G Sam
JF-Expert Member
- Apr 20, 2013
- 11,555
- 35,880
Juzi niliona picha ya Rais Magufuli akimuombea mama yake mzazi ambaye amepatwa na maswahibu kama yaliyokatisha uhai wa binti yake ambaye alizikwa hivi karibuni.Nilipomuona nilijikuta nikiwaza sana!
Turudi kwenye mada. Ben Saanane mara ya mwisho kabla hajapotea alitoka kwao asubuhi kama kawaida kwenda kwenye mihangaiko ila hakurudi tena hadi leo. Siku chache baada ya kupotea namba yake ikaondolewa kwenye makundi yote ya WhatsApp naamini alikuwa akishurutishwa fanya hili...fanya hili...Siku baada ya siku hadi alipomaliza yote. Mbaya zaidi kuna ujumbe aliotuachia "Tuutafakari" ambapo alikuwa akilalamika kuwa yupo mtu mmoja alikuwa akimtumia ujumbe kila alipokuwa akiishambulia elimu ya mfalme kule kisiwani kwenye mitandao ya kijamii kuwa "mara umebakiza post tatu mara mbili" na mwisho kabisa akamwambia "Naamini sasa hutapost tena" Ujumbe zaidi aliambiwa "Baba yako atajilaumu sana kwa kukusomesha na sasa hatayafaidi matunda ya elimu yako,Ben wewe bado ni kijana mdogo sana kufa"
Ninachoamini ni kuwa dola inajua kabisa yaliyomkuta Ben. Kama sivyo basi wangeshachukua hatua stahiki. Emb fikiria watu wote waliokuwa wamekithiri kwa ukosoaji kipindi kile walifanywa nini? Tundu Lissu mbunge na mwanasiasa maarufu sana alishambuliwa kwa risasi nyingi mchana kweupe tena mbele ya makazi yenye ulinzi mkali na hakuna chochote mpaka leo. Njoo kwa kuke kwa ofisi za Fatuma Karume hadi bomu likarushwa kwenye ofisi zao. Kina Roma walivyopigwa kwenye majumba yasiyojulikana! Itakuwaje kwa Ben aliyekuwa naye amekithiri kwa ukosoaji?
Mimi naweza kufikiria haya na huenda moja wapo likawa sahihi
1. Huenda Ben kapigwa ban labda kwa kipindi fulani....Ila hapana, siku wakimtoa huko je? Si wataaibika?
2. Huenda walidhamiria kumpiga kisha wamuachie ila wakazidisha kipigo na ikawa bahati mbaya jumla!
3. Au moja kwa moja walimmaliza.
4. Au labda walimpa ofa ya kwenda nchi za watu kukaa tu huko ili asiwe tena anashambulia....Thubutuuu yani mfalme umkosoe, uwe mfuasi wa "mabeberu" halafu akupeleke kula bata?
Wazo namba 2 linanishawishi nikubaliane nalo zaidi kwakuwa naamini hata kina Roma Mkatoliki na wenzake walipokuwa wanapigwa kama ingetokea bahati mbaya iwe jumla basi nao wasingeonekana mpaka leo.Linanishawishi nikubaliane nalo kwakuwa wote waliokosoa walielekezwa kwenye mfumo huu wa kupotezwa ila baadhi yao Mola akawanusuru!
Kuna kile kipindi maiti zilikuwa zinaokotwa kiholela sana kule baharini mara mto Ruvu huku zikiwa zimefungwa kwenye viroba. Hiki ndicho kipindi kile cha kukamatwa watu kule MKIRU na kwenda kuona joto la motoni kule Stakishari! hiki ndicho kipindi kilichokuwa muda mfupi tu tangia Ben atoweke. Ndicho kipindi alichopotea Azory.........Mbona siku hizi zile maiti za "wahamiaji haramu" hazipo tena? Kwanini kipindi kile ziliibuka sana zikiwa zimefungwa kwenye mifuko huku sisi wengine tukielewa kuwa kule Stakishari kulikuwa na kwata la kufa mtu likiendelea? Hadi watu wakawa wanatambaa kama nyoka? Kwanini kwanini kwanini?
Ukweli wa haya naamini kuwa hautajulikana kama tutaujenga "mfumo mfalme wa kisiwa" kama tulivyotahadharishwa humu Jf......"Mfumo mfalme huyu" ni hatari kwa afya yetu hivyo tuchukue tahadhari mapema sana.
Turudi kwenye mada. Ben Saanane mara ya mwisho kabla hajapotea alitoka kwao asubuhi kama kawaida kwenda kwenye mihangaiko ila hakurudi tena hadi leo. Siku chache baada ya kupotea namba yake ikaondolewa kwenye makundi yote ya WhatsApp naamini alikuwa akishurutishwa fanya hili...fanya hili...Siku baada ya siku hadi alipomaliza yote. Mbaya zaidi kuna ujumbe aliotuachia "Tuutafakari" ambapo alikuwa akilalamika kuwa yupo mtu mmoja alikuwa akimtumia ujumbe kila alipokuwa akiishambulia elimu ya mfalme kule kisiwani kwenye mitandao ya kijamii kuwa "mara umebakiza post tatu mara mbili" na mwisho kabisa akamwambia "Naamini sasa hutapost tena" Ujumbe zaidi aliambiwa "Baba yako atajilaumu sana kwa kukusomesha na sasa hatayafaidi matunda ya elimu yako,Ben wewe bado ni kijana mdogo sana kufa"
Ninachoamini ni kuwa dola inajua kabisa yaliyomkuta Ben. Kama sivyo basi wangeshachukua hatua stahiki. Emb fikiria watu wote waliokuwa wamekithiri kwa ukosoaji kipindi kile walifanywa nini? Tundu Lissu mbunge na mwanasiasa maarufu sana alishambuliwa kwa risasi nyingi mchana kweupe tena mbele ya makazi yenye ulinzi mkali na hakuna chochote mpaka leo. Njoo kwa kuke kwa ofisi za Fatuma Karume hadi bomu likarushwa kwenye ofisi zao. Kina Roma walivyopigwa kwenye majumba yasiyojulikana! Itakuwaje kwa Ben aliyekuwa naye amekithiri kwa ukosoaji?
Mimi naweza kufikiria haya na huenda moja wapo likawa sahihi
1. Huenda Ben kapigwa ban labda kwa kipindi fulani....Ila hapana, siku wakimtoa huko je? Si wataaibika?
2. Huenda walidhamiria kumpiga kisha wamuachie ila wakazidisha kipigo na ikawa bahati mbaya jumla!
3. Au moja kwa moja walimmaliza.
4. Au labda walimpa ofa ya kwenda nchi za watu kukaa tu huko ili asiwe tena anashambulia....Thubutuuu yani mfalme umkosoe, uwe mfuasi wa "mabeberu" halafu akupeleke kula bata?
Wazo namba 2 linanishawishi nikubaliane nalo zaidi kwakuwa naamini hata kina Roma Mkatoliki na wenzake walipokuwa wanapigwa kama ingetokea bahati mbaya iwe jumla basi nao wasingeonekana mpaka leo.Linanishawishi nikubaliane nalo kwakuwa wote waliokosoa walielekezwa kwenye mfumo huu wa kupotezwa ila baadhi yao Mola akawanusuru!
Kuna kile kipindi maiti zilikuwa zinaokotwa kiholela sana kule baharini mara mto Ruvu huku zikiwa zimefungwa kwenye viroba. Hiki ndicho kipindi kile cha kukamatwa watu kule MKIRU na kwenda kuona joto la motoni kule Stakishari! hiki ndicho kipindi kilichokuwa muda mfupi tu tangia Ben atoweke. Ndicho kipindi alichopotea Azory.........Mbona siku hizi zile maiti za "wahamiaji haramu" hazipo tena? Kwanini kipindi kile ziliibuka sana zikiwa zimefungwa kwenye mifuko huku sisi wengine tukielewa kuwa kule Stakishari kulikuwa na kwata la kufa mtu likiendelea? Hadi watu wakawa wanatambaa kama nyoka? Kwanini kwanini kwanini?
Ukweli wa haya naamini kuwa hautajulikana kama tutaujenga "mfumo mfalme wa kisiwa" kama tulivyotahadharishwa humu Jf......"Mfumo mfalme huyu" ni hatari kwa afya yetu hivyo tuchukue tahadhari mapema sana.