Hazina imekauka - pensheni za wastaafu zakatwa

Wacha wakatwe tu hizo ela zao. Wazee hawa hawa si ndo wanasema ccm imewalea, ccm inawafanya waishi kwa amani, afu kipindi cha uchaguzi si wanaipigia kura ccm, huku wakiwa na nyuso za furaha kwenye ma t-shit na makofia yao ya njano na kijani...
Baba mwanaasha endelea kuwapini mpaka wakome!

Jamani si wazee wote wanaoipigia chapuo CCM! Kuna wazee wamezinduka siku nyingi, kwa mfano baba yangu mie ni mstaafu na anapokea hizo laki 3 kila baada ya miezi 6! yaani kama sisi watoto wake hatumpi tafu mzee anaadhirika! Wazee wengi wastaafu ni wale ambao walikuwa waaminifu na watiifu kwa serikali yao, walilelewa chini ya Azimio la Arusha hivyo hata kuiba hawakujua! Hao ndio wanaopigika kwa sasa maana waliamini kwenye mshahara tu.

Kwa nini wasiwakate Wabunge??? kuwakata wazee hao dhambi hiyo itakuwa juu yao wao pamoja na vizazi vyao!
 
Kilio hiki kipo kweli. Wazee wanalalamika na hawajui nini wafanye. Serikali haitakiwi kuwachakachua wazee hawa, bora kuangalia namna nyingine lakini si kuwachakachua wazee!
kumbuka waliyotendewa wazee wa east afrika
ndio utajua tuko kwenye nchi ya namna gani.
 
Hiyo serikali haiwatendei haki hao wazee hyo balaa. Kwann wanawanyanyasa kwa sababu hakuna wakuwatetea!.
 
Kilio hiki kipo kweli. Wazee wanalalamika na hawajui nini wafanye. Serikali haitakiwi kuwachakachua wazee hawa, bora kuangalia namna nyingine lakini si kuwachakachua wazee!

Heshima kwako mkuu invisible, Hawa wazee si pamoja na wale wanaoitwa wazee wa Dar es Salaam? Si ndo walikuwa wanamshangilia mkuu wa kaya wakati anamsema Mgaya? Si ndo wanajiita mtaji wa CCM? Nawatakia kila la heri. Daima wakumbuke kuwa kucheka na nyani unavuna mabua.
 
Hawakurushwa pensheni tena 2007? Tena ya miezi 6? Halafu inavyoonekana kuanzia July 2011 hadi December 2011 hawajalipwa, maana eti wanalipwa ya miezi mitatu mitatu ambayo ni Januari hadi Machi 2012. Mwenye taarifa sahihi zaidi atujuze tafadhali.Ni janga!
 
Wakuu heshima mbele,
Naomba kusahihisha ,serikali haijakata pensheni za wazee ila wanawalipa kwa miezi mitatu mitatu na sio kwa miezi Sita Sita tena.in short ndio hivyo
 
Badala ya kuwaonea hawa wazee wastaafu, kwanini wasawakate viongozi wakuu wa KITAIFA wastaafu ambao ndiyo wanapata marupurupu makubwa eg 80% ya mshahara wa kiongozi aliyeko madarakani, mishahara ya walinzi wawili, dereva 1, House Maid 1, posho ya mafuta etc. Viongozi hawa tunao lundo na serikali ingeweza kupata mi-pesa mingi kutoka kwao
  1. Julius Kambarage Nyerere
  2. Rashid Mfaume Kawawa
  3. Edward Moringe Sokoine
  4. Alhaji Ali Hassan Mwinyi
  5. Aboud Jumbe Mwinyi (VP)
  6. Abdul Wakil Juma
  7. Dr. Omari Ali Juma
  8. David Cleopa Msuya
  9. Salim Ahmed Salim
  10. Joseph Sinde Warioba
  11. John Samwel Malecela
  12. Benjamin William Mkapa
  13. Frederick Tuluway Sumaye
  14. Edward Ngoyayi Lowassa
  15. Adam Sapi Mkwawa (Speaker)
  16. Pius Msekwa
  17. Samuel Sitta (?)
  18. Francis Nyalali (CJ)
  19. Augustin Ramadhani

huyu mzee alishafariki kuna habari walimchakachua maana lilikuwa jembe hasa
 
Wakuu heshima mbele,
Naomba kusahihisha ,serikali haijakata pensheni za wazee ila wanawalipa kwa miezi mitatu mitatu na sio kwa miezi Sita Sita tena.in short ndio hivyo
Mkuu,

Huenda hujui kuwa wengine tunaoandika hapa yawezekana ndo 'wazee' wenyewe.

Maelezo yanayotolewa na 'vijana' ni tofauti na unachosema hapa. Wao wamesema michango 'yetu' iliyolipwa ni ya Jan-March 2012 ilhali ilitakiwa kulipwa ya tangu July 2011 kwa kipindi cha miezi 6. Maelezo haya ukiuliza utaambiwa na 'wenzangu' wengine mikoani.

Wengine walipandwa na jazba na kufikia kutoa kauli za '2015 hatuichagui CCM'.

Niseme, hii inawapunguzia wazee siku zao za kuishi, ni mauaji ya polepole!
 
Siwezi kuongelea kukauka kwa Hazina ila kuna mabadiliko katika mgao wa pensheni za wastaafu wanaolipiwa hazina. Kuanzia january mwaka huu serikali imebadilisha utaratibu wa kulipa badala ya miezi sita sita itakua inalipa miezi mitatu mitatu. Huu utaratibu wa miezi sita sita hata mimi mlikua siupendi naona bora watumie wa miezi mitatu mitatu au wakiweza walipe mwezi mmoja mmoja.
Kwa kifupi unataka kusema hii habari si ya kweli? Je huwa analipwa in advance au in arrears? Manake kama wanalipwa in advance itakuwa aawa kwamba wanalipwa za mwezi wa kwanza hadi wa tatu. Lakini kama ni in arrears ina maana wanalipwa kwa miezi ya nyuma kwa utaratibu wa zamani kwa nini walipwe nusu badala ya kulipwa pesa yao yote ya nyuma na kuanza utaratibu mpya kwenye malipo ya match/april kwa ajili ya january - march?
 
Katika kile kinachoonekana sasa serikali imefilisika, imewakata nusu ya pensheni ya wastaafu ya mwezi February.

Kwa mfano wastaafu wengi hupokea sh 300,000 kila baada ya miezi sita. Sasa wamepewa 150,000/=!.

Wacha wachakachuliwe sababu wakati wa uchaguzi wazee ni washabiki wakubwa wa magamba hiyo ndiyo zawadi yao.Tena wengine huwe kimbelembele sana kumbuka yule mzee pale igunga wkati wa uchaguzi maneno aliyokuwa akiyabwabwaja.
 
Wacha wachakachuliwe sababu wakati wa uchaguzi wazee ni washabiki wakubwa wa magamba hiyo ndiyo zawadi yao.Tena wengine huwe kimbelembele sana kumbuka yule mzee pale igunga wkati wa uchaguzi maneno aliyokuwa akiyabwabwaja.

mzee wangu ni cdm kindakindaki japo hana kadi, huwa ananiambia km wewe ni mcha mungu huwezi kubakia CCM! Na alikua bosi wa chama ktk mkoa mmoja na hata kuwa mbunge miaka ya 1980s. Sikumoja alinishangaza tukiwa tunaangalia TV mara wakaweka kipindi maalumu, JK akihutubia taifa....nikaona kachukua rimoti akaweka chanel 5 EATV.
 
huyu mzee alishafariki kuna habari walimchakachua maana lilikuwa jembe hasa

Ninafahamu Judge Francis Nyalali alishafariki dunia kama ambavyo hatunao akina Nyerere, Kawawa, Sokoine, Abdul Wakil Juma, Dr. Omari Ali Juma.

Lakini sheria ya mafao ya viongozi wa KITAIFA kama ilivyorekebishwa na Sophia Simba inasema familia za hao viongozi zitaendelea kupata hayo marupurupu hata kama viongozi hao watakuwa wamekufa.

Yaani akina Vita Kawawa (sorry ni mfano tu) pamoja na wajukuu, vitukuu, vilembwe vitaendelea kupata 80% ya mshahara wa PM current, kulipiwa walinzi wawili, dereva, house girl, na mafuta ya gari.

Huu ni Mzigo mkubwa sana kwa walalahoi. Vilembwe au Vitukuu vya Nyerere, Kawawa, Sokoine, Dr. Omari, Wakili sisi (watanzania)vinatuhusu nini? Haya mambo inabidi yaangaliwe upya kwenye katiba mpya.
 
Katika kile kinachoonekana sasa serikali imefilisika, imewakata nusu ya pensheni ya wastaafu ya mwezi February.

Kwa mfano wastaafu wengi hupokea sh 300,000 kila baada ya miezi sita. Sasa wamepewa 150,000/=!.


Mkapa karudi ikulu?
 
Back
Top Bottom