Jumbe Brown
JF-Expert Member
- Jun 23, 2020
- 12,078
- 12,756
Kongamano la Maombi,Dua Na MARIDHIANO ya Amani Kuelekea Uchaguzi Wa Oktoba 2020.
Hakika Alichokihubiri Mzee John Magalle Shibuda Akiwakilisha Vyama 19 vya siasa nchini,kitabaki kuwa Ni MANENO YA DHAHABU Leo,Kesho na Milele. Shibuda Anabaki Ni Alama Ya Kutukumbusha kuwa TAIFA Hili litabaki hata baada ya UCHAGUZI ujao na zile za miaka Ijayo.
Ulimi FASWAHA wa Shibuda, Ukihanikiza Sauti Tamu Yenye Utajiri Wa Kujipenyeza Mioyoni mwa wamsikilizao,ilitukumbusha kuwa SIASA Ni njia na lengo la kutufikisha kupata WAWAKILISHI wetu Uongozini ambao WATATENDA kwa niaba yetu,WATATENDA Kwa Kodi Zetu Ili kuileta nchi pamoja na kutupeleka kule Tutakako kwa FAIDA yetu na vizazi vyetu vijavyo bila kubaguliwa KIDINI, KIKABILA, KIRANGI, KIKANDA na FAMILIA WATOKAZO.
Msikilize Mzee Shibuda Akisema kuwa Mwalimu Nyerere alipata kusema kuwa;huwezi kuyatatua Matatizo kwa kujitia kuwa HAYAPO.
Shibuda aliendelea kusema ya kwamba;
< WANASIASA Waache kuwa CHANZO Cha kumwaga petroli katika Moto.
< Huwezi Kuweka Miiba Nje Ya Nyumba Na Njiani Kwako Ukategemea Utakwenda na Kurudi Kwa Amani.
< WANASIASA Waangalie Wasijikwae Mwili Badala ya kidole.
< Japo kuwa Siasa Ni kupigana Vijembe ila Waangalie WASIACHE kutumia lugha za Staha zenye Kurindimisha AMANI TELE.
< TAMISEMI iache ilichokifanya katika mchakato wa Uchaguzi wa Serikali Za Mitaa.
< MaDC na maRC Waache Kujipendekeza Kwa Mpendwa Rais Wetu Magufuli na kuacha Ukweli unaojulikana.
< Werevu hutembea na Hoja zenye HEKIMA NA BUSARA.
< Amemsifu Rais kwa mapambano dhidi ya CORONA na KUKUKUMBUSHA kuwa,UKIPENDA KUSIFIWA VYAKO VIZURI BASI UWE NA HULKA YA KUSIFU VIZURI VYA WENZAKO.
< WANASIASA mkashindanishe utamu wa HOJA na Nyinyi Serikali mkae mkijua kuwa WANASIASA NA SIASA Ina VIONJO VYAKE kwani mwalimu HAWEZI kuvijua VIONJO vya DAKTARI.
< Vyama Vingi vilianzishwa na CCM kwa hiyo Mmakonde Asiogope kinyago chake.
< TAMISEMI isisahau kuyafanyia kazi YALIYOJIRI KATIKA KAMATI ZA MARIDHIANO YA KISIASA NA KIDINI.
< Rais Wetu Anapenda Ukweli na Hapendi Maneno Ya KUFUBAZA Kwani SI DAWA YA UKIMWI.
John Magalle Shibuda alimalizia kwa KUKUKUMBUSHA kuwa UNAFIKI hula THAWABU,na Uchaguzi Ni KAA LA MOTO,twendeni kwenye Uchaguzi tukitanguliza AMANI, HAKI, UPENDO, MARIDHIANO, MSHIKAMANO NA UMOJA WETU kwa Maana Mwalimu Nyerere HATUKO NAYE KIMWILI ila bado anaishi kwa MANENO NA VITENDO VYAKE tunduizi kwa FAIDA Pana ya nchi hii zaidi ya FAIDA za vyama na LEGACIES ZA KISIASA za watu wachache.
Mwenyezi Mungu Ambariki mzee wetu John Magalle Shibuda aaamin aaaamin.
Na Pia ninamuomba Mwenyezi Mungu Ayaweke Maneno Haya yaliyo DHAHABU kutoka kinywani mwa Shibuda, Tuyasome na Tuyaelewe Sisi Tuliopo Sasa, na Ukifika muda huko mbeleni wayasome Wanangu na Wanetu Walio Wadogo pale Watakapokuwa VIJANA wakubwa Kama Sisi,aaaamin aaaamin.
Tanzania Kwanza,
Maridhiano Kwanza,
Amani Na Haki Kwanza,
Siempre Siempre TZ,
Hasta la Victoria TZ.
Jumbe Brown
Kijana Muuza Al Kasus
Tandale Kwa Mtogole.
24/8/2020
Hakika Alichokihubiri Mzee John Magalle Shibuda Akiwakilisha Vyama 19 vya siasa nchini,kitabaki kuwa Ni MANENO YA DHAHABU Leo,Kesho na Milele. Shibuda Anabaki Ni Alama Ya Kutukumbusha kuwa TAIFA Hili litabaki hata baada ya UCHAGUZI ujao na zile za miaka Ijayo.
Ulimi FASWAHA wa Shibuda, Ukihanikiza Sauti Tamu Yenye Utajiri Wa Kujipenyeza Mioyoni mwa wamsikilizao,ilitukumbusha kuwa SIASA Ni njia na lengo la kutufikisha kupata WAWAKILISHI wetu Uongozini ambao WATATENDA kwa niaba yetu,WATATENDA Kwa Kodi Zetu Ili kuileta nchi pamoja na kutupeleka kule Tutakako kwa FAIDA yetu na vizazi vyetu vijavyo bila kubaguliwa KIDINI, KIKABILA, KIRANGI, KIKANDA na FAMILIA WATOKAZO.
Msikilize Mzee Shibuda Akisema kuwa Mwalimu Nyerere alipata kusema kuwa;huwezi kuyatatua Matatizo kwa kujitia kuwa HAYAPO.
Shibuda aliendelea kusema ya kwamba;
< WANASIASA Waache kuwa CHANZO Cha kumwaga petroli katika Moto.
< Huwezi Kuweka Miiba Nje Ya Nyumba Na Njiani Kwako Ukategemea Utakwenda na Kurudi Kwa Amani.
< WANASIASA Waangalie Wasijikwae Mwili Badala ya kidole.
< Japo kuwa Siasa Ni kupigana Vijembe ila Waangalie WASIACHE kutumia lugha za Staha zenye Kurindimisha AMANI TELE.
< TAMISEMI iache ilichokifanya katika mchakato wa Uchaguzi wa Serikali Za Mitaa.
< MaDC na maRC Waache Kujipendekeza Kwa Mpendwa Rais Wetu Magufuli na kuacha Ukweli unaojulikana.
< Werevu hutembea na Hoja zenye HEKIMA NA BUSARA.
< Amemsifu Rais kwa mapambano dhidi ya CORONA na KUKUKUMBUSHA kuwa,UKIPENDA KUSIFIWA VYAKO VIZURI BASI UWE NA HULKA YA KUSIFU VIZURI VYA WENZAKO.
< WANASIASA mkashindanishe utamu wa HOJA na Nyinyi Serikali mkae mkijua kuwa WANASIASA NA SIASA Ina VIONJO VYAKE kwani mwalimu HAWEZI kuvijua VIONJO vya DAKTARI.
< Vyama Vingi vilianzishwa na CCM kwa hiyo Mmakonde Asiogope kinyago chake.
< TAMISEMI isisahau kuyafanyia kazi YALIYOJIRI KATIKA KAMATI ZA MARIDHIANO YA KISIASA NA KIDINI.
< Rais Wetu Anapenda Ukweli na Hapendi Maneno Ya KUFUBAZA Kwani SI DAWA YA UKIMWI.
John Magalle Shibuda alimalizia kwa KUKUKUMBUSHA kuwa UNAFIKI hula THAWABU,na Uchaguzi Ni KAA LA MOTO,twendeni kwenye Uchaguzi tukitanguliza AMANI, HAKI, UPENDO, MARIDHIANO, MSHIKAMANO NA UMOJA WETU kwa Maana Mwalimu Nyerere HATUKO NAYE KIMWILI ila bado anaishi kwa MANENO NA VITENDO VYAKE tunduizi kwa FAIDA Pana ya nchi hii zaidi ya FAIDA za vyama na LEGACIES ZA KISIASA za watu wachache.
Mwenyezi Mungu Ambariki mzee wetu John Magalle Shibuda aaamin aaaamin.
Na Pia ninamuomba Mwenyezi Mungu Ayaweke Maneno Haya yaliyo DHAHABU kutoka kinywani mwa Shibuda, Tuyasome na Tuyaelewe Sisi Tuliopo Sasa, na Ukifika muda huko mbeleni wayasome Wanangu na Wanetu Walio Wadogo pale Watakapokuwa VIJANA wakubwa Kama Sisi,aaaamin aaaamin.
Tanzania Kwanza,
Maridhiano Kwanza,
Amani Na Haki Kwanza,
Siempre Siempre TZ,
Hasta la Victoria TZ.
Jumbe Brown
Kijana Muuza Al Kasus
Tandale Kwa Mtogole.
24/8/2020