PakaJimmy
JF-Expert Member
- Apr 29, 2009
- 16,203
- 8,723
Mimi na mdogo wangu wa kike ambaye anasoma form 3 tumehamia makao mapya. Nyumba hiyo tuliyohamia inatazamana na nyumba ya majirani fulani, ambapo kuna watoto kadha wa kike na wa kiume.
Kipindi fulani nilipata kugundua kwamba dogo fulani wa nyumba hiyo ya jirani anamfukuzia mdogo wangu kwa udi na uvumba.
Najua mdogo wangu hadanganyiki, lakini ishu hiyo iliniboa kishenzi maana namsomesha huyu dadangu kwa kujinyima. Nikaamua kiume kumwita huyo dogo mbele ya wazazi wake na kumpa maneno makali na kumtaka aachane na kumlostisha dadandu haraka iwezekanavyo.Dogo alikoma na hiyo tabia moja kwa moja hadi sasa.
Lakini, ndugu mwanaJF, NAPENDA nikwambieni kwamba Kitabu kimenirudia mimi sasa.
Ni kwamba kumbe nyumba hiyo ina mdada mmoja ambaye alikuwa sijui safari...sijui labda college, sa ndo kawasili hapa majuzi kati. Huyo dada ni mtata wandugu. Yuko bomba mwanzo-mwisho, yaani amekamilika, na pia ni mpole, anasalimia fresh mbaya!.
Kwakweli, kwahali aliyo nayo, niko tayari kubeba kwa jumla.
Nilipofuatilia mtaa wakanambia yuko single, ambapo nami niko hivyo!
Sasa wanaJF itakuwaje hii mambo, je hawa akina dogo mashemeji watanielewaje na watanipokeaje?
Embu nipeni ushauri jamani, nateseka na huyu mdada!
Kipindi fulani nilipata kugundua kwamba dogo fulani wa nyumba hiyo ya jirani anamfukuzia mdogo wangu kwa udi na uvumba.
Najua mdogo wangu hadanganyiki, lakini ishu hiyo iliniboa kishenzi maana namsomesha huyu dadangu kwa kujinyima. Nikaamua kiume kumwita huyo dogo mbele ya wazazi wake na kumpa maneno makali na kumtaka aachane na kumlostisha dadandu haraka iwezekanavyo.Dogo alikoma na hiyo tabia moja kwa moja hadi sasa.
Lakini, ndugu mwanaJF, NAPENDA nikwambieni kwamba Kitabu kimenirudia mimi sasa.
Ni kwamba kumbe nyumba hiyo ina mdada mmoja ambaye alikuwa sijui safari...sijui labda college, sa ndo kawasili hapa majuzi kati. Huyo dada ni mtata wandugu. Yuko bomba mwanzo-mwisho, yaani amekamilika, na pia ni mpole, anasalimia fresh mbaya!.
Kwakweli, kwahali aliyo nayo, niko tayari kubeba kwa jumla.
Nilipofuatilia mtaa wakanambia yuko single, ambapo nami niko hivyo!
Sasa wanaJF itakuwaje hii mambo, je hawa akina dogo mashemeji watanielewaje na watanipokeaje?
Embu nipeni ushauri jamani, nateseka na huyu mdada!