Kwa kawaida binadamu hupambana na changamoto zinazomkabili kwa kutumia kile alicho nacho.
Kiongozi mwenye akili ndogo, hata siku moja hawezi kutumia akili kupambana na hoja za wapinzani wake. Kwa vile atakuwa na nguvu za mamlaka, atatumia nguvu za dola.
Ukiona utawala unatumia sana nguvu za dola kwenye ngazi mbalimbali, ujue kuwa utawala huo umejaza watu wenye akili ndogo. DC, RC, RPC, Waziri, mwenye akili ndogo, mara nyingi atapenda kutumia polisi hata kwa matukio yasiyohitaji polisi.
Kwenye ngazi ya Taifa, kiongozi akiwa na akili kidogo, atajitahidi kutumia polisi, TIS, magereza, mahakama, na hata kuwabambikia kesi wote wenye kumpa changamoto ili kuzima hoja zao, ambazo anashindwa kuzikabili kwa hoja na weledi.
Ukiona matumizi ya vyombo vya dola yanakuwa kwa kiwango cha hali ya juu katika kukabili hoja, ujue kuwa nafasi nyingi za maamuzi zimeshikwa na watu wenye akili ndogo.
WITO: Tunapochagua viongozi, tuhakikishe tunachagua watu wenye akili kubwa. Hao watajibu hoja kwa hoja maana kuijibu au kuishinda hoja kunahitaji akili na siyo nguvu. Mwenye akili ndogo hawezi kutumia asichokuwa nacho, atatumia nguvu kwa sababu ana mamlaka na vyombo vya mabavu, kama vile polisi.
Unapomchagua mtu mwenye akili ndogo, ujue unakaribisha maafa kwa Taifa. Tuwapige vita viongozi wote wenye akili kidogo, na uthibitisho kuwa kiongozi ana akili kidogo, angalia huyo kiongozi anapenda kwa kiwango gani kutumia vyombo vya mabavu.
Ni rahisi sana kiongozi mwenye akili kidogo kutoa amri ya kuua au mtu fulani afungwe hata kama hana hatia, kuliko kwa kiongozi ambaye ni super intelligent.
Kiongozi mwenye akili ndogo, hata siku moja hawezi kutumia akili kupambana na hoja za wapinzani wake. Kwa vile atakuwa na nguvu za mamlaka, atatumia nguvu za dola.
Ukiona utawala unatumia sana nguvu za dola kwenye ngazi mbalimbali, ujue kuwa utawala huo umejaza watu wenye akili ndogo. DC, RC, RPC, Waziri, mwenye akili ndogo, mara nyingi atapenda kutumia polisi hata kwa matukio yasiyohitaji polisi.
Kwenye ngazi ya Taifa, kiongozi akiwa na akili kidogo, atajitahidi kutumia polisi, TIS, magereza, mahakama, na hata kuwabambikia kesi wote wenye kumpa changamoto ili kuzima hoja zao, ambazo anashindwa kuzikabili kwa hoja na weledi.
Ukiona matumizi ya vyombo vya dola yanakuwa kwa kiwango cha hali ya juu katika kukabili hoja, ujue kuwa nafasi nyingi za maamuzi zimeshikwa na watu wenye akili ndogo.
WITO: Tunapochagua viongozi, tuhakikishe tunachagua watu wenye akili kubwa. Hao watajibu hoja kwa hoja maana kuijibu au kuishinda hoja kunahitaji akili na siyo nguvu. Mwenye akili ndogo hawezi kutumia asichokuwa nacho, atatumia nguvu kwa sababu ana mamlaka na vyombo vya mabavu, kama vile polisi.
Unapomchagua mtu mwenye akili ndogo, ujue unakaribisha maafa kwa Taifa. Tuwapige vita viongozi wote wenye akili kidogo, na uthibitisho kuwa kiongozi ana akili kidogo, angalia huyo kiongozi anapenda kwa kiwango gani kutumia vyombo vya mabavu.
Ni rahisi sana kiongozi mwenye akili kidogo kutoa amri ya kuua au mtu fulani afungwe hata kama hana hatia, kuliko kwa kiongozi ambaye ni super intelligent.