Hebu tulinganishe Kigali master plan 2040 na Dar es Salaam master plan, (watanzania tumerogwa sio bure)

ego

JF-Expert Member
Apr 10, 2013
1,620
1,407
Jamani nimejaribu kupitia kwenye mitandao kutafuta mipango ya maendeleo ya makazi kwa hii miji miwili Kigali na Dar es salaam.

Nini kimenisukuma kwanza ni kutokana na maneno ninayoyasikia mtaani kuwa kigali rwanda ni kuzuli ni kuzuli.

Nikaingia kwenye youtube nikajaribu kutafuta kigali kwa bahati nzuri nikakutana "kigali master plan 2040" ki msingi nilijisikia kushikwa na wivu sana.

Kwa kifupi mimi katika katika kabila langu wanyarwanda walikuwa wanadhaurika sana tena sana. Hii kudhaurika ni kutokana na maisha yao waliyokuwa nayo huko nyuma ya vita na kuishia kuwa wakimbizi kule kwetu.

Watu hawa walikuwa wakifanya kazi za vibarua na kutuhumiwa kufanya matukio ya uhalifu kwenye jamii yetu hivyo walionekana watu wa chini sana.

Kwenye jamii yetu mtu akiambiwa mnyarwanda ilikuwa tusi kubwa sana. katika jamii yetu hii kuoa mnyarwanda ilikuwa ni kitendo cha kashifa ambacho ilikuwa ni kufanya kituko cha aibu.

Hivyo nilitafuta kutazama kigali nikiwa na mentality ya dharau hiyo kichwani lakini nimestaajabu kuona mipango ya jinsi kigali itakavyokuwa mwaka 2040 sio ya bara hili la afrika labda ulaya au amerika sawa.

Nikataharuki kwa maana waswahili wanasema "ukiona mtu kapiga hatua za kimaendeleo ukaona kawaida bila kusikia taharuki ya wivu ya kujiuliza hivi sisi tunafanya kitu gani? jua wewe upoupo tu.

Nikajaribu kutafuta "Dar es Salaam master plan"

Nilichokutana nacho kimeandikwa kama Dar es Salaam master plan kwenye youtube ni kituko. Nimekutana na porojo za watanzania wamerekodiwa mara wakilalamika majengo ya kihistoria yasibomolewe na porojo tu na picha za mji. Nilijisikia kunyongonyea nikajiuliza hivi natakiwa kudharau wanyarwanda au kujidharau kwa kuwa mtz.

Kama mpaka sasa hatuna master plan ya miji yetu kuona jamani mpango wa maendeleo wa makazi yetu tunaojaribu kuutekeleza ni huu, kuwa labda ikifika mwaka 2040 tunataka kuwa tumefikia hapa. Kila mmoja anatekeleza yake kichwani. Huyu akiamka anasema jangwa tunaweka hiki huyu kile, huyu anajenga hapa yule akija anabomoa.

Jamani wenye dhaman katika jambo hili mnatuangusha, jaribuni kutafuta hiyo kigali "2040 ilivyo mjaribu kuzisukuma miji yetu yote itengeneze dira kama hizo za maendeleo. Mkisha kuwa na hizo dira wekeni kanuni za kutuwezesha kufika huko.

Watu binafsi wajue kufika 2040 makazi yake kulingana na eneo alilopo linatakiwa liweje, manispaa zijue maeneo ambayo yako chini yao yanatakiwa yaweje, n.k.

Tukiwa na mipango tutafika lakini tukifanya bila mipango hatuwezi kufika popote. Maendeleo ni sawa na ujenzi wa nyumba ukijenga nyumba bila ramani leo unajenga chumba kimoja kesho unabomoa hapa unaongeza chumba pale utakuwa na nyumba kubwa mwishoni lakini isiyoeleweka na hivi ndivyo tunavyojenga miji yetu.

hii ndio kazi ya msingi ya wale wenye dhamana ya ardhi na maendeleo ya makazi kwa mijini.
 
Jamani nimejaribu kupitia kwenye mitandao kutafuta mipango ya maendeleo ya makazi kwa hii miji miwili Kigali na Dar es salaam.

Nini kimenisukuma kwanza ni kutokana na maneno ninayoyasikia mtaani kuwa kigali rwanda ni kuzuli ni kuzuli.
na ya ardhi na maendeleo ya makazi kwa mijini.
Sisi tupo tunakomaa na ilani ya chama kile huku tunasifu ujenzi wa fly over zisizokua na kwenye city plan
 
Kazi tunayo sana na ukikutana na wataalamu wetu waliobobea watakupigia pwelepwete kibao wemwenyewe utaona Kigali sio kitu. Hiyo ni Tanzania
 
Usirudie tena kufananisha DSM Na vitu vya kawaida..Dar ea salaam inapaa pita Ubungo ujionee mji wa kisasa utakavyokuwa
 
Kwani hizo pesa za huo mpango Ni sawa na zile walitoa wakorea shirica la JICA Kwa ajili ya DOM.KIGALI KINA CHO I FEVER NI NDOGO
 
Sisi tupo tunakomaa na ilani ya chama kile huku tunasifu ujenzi wa fly over zisizokua na kwenye city plan

Mambo mengine tunafanya mambo ya aibu, nakumbuka miaka ya tisini na mwisho na elfu mbili na mwanzo nilikuwa nasoma chuo, nilipanda treni ya kati kutokea huko nikiwa na kijana mmoja ambaye ilikuwa mara yake ya kwanza kuja Dar. Tulipofika maeneo ya pugu watu kwenye treni wakasema tumeingia Dar, basi kijana akatoa macho yote nje kuitazama Dar.

Tukasafiri we kutokea pugu tukaenda, tulipofika maeneo ya vingunguti kijana uvumilivu ukamshinda ikabidi anigeukie aniulize hivi hii ndio Dar au ? mbona inazidiwa hata na mikoa huko tulikotoka? Nadhani kwa wale waliowahi kupanda treni ya katika katika maeneo hayo wanaelewa.

Ki msingi hulka za binadamu zilivyo ni kwamba huwa na tabia za kuyazoea mazingira yaliyomzunguka. Mwanadamu akikaa kwenye mazingira fulani kwa mda mrefu basi anaanza kuyazoea hayo mazingira na kuyaona kama ndiyo maisha yake na kujenga negativity ya mabadiliko.

Hivyo maeneo mengi ya makazi yetu sio kwamba hayabadiliki kutokana na hali za maisha za wakazi wa maeneo hayo bali ni kutokana na wakazi wa maeneo hayo wamekwisha kuyazoea maeneo hayo na wanayaona ya kawaida na ndivyo wanavyotakiwa kuishi.

Hapa ndipo serikali hutakiwa kuingilia kwa sheria kuwapa mwongozo wa makazi yao yanatakiwa kuwaje.

ila ukiwa na viongozi wale wale basi unakumbana na tatizo lile lile kwenye uongozi kwa kuwa na viongozi wanaoamini mazingira hayo hayawezi kubadilika kwa kusingizia watu walikwisha kaa hivyo kuona kama ukitaka kubadilisha maeneo hayo labda uwalipe watu fidia uwaondoe upajenge upya.

Kama nikiwa kiongozi mtu mwenye mawazo kama ya hivyo ya kwanza uwalipe watu uwaondoe ndio upaendeleze namwambia kaa pembeni nafasi hii inahitaji mtu anayeamini mabadiriko yanaweza kufanyika! period.

Nyuma yoyote inaweza kubadilishwa vyovyote kupitia "renovation" mitaa inaweza kubalishwa mionekano cha msingi pale unapofanya mabadiliko basi ni lazima kuzingatia vitu vilivyopo viendelee kutumika kwa asilimia kubwa.

Najaribu kuwa tutakavyokuwa tukipita maeneo ya vingunguti kwenye treni la umeume likiwa juu huku tukitazama mandhari za vingunguti, kipawa, banana, mombasa, gongo la mboto, pugu na kadhalika.

maendeleo ya mji yanatakiwa yaende pamoja.

tujenge miundo mbinu huku tukiachia fedha ziende kwa wananchi na kuwabana kwa kutumia sheria na kanuni ili nao waboreshe mazingira yao
 
Jamani nimejaribu kupitia kwenye mitandao kutafuta mipango ya maendeleo ya makazi kwa hii miji miwili Kigali na Dar es salaam.
a hivi ndivyo tunavyojenga miji yetu.

hii ndio kazi ya msingi ya wale wenye dhamana ya ardhi na maendeleo ya makazi kwa mijini.
Amerogwa Jiwe na CCM mkuu, sisi tuko salama mikononi mwa Kristo Yesu
 
Kwani hizo pesa za huo mpango Ni sawa na zile walitoa wakorea shirica la JICA Kwa ajili ya DOM.KIGALI KINA CHO I FEVER NI NDOGO
wabongo majua kujitetea,

china ikipaa mnasema china kinachoifever ni wingi wa watu kwa maana soko lake ni kubwa, haya

Rwanda ikipaa mnasema rwanda kinachoifever ni udogo sasa wapi na wapi?

Dar ikiwa na watu wengi zaidi maana yake ina mzunguko mkubwa wa fedha, shughuli za kibiashara zitakuwa ni nyingi na makusanyo ya kodi yanayokusanywa na serikali yanayotakiwa kutumika kuendeleza mji yatakuwa makubwa.

Chukulia mfano mdogo tu wa umoja wa wafanya kazi. Chama cha walimu kina uwezo mpaka wa kujenga majengo ya vitega uchumi kwa sababu kina wanachama wengi. kwa wingi wao hata kila mwanachama akichanga shlingi elfu moja tu ya maendeleo wao ndani ya miezi sita wanasimamisha jengo la kitega uchumi lakini mkiwa na chama kina wanachama mia tu basi mkichanga elfu moja moja basi yote itaishia kwenye posho za viongozi kwenye vikao. Hata ipite miaka 10 hamtafanya chochote.

Lakini hapa mambo ni tofauti, wachache kama wanafanya hayo wanayoyafanya basi sisi wengi tuna nafasi kubwa zaidi ya kufanya makubwa zaidi lakini uvivu na kukosa focus ndio kikwazo
 
Dar es salaam Kuzuri
Wewe Huna Uzalendo
Nenda Kaishi Kigali 🤣😁😃😂👍
 
Dar es salaam Kuzuri
Wewe Huna Uzalendo
Nenda Kaishi Kigali 🤣😁😃😂👍

Tunahitaji tafsiri ya neno uzalendo maana hatuwezi kukumbatia mambo yanayoturudisha nyuma kwa kuyavisha ngozi ya uzalendo.
 
Kigali hakuna siasa kule ni jeshi la mtu mmoja tu kule hakuna watu neutral kule ILA siku Kagame aking'oka ndo basi tena sidhani kama ataacha taasis imara na zenye uadilifu.
 
Usirudie tena kufananisha DSM Na vitu vya kawaida..dar ea salaam inapaa pita ubungo ujionee mji wa kisasa utakavyokuwa
Hizi sifa ndio inabidi tuziache tufanye utekelezaji,sifa za hivi zinalevya watendaji wanakaa wanaamini wapo sawa,lazima tujifunze kukikubali kiwango chetu ila sio kukizidisha,pia jitihada nazo kuziunga mkono,bila kusahau kupinga Rushwa na Ufujaji uliosababisha chuki kuu kwa raia wengi kwa Serikali yao
 
Screenshot_20181115-173403.jpg
IMG_20181025_142442.jpg
We jamaa usifananishe dar es salaam na vitu vya ajabu..

Wao wanaongea kuwa na mpango wa BRT 2040, sisi huku tunatumia now,

wao wanaongelea kuwa na tren za umeme 2040 sisi huku tunaanza kutumia mwakani hizo tren.
Wao wana panga kujenga majumba ya kufanya mji wao uwe na mvuto2040..
Sisi huku hata nafasi hapo posta hakuna kumejaa migorofa tu...
Nasema hivi hatuwezi kuwa sawa na dubai sijui hong kong au New York huko ila kwa hizi nchi wenzetu za dunia ya tatu tupo vizuri kwa kiasi chake na tunaweza kuwatambia tu..
 
kwa dar master plan ya 2040 sio lazima kwani kwa tafiti za wataalamu kufika 2070 sehemu kubwa ya dar itakuwa imemezwa na maji kwa sababu ya ongezeko la joto duniani ndio maana unaona serikali ya awamu hii inaharakisha kuhamia dodoma
 
Back
Top Bottom