Hayati Edward Sokoine aliwahi kuyasema haya ...

wandamba

JF-Expert Member
Apr 29, 2014
510
839
Tukiwa tunaelekea kwenye maadhimisho ya Kumbukumbu ya Kifo cha Aliyekuwa waziri Mkuu wa Tanzania, Edward Moringe Sokoine aliyefariki April 12 mwaka 1984 kilichotokana na ajali ya Gari eneo la Dakawa Morogoro akitokea mkoani Dodoma, ninakuleta baadhi ya Nukuu bora kabisa kutoka kwake ambazo aliwahi kuzisema.

*Nukuu bora kabisa za Hayati Edward Sokoine*

“Ole wake kiongozi mzembe na asiye na nidhamu nitakayemkuta: Kiongozi wa siasa hana usalama wa aina yoyote. Usalama wake ni kudra ya Mungu na Wananchi peke yake. Viongozi wazembe na wabadhirifu wahesabu siku zao. Labda tusiwajue. Hawa hatuna sababu ya kuwapa imani, kuwa tutawalinda kama vitendo vyao viovu” – Sokoine, 26 Machi 1983

“Wajibu wa kila Mtanzania, kila familia na kila anayekula ni kujilisha mwenyewe. Si wajibu wa Taifa kumlisha mtu. Unaweza ukasaidiwa unapopatikana na janga. Lakini kama hakuna janga ni wajibu wa kila mtu aweze kujitosheleza kwa chakula na atoe ziada kwa Taifa” – Sokoine, 4 Oktoba 1983

“Vijana leo wengi wana mali zaidi kuliko wazee waliofanya kazi miaka thelathini hadi arobaini. Lakini wanaitaka Serikali ndiyo iwaulize mali hiyo wameipata wapi. Hivi kwa nini mzazi asimuulize mwanae, ‘mali hii umeipata wapi?'” – Sokoine, 23 Oktoba 1983

"Juu ya suala hili la mapato kutolingana na matumizi ni kwamba tungependa kupunguza uongezaji wa wataalam katika Serikali na mashirika ya umma mpaka hapo hali yetu ya uchumi itakapokuwa katika hali nzuri" - Sokoine, 23 Oktoba 1982.

"Serikali inasimamia bei, lakini Serikali yetu itakwenda mpaka itasimamia bei ya mhogo, dagaa na being ya kila kitu? Haiwezekani, vitu vingine ni lazima vizalishwe kwa wingi I'll bei yenyewe iweze kujirekebisha" - Sokoine, 24 Septemba 1983

Hakika, Watanzania na Taifa kwa ujumla watakukumbuka daima. Pumzika kwa amani Mzalendo, shujaa na mchapa kazi Edward Sokoine.
FB_IMG_1554839317007.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
hakika huyu baba angekuwa rais ingeandikwa historia nzito sana katika taifa letu ila mipango ya Mungu ni mkuu kwa kutupatia Magufuli wa mfano wake

..siyo kweli.

..aliumiza wananchi wasio na hatia ktk zoezi lake la kukamata "wahujumu uchumi."

..matatizo yetu ya uchumi yalisababishwa na uongozi na usimamizi mbaya wa utawala wa wakati ule, na siyo hao waliopewa jina baya la "wahujumu uchumi."
 
kwa jinsi jina lake lilivyokuwa kubwa nilitegemea kukuta vitu deep kuliko hivyo
 
hakika huyu baba angekuwa rais ingeandikwa historia nzito sana katika taifa letu ila mipango ya Mungu ni mkuu kwa kutupatia Magufuli wa mfano wake

Ukweli ni kwamba mtu ambaye anasema Sokoine angekuwa raisi bora sana, hapaswi kulalamika kuhusu Magufuli. Magufuli ana silka iliyo karibu sana na Sokoine.

Ukweli ni kwamba wote Sokoine na Magufuli hawakufaa kuwa maraisi wa nchi, lakini walifaa sana kuwa mawaziri wakuu. Mtu kama Magufuli angefaa sana kuwa waziri Mkuu chini ya raisi kama Kikwete, kama ambavyo Sokoine alifaa kuwa waziri mkuu chini ya raisi Nyerere. Nyerere mara nyingi sana alikuwa akimdhibiti Sokoine asipite kiasi.
  • Sokoine kuna wakati alitaka kumtia ndani Kawawa kwa mambo ya uhujumu uchumi - Nyerere akamwambia wewe Edward, unataka kuleta mgawanyiko serikalini
  • Sokoine alitaka wahujumu uchumi wafungwe bila kufikishwa mahakamani, Nyerere akasema haiwezekani, lazima tuonekane tunafuata utawala wa sheria
  • Sokoine alitaka ukihitimu elimu kama chuo kikuu usikabidhiwe cheti kwa kuwa umesomeshwa na serikali, Nyerere akasema acha wanaoweza kutafuta fursa zaidi sekta binafsi au nje waende. Sokoine alidai kuwa serikali ndio imegharamia elimu hivyo cheti ni mali ya serikali.
  • Sokoine alianzisha kampeni ya nguvu kazi ya kukamata mtu yeyote asiye na kazi mjini na kumrudisha kijijini kwa nguvu japo Nyerere alisema akicheka, Edward Watanzania hawa, wana uhuru wa kutembea popote chini. Sokoine akasema kama hawana kazi wasije mijini wakafanye kazi vijijini!
  • Sokoine alikuwa akimwambia Nyerere ana huruma sana, na yeye akiwa raisi ataweka mambo sawa, kitu ambacho kiliwafanya vigogo wengi sana kuogopa sana kitakachowapata Sokoine akiwa raisi baada ya Nyerere
  • Sokoine viongozi waliokuwa karibu na Nyerere walikuwa wanaenda kwa Nyerere kumlalamikia kila wakati, na ndio maana basi, alipokufa, watu wakasema ulikuwa mchoro wa vigogo. Hata wanasema ushirikina au staged accident ilifanyika, na kwamba alivyokufa na gari ilivyogogwa havikuendana kabisa.
NI vizuri kumkumbuka Sokoine kwa mazuri, lakini mara nyingine tuwe wakweli. Sokoine bwana alikuwa extreme kwelikweli, aina ya kiongozi ambae angeweza hata kusema chuo kikuu wavae uniform!. Ila tu, wakati huo wa chama kimoja na Tanzania ya zidumu fikra za mwenyekiti na uzalendo wa kweli, sidhani kama ingekuwa shida sana. Tungekuwa Cuba ya namna fulani.
 
Ukweli ni kwamba mtu ambaye anasema Sokoine angekuwa raisi bora sana, hapaswi kulalamika kuhusu Magufuli. Magufuli ana silka iliyo karibu sana na Sokoine.

Ukweli ni kwamba wote Sokoine na Magufuli hawakufaa kuwa maraisi wa nchi, lakini walifaa sana kuwa mawaziri wakuu. Mtu kama Magufuli angefaa sana kuwa waziri Mkuu chini ya raisi kama Kikwete, kama ambavyo Sokoine alifaa kuwa waziri mkuu chini ya raisi Nyerere. Nyerere mara nyingi sana alikuwa akimdhibiti Sokoine asipite kiasi.
  • Sokoine kuna wakati alitaka kumtia ndani Kawawa kwa mambo ya uhujumu uchumi - Nyerere akamwambia wewe Edward, unataka kuleta mgawanyiko serikalini
  • Sokoine alitaka wahujumu uchumi wafungwe bila kufikishwa mahakamani, Nyerere akasema haiwezekani, lazima tuonekane tunafuata utawala wa sheria
  • Sokoine alitaka ukihitimu elimu kama chuo kikuu usikabidhiwe cheti kwa kuwa umesomeshwa na serikali, Nyerere akasema acha wanaoweza kwenda nje kutafuta fursa zaidi sekta binafsi au nje waende. Sokoine alidai kuwa serikali ndio imegharamia elimu hivyo cheti ni mali ya serikali.
  • Sokoine alianzisha kampeni ya nguvu kazi ya kukamata mtu yeyote asiye na kazi mjini na kumrudisha kijijini kwa nguvu japo Nyerere alisema akicheka, Edward Watanzania hawa, wana uhuru wa kutembea popote chini. Sokoine akasema kama hawana kazi wasije mijini wakafanye kazi vijijini!
  • Sokoine alikuwa akimwambia Nyerere ana huruma sana, na yeye akiwa raisi ataweka mambo sawa, kitu ambacho kiliwafanya vigogo wengi sana kuogopa sana kitakachowapata Sokoine akiwa raisi baada ya Nyerere
  • Sokoine viongozi waliokuwa karibu na Nyerere walikuwa wanaenda kwa Nyerere kumlalamikia kila wakati, na ndio maana basi, alipokufa, watu wakasema ulikuwa mchoro wa vigogo. Hata wanasema ushirikina au staged accident ilifanyika, na kwamba alivyokufa na gari ilivyogogwa havikuendana kabisa.
NI vizuri kumkumbuka Sokoine kwa mazuri, lakini mara nyingine tuwe wakweli. Sokoine bwana alikuwa extreme kwelikweli, aina ya kiongozi ambae angeweza hata kusema chuo kikuu wavae uniform!. Ila tu, wakati huo wa chama kimoja na Tanzania ya zidumu fikra za mwenyekiti na uzalendo wa kweli, sidhani kama ingekuwa shida sana. Tungekuwa Cuba ya namna fulani.
Napingana kidogo na mtazamo wako ndugu kwakuwa nchi ilihitaji maraisi madikteta na wajinga kama magufuli na kama angekuwamo Sokoine. Hao uliowataja Nyerere na Kikwete unatambua walikumbatia wajinga na wala rushwa kwa sababu ya mahusiano kati yao na hivyo nchi kudidimia hadi kufikia hapa. Hata hao kina Nyerere na Kikwete kuna vingi walikosea ikiwamo kuonea watu wengi na wengine hata bila makosa na wengine kutokana na kuwashauri wasivyoviamini.

Nchi ilifika kipindi ya kama ilivyo sasa ilimuhitaji kichaa kama Magufuli kuliko kuwadhibiti.. Ukisema kuwa Magu alifaa kuwa Waziri mkuu bado ingetegemea maamuzi ya Raisi yakama Magu alivyokuwa Waziri wa Ujenzi alikosa support ya Kikwete hasa pale alipogusa friends wa kikwete.

Tulihitaji Raisi kichaa... we got one.. Am happy
 
Napingana kidogo na mtazamo wako ndugu kwakuwa nchi ilihitaji maraisi madikteta na wajinga kama magufuli na kama angekuwamo Sokoine. Hao uliowataja Nyerere na Kikwete unatambua walikumbatia wajinga na wala rushwa kwa sababu ya mahusiano kati yao na hivyo nchi kudidimia hadi kufikia hapa. Hata hao kina Nyerere na Kikwete kuna vingi walikosea ikiwamo kuonea watu wengi na wengine hata bila makosa na wengine kutokana na kuwashauri wasivyoviamini.

Nchi ilifika kipindi ya kama ilivyo sasa ilimuhitaji kichaa kama Magufuli kuliko kuwadhibiti.. Ukisema kuwa Magu alifaa kuwa Waziri mkuu bado ingetegemea maamuzi ya Raisi yakama Magu alivyokuwa Waziri wa Ujenzi alikosa support ya Kikwete hasa pale alipogusa friends wa kikwete.

Tulihitaji Raisi kichaa... we got one.. Am happy
Kimsingi, unasema nilichosema, kwamba Sokoine na Magufuli ni "vichaa". Na mimi nilichosema ni kwamba ukiwa na kiongozi kichaa hapaswi kupewa madaraka ya bila kudhibitiwa, sana sana mtaingia matatizoni. Inabidi kuwe na nguvu ya kumdhibiti, kwa mfano Sokoine kwa Nyerere. Unampa kichaa rungu akatulize watoto darasani kupiga kelele?

Idd Amin alikuwa kichaa. Mengistu Haile Marian alikuwa kichaa. Hitler alikuwa kichaa. Pamoja nia zao nzuri kwa nchi zao, walizifikisha wapi?

Sidhani kama ni jambo jema kwa raisi kichaa kusema bomoa nyumba za Ubungo bila fidia kwa kuwa tulishnda kesi. Lazima iwepo nguvu ya kusema katika ubinadamu wapeni fidia, kwa sababu hawa watu hawana kwa kwenda na walijenga kwa kupewa vibali na serikali yetu hii hii.
 
hakika huyu baba angekuwa rais ingeandikwa historia nzito sana katika taifa letu ila mipango ya Mungu ni mkuu kwa kutupatia Magufuli wa mfano wake

Huyo jamaa ukauzu wake dagaa cha mtoto,waulize wahujumu uchumi wanamuelewa fresh.


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Ubungo bila fidia kwa kuwa tulishnda kesi
Mbona una ruka ruka...kwenye post yako ya msingi...umesema Mwl. Nyerere alimdhibiti Sokoine asifunge wahujumu uchumi bila kupitia mahakamani kwa misingi ya kufuata sheria, mara hii unamlaumu Rais Dr. Magufuli kwa kutekeleza maagizo ya kisheria iliyodhibitishwa na mahakama. Hivi ukiulizwa unajua unachokitaka utakuwa namajibu kweli!?
 
..siyo kweli.

..aliumiza wananchi wasio na hatia ktk zoezi lake la kukamata "wahujumu uchumi."

..matatizo yetu ya uchumi yalisababishwa na uongozi na usimamizi mbaya wa utawala wa wakati ule, na siyo hao waliopewa jina baya la "wahujumu uchumi."

Umeambiwa tu hukuwepo. Basi aliekuambia kuwa aliumiza wananchi muongo. Watu walihodhi kila kitu. Hapo ndio palipozuka neno “mwendo wa kuruka”. Ukitaka bidhaa zililkuwepo lakini mikononi mwa watu wachache waliohodhi na utanunua kwa bei wanaopanga wao. Hao ndio wahujumu uchumi. Usiongelee jambo usilolijua undani wake.
 
Kimsingi, unasema nilichosema, kwamba Sokoine na Magufuli ni "vichaa". Na mimi nilichosema ni kwamba ukiwa na kiongozi kichaa hapaswi kupewa madaraka ya bila kudhibitiwa, sana sana mtaingia matatizoni. Inabidi kuwe na nguvu ya kumdhibiti, kwa mfano Sokoine kwa Nyerere. Unampa kichaa rungu akatulize watoto darasani kupiga kelele?

Idd Amin alikuwa kichaa. Mengistu Haile Marian alikuwa kichaa. Hitler alikuwa kichaa. Pamoja nia zao nzuri kwa nchi zao, walizifikisha wapi?

Sidhani kama ni jambo jema kwa raisi kichaa kusema bomoa nyumba za Ubungo bila fidia kwa kuwa tulishnda kesi. Lazima iwepo nguvu ya kusema katika ubinadamu wapeni fidia, kwa sababu hawa watu hawana kwa kwenda na walijenga kwa kupewa vibali na serikali yetu hii hii.
Ukichaa sio necessary sababu za kushindwa... wako vichaa wamefanya vizuri.....
Kimsingi ni vichaa tu huwa wanafanikisha mambo... most of them are risk takers
Na ni wenye busara tu huwa wanakwamisha vitu... kama walivyo viongozi wa TZ ikiwamo Nyerere na waliofuata
Kwa sasa kichaa Magufuli ndio anahitajika na analeta mapinduzi ya kweli japo ana mapungufu ikiwamo kubana demokrasia
 
Back
Top Bottom