Hayati Magufuli alikuwa mtawala na siyo kiongozi

Hayati Magufuli aliamini kuwa yeye ana akili kuliko watanzania wote na ndio maana hata alipodanganywa kwa sifa za uongo Kama sio kumkebehi kuwa anajua idadi ya samaki wote kwenye mito, ziwani, na baharini alibaki kukenua kwa kicheko.

Mtawala anapenda sifa usipo msifu una geuka kuwa adui wake mkubwa. Mtawala ana amini katika mabavu hataki mijadala katika kufikia maamuzi. Mtawala ana amini kuwa dawa pekee ya kubaki katika maamuzi yake ya kibabe ni kuwaondoa wote wenye mawazo kinzani na yake, Kama sio kwa kuwafunga jela, Basi ni kwa mauwaji.

Awamu ya tano ndio awamu iliongoza kwa kuwapoteza watanzania wengi walio kuwa na mawazo tofauti na ya mtawala.

Mtawala hata akikaa uchi usimwambie na ukthubutu atakwambia kwanini una mchunguza chunguza wakati nguo aliyovaa inampendeza, ataamuru ukamatwe.

Kuna wakati mbunge mmoja na mbobezi katika siasa za nchi hii, alizungumzia kuwa kitendo Cha Paulo kuvamia ofisi za Cloud media tena kwa mtutu wa bunduki si sawa aliambulia kufukuzwa uwaziri.

Huyo huyo mbunge alipotoa ushauri kuhusu nchi kuwa na miradi mikubwa sio kosa isipokuwa Basi iwekewe kipaumbele yaani ichukuliwe michache michache ili kulinda uchumi wa nchi, alitishiwa hata kufukuzwa ndani ya chama.

Kwa ujumla kiongozi ni yule anaye amini katika kushirikiana katika maamuzi ya pamoja. Na Kama awamu ya tano ingefanikiwa kukaa miaka yote kumi hakika ni kwamba vazi rasmi la Taifa lingekuwa ni kaniki.
Inaelekea pia hujui maana ya Mtawala (Administrator) na Kiongozi (Leader). Administrator ni msimamizi wa sheria kanuni na taratibu, wakati leader ni mtoa kwa dira kwa jamii. Rais hawezi kuwa Kiongozi tu na akaacha kuwa Mtawala ! Unapokuwa na rais ambaye ni kiongozi tu siyo mtawala ndipo nchi inafanya mambo ya hovyo na kuongezeka kwa uvunjanji sheria na kanuni (banana republic).
 
Jamaa alikuwa mubaya sana. Mpka Leo tangu kufa kwake sijasikia watu kutekwa kupotea au kuokotwa, kupigwa risasi na kadharika.

Mungu mkubwa alituondolea huyo
 
Hata Iddi Amin, Kaburu Botha au Hitler?
"Ukikuta mtu anamsimanga marehemu, hayati, au maiti ujue utu wa huyo msengenyaji, msimangaji, ulisha kufa zamani za kale,yaani kitambo, huyo ni msukule huru,ulioachwa uraini uendelea kuvunda taratibu mbele ya ubani." Hivi huyo uliye mwandika hivyo angekuwa ndugu yako, au mwanao ndo kaandikwa hivyo ungejichukuliaje, nafsi mwako?
 
21 Reactions
Reply
Back
Top Bottom