA MKUU,????
TOA SUGGESTION BASI NINI KIFANYIKE.
Unajua HISTORIA ya taifa lako lakini??
 
-Nilikua sifahamu ati hata WAKENYA waliwahi kuwa viongozi wa TAA kabla ya kuundwa kwa TANU ,kweli Historia ya inchi hii ina mambo mengi ambayao ama kwa hakika yalifichwa.
 
John Okello "Field Marshal" na Zanzibar revolution-Lawerence Kilimwiko,Hii ndio habari ya leo.
Nashauri watu hapa JF tuwe tunasoma hizi habari ili mijadala iwe based on facts kuliko ilivyo sasa.
Narudia tena,Hongera sabna Gazeti a mwananchi
 
Nina endelea kupongeza gazeti kwa hizi makala za 50 ya uhuru


"watekaji walikuwa wahuni tu!?" William Shayo
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom