Hebu ' nishawishini ' na Mimi niamini kwamba Hayati Ghaddafi ndiyo alikuwa akiwatendea vyema Wananchi wake

Ghadafi alikua mtu wa hovyo tu, yaani kisa umenilipia mahari, umenipa nyumba na umeniwekea pesa kwenye account bila ya kuvifanyia kazi basi niendelee na maisha tu. Yaani kama nataka kuwa mfanyabiashara mkubwa au mwanasiasa nifute hizo ndoto sababu tu naoa, nakula na kulala kwenye nyumba nzuri!!
Kwa mbongo huyo ndiyo kiongozi

Kama ikitokea nikaambiwa nichague JamiiForums Members Kumi ( 10 ) tu ninaowakubali kwa 100% kuwa wana ' IQ ' kubwa basi Wewe na Bila bila hamtakosekana katika hiyo idadi. Na sikusifii hivi au siwasifieni hivi labda nikimaanisha kuwa huwa mnakubaliana na ' Mabandiko ' yangu hapana kwani kuna ' Mabandiko ' yangu mengine huwa tunapishana ' Kimtizamo ' ila ninachopenda Kwenu nyie ni kwamba mnajua sana Kujenga Hoja na Kuzitumia vyema kabisa ' akili ' zenu katika ' Uwasilishaji ' wa masuala mbalimbali hapa Jamvini.
 
gadafi alishindwa kusoma alama za nyakati! binadamu sio mnyama wa kufugwa, kwamba kwakua unampa chakula, maji na malazi basi utegemee ataridhika! wanyime watu kilakitu lakini wape uhuru wa kuchagua
Hata huyo mbwa ukimletea za kuleta pamoja na mavyakula yako anakugeuka na kukufanzia kitu mbaya usipopata chanjo unapata kichaa cha mbwa kifuatacho itv2 rip zinatiririka.
 
Libya ndo nchi yenye visima vingi vya mafuta na gesi barani Afrika.

Libya ni nchi ya tisa kwa ukubwa duniani.

Libya ni nchi ambayo ndo unapita kuingia barani humo kupitia bahari ya Mediterranean.

Mabomba mengi ya mafuta na gesi yametokea Libya kwenda ng'ambo ya bahari ya Mediterranean.

Kwa muda mrefu nchi za Italia na Ufaransa zimekuwa zikigombania Libya kupitia kampuni zao za mafuta za Eni na Total.

Eni ya Italy ipo Libya tangu mwaka 1959 na Total ameikuta Eni Libya.

Kampuni hizi mbili ndizo zinazofadhili migogoro inayoendelea nchini humo kwa kuwapatia fedha makundi mbalimbali yalojitokeza baada ya Libya kusambaratishwa na Gaddafi kuuawa.

Uchaguzi na serikali ya Libya ya sasa ambayo ni ya vibaraka, vinasimamiwa na nchi za Italia na Ufaransa.

Tangu mwaka 2014, Italia imeweka kambi ya kijeshi mjini Mistrata na kuna wanajeshi 350 hapo kazi yao ikiwa ni kulinda visima vya mafuta na kuwafunza askari wa majini wa kuzuia wazamiaji wa Ulaya.

Gaddafi aliuawa kwa njama zilizofanywa na nchi za magharibi kwa kushirikiana na vibaraka ambao ni wananchi wa Libya.

Mwaka 2008 Italia iliingia mkataba na Gaddafi ambapo waziri mkuu wa italia Berlusconi alikubaliana na Gaddafi kwamba wahamiaji wa Ulaya watadhibitiwa na Italia ilailipa Libya fidia ya makosa yalotokana na ukoloni.

Lakini Gaddafi pia akakubaliana na Italia kwamba angawapa sehemu kubwa ya visima vya mafuta kupitia kampuni yao ya Eni.

NATO ikiongozwa na Ufaransa, Uingereza na Marekani (ambao walikwishapanga na vibaraka kumuondoa Gaddafi) ikakataa makubaliano hayo ya Italia na Libya na ikaamua Gaddafi aondolewe na kuuawa.

Lakini Italia haikukaa kimya bali iliamua kusaidia kampeni ya vita kwa Libya kwa kutumia kambi yake ya kijeshi mjini Sicily ambako mashambulizi yote ya makombora ya Majeshi ya NATO yalitokea hapo.

Kiongozi wa Libya wa sasa ni mmoja wa vibaraka wa nchi za magharibi aitwae Fayez al-Sarraj na hana madaraka makubwa kutokana na jeshi la nchi hiyo kuwa mikononi mwa wanamgambo.

Wanamgambo hao ndo wanashikilia njia kuu za uchumi wa Libya, visima vya mafuta, magereza mbalimbali, vikosi vya mauaji na ndo wanashirikiana na nchi mbalimbali za magharibi kwenye baadhi ya shughuli zingine za kiuchumi kama ubadilishaji fedha.

Ni vikosi hivi vya wanamgambo ambavyo zimeifanya Libya kuwa nchi ambayo uchumi wake umeporomoka kama mvua na kuwaacha wananchi walio wengi maskini wa kutupwa.

Libya nchi ambayo elimu na huduma za Afya zilikuwa ni bure leo hii imeghubikwa na matatizo kama ukosefu wa maji, umeme wa uhakika na hata huduma za mfumo wa vyoo zimevurugwa.

Libya sasa hivi kupata chakula ni shida na hata kukipata inabidi ulipie gharama kubwa huku chakula chenyewe kikiwa ni adimu.

Libya leo imekuwa ni nchi huru na inayouza raia wake ng'ambo kama watumwa.

Gaddafi kuna sehemu alifeli.
 
Yaani kila ukipita utasikia Watanzania wanamsifia sana na kumpamba mno aliyekuwa Rais wa Libya Ghaddafi na ukizisikia sababu zao wanazokupa za Kumsifia kote huko hazina Kichwa wala miguu sana sana ni za Kidhaifu mno.

Naombeni leo nami mnishawishi niamini kuwa Ghaddafi alikuwa ni bonge la Rais hapa Barani Afrika.

Nawasilisha.
Ni sababu kama zipi huwa unazisikia toka kwao ambazo hazina kichwa wala miguu?
 
Alijimilikisha nchi ikawa ya kwake, yeye na familia yake, hata walipombana akataka kumlisisha mwanawe,.kama hapa ccm wamavyofanya.
 
Pesa yote ya mafuta Libya ilikuwa mali binafsi ya Gadafi na yeye ndiye aliamua ataitumia vipi. Ukisika umehoji matumizi ya pesa kesho unapotea, ndugu watatafuta mwisho wanasoma hitma.
 
..Gaddafi alimsaidia Iddi Amini wakati wa vita vya Kagera.

..Gaddafi alimwaga DAMU ya askari wetu waliokwenda mstari wa mbele Uganda.

..inanishangaza sana wanapotokea waTz wenzetu, tena ni viongozi na wana elimu kubwa-kubwa, na kuanza kumsifia na kumsujudia Gaddafi.

..Ni kweli kwamba Mwalimu Nyerere kwa niaba ya waTz alirudisha mahusiano na Gaddafi. Lakini kwa maoni yangu, kuanza kumlilia na kumsifia Gaddafi ni kutowathamini askari wetu waliopoteza maisha au kupata vilema kutokana na mashambulizi ya askari wa Gaddafi.
 
Deep inside unaweza kuta source ya kutoa comment ya chuki ya namna hii ni kwa sababu za kidini.
mbwewe acha kulisha watu maneno/mawazo kama ni chuki za dini, na aliowafanyia hayo mambo ni dini ileile.
 
Ghadafi alikua mtu wa hovyo tu, yaani kisa umenilipia mahari, umenipa nyumba na umeniwekea pesa kwenye account bila ya kuvifanyia kazi basi niendelee na maisha tu. Yaani kama nataka kuwa mfanyabiashara mkubwa au mwanasiasa nifute hizo ndoto sababu tu naoa, nakula na kulala kwenye nyumba nzuri!!
Kwa mbongo huyo ndiyo kiongozi
Kuna watanzania wamejaliwa akili dhaifu sana. Wanawaza ngono, tumbo, na umbea.
 
Yaani kila ukipita utasikia Watanzania wanamsifia sana na kumpamba mno aliyekuwa Rais wa Libya Ghaddafi na ukizisikia sababu zao wanazokupa za Kumsifia kote huko hazina Kichwa wala miguu sana sana ni za Kidhaifu mno.

Naombeni leo nami mnishawishi niamini kuwa Ghaddafi alikuwa ni bonge la Rais hapa Barani Afrika.

Nawasilisha.
Walibya wenyewe ndio wanasema hivyo kama gadafi alikuwa mtu mzuri. Sio watz
 
Kwangu mimi Ghadafi ni gaidi kama magaidi wengine, kitendo cha kumsaidia Idd Amini Dada kuiteketeza Tanzania kinanifanya nimchukie jumla.
Kwa hiyo nyerere nae kuzisaidia nchi nyingine kupata uhuru alikuwa gaido
 
Pesa yote ya mafuta Libya ilikuwa mali binafsi ya Gadafi na yeye ndiye aliamua ataitumia vipi. Ukisikaka umehoji matumizi ya pesa kesho unapotea, ndugu watatafuta mwisho wanasoma hitma.
Western propaganda
 
Back
Top Bottom