Hayati Dkt. Magufuli aliwatumia wamachinga ili kujizolea umaarufu wa kisiasa, hakuwa na huruma na wamachinga

Kiboko ya Jiwe

JF-Expert Member
Apr 7, 2020
12,684
36,045
Tuliyasema haya wakati akiwa hai na tutayasema wakati huu ambao hatunaye.

Kwanza Wamachinga hawakuzi uchumi wa nchi hii kwa kiwango kikubwa bali wanaukuza uchumi wa China, India na Thailand maana huko ndiko zitokazo bidhaa wanazouza.

Serikali ya Magufuli iliwatumia wanyonge kama mtaji wake mkuu wa kufukia mashimo yake ya kisiasa.

Huwezi mtu kumwacha achafue mji eti kisa mnyonge asibughuziwe.

Aliyejenga Machinga complex nadhani ni Kikwete huyo ndiye unaweza kusema kuwa ana harufu ya huruma kwa wamachinga.

Dar es salaam ina wilaya tano kama sikosei. Kila wilaya ingepata soko la wamachinga lililojengwa kisasa na kugawa vizimba kwa wamachinga hiyo ndio huruma kwa wamachinga.

Kariakoo ingebaki na maduka ya Jumla tu.

Mji ungenoga, wananchi wangerahisishiwa huduma.

Mtu aweke banda lake kwenye mtaro umwache tu kisa mnyonge. No.
 
Screenshot_20210912-120221_Instagram.jpg
 
That's the mere fact! At the beginning, Hitler alipendwa sana Ujerumani kwa sababu hizo hizo za kujifanya yuko upande wa wanyonge kumbe alikuwa na ajenda yake aliyoijua mwenyewe! Kilichokuja kuwapata wajerumani hawatokaa wakisahau. Ogopa sana mbaguzi kwa kigezo chochote kile!
 
... that's the mere fact! At the beginning, Hitler alipendwa sana Ujerumani kwa sababu hizo hizo za kujifanya yuko upande wa wanyonge kumbe alikuwa na ajenda yake aliyoijua mwenyewe! Kilichokuja kuwapata wajerumani hawatokaa wakisahau. Ogopa sana mbaguzi kwa kigezo chochote kile!
Magufuli katuharibia sana nchi yetu
 
Wewe ni poyoyo tu

Wamachinga hata Mzee Mwinyi aliwaacha, Mkapa na Yusuph Makamba akiwa mkuu wa mkoa alishindwa, huyo cha kuzurura ndiyo kabisa hakufanya lolote!

Soko la machimba limejengwa na City council kwa mkopo toka NSSF

Wakati wa JPM machinga wamepata heshima, na aliwaambia wakuu wa Wilaya kabla ya kuwaondoa barabarani tafuta maeneo kwanza ya kuwaweka
 
Hili suala tunavyoliangalia ni kama kuondoa tatizo la magugu kwa kukata majani na sio kuyangoa (kuondoa mizizi)

Hata ukimwaga Machinga Complex kila mtaa in the end zitajaa. Kama taifa hatuwezi kuwa na 90% Machinga hio ingewezekana kama tungekuwa machinga wa dunia nzima yaani tunatembeza bidhaa mpaka huko North na South Pole.

Hatuwezi kuwa taifa la wachuuzi na madalali, mwisho wa siku nani atamuuzia nani ? Kipato chenyewe cha wadau ni cha kuunga unga (no buying power)

Its a Shame kwa nchi tajiri yenye vyanzo vingi ambavyo vingetumika kuwasaidia raia vinasaidia wachache (na kwa mwendo huu wa kufuja hizo mali in the end tutabakia kujuta tu, na kujiuliza what might have been)
 
Hili suala tunavyoliangalia ni kama kuondoa tatizo la magugu kwa kukata majani na sio kuyangoa (kuondoa mizizi)

Hata ukimwaga Machinga Complex kila mtaa in the end zitajaa..., Kama taifa hatuwezi kuwa na 90% Machinga hio ingewezekana kama tungekuwa machinga wa dunia nzima yaani tunatembeza bidhaa mpaka huko North na South Pole... Hatuwezi kuwa taifa la wachuuzi na madalali, mwisho wa siku nani atamuuzia nani ? Kipato chenyewe cha wadau ni cha kuunga unga (no buying power)

Its a Shame kwa nchi tajiri yenye vyanzo vingi ambavyo vingetumika kuwasaidia raia vinasaidia wachache (na kwa mwendo huu wa kufuja hizo mali in the end tutabakia kujuta tu, na kujiuliza what might have been)
... kila mwaka maelfu ya vijana hu-migrate kutoka vijijini kwenda mijini kutafuta maisha na mitaji pekee wanayokuwa nayo sio kingine zaidi ya nguvu zao. Asilimia kubwa ya hawa huishia katika umachinga na kwa kuwa maelfu kwa maelfu ya watoto huzaliwa kila mwaka; bila sera madhubuti tatizo la ukosefu wa ajira na umachinga halitakoma na hali itakuwa mbaya sana siku za usoni.

Swali la msingi; tumefeli wapi? Sera? Sera ya elimu? Sera ya uzazi? Sera ya kilimo? Ni kwanini vijana wasitamani kubaki vijijini kuzalisha? Ni kwanini vijana wasihame mijini kwenda vijijini kuzalisha? Unapopandisha kwa mfano bei ya mbolea kutoka 50,000 hadi 120,000 ndani ya mwaka mmoja huku mazao ya wakulima yakikosa soko tutegemee nini? Kuna mahali sera zimefeli!
 
Usimtaje mtu wala wewe nenda kwenye point tu ya msingi.

Kwa maana huu ni kweli wamachinga wamekuwa wanajazana kila mahali haipendezi ila wataenda wapi na hela ya chap wakikaa walipotengenezewa nani awafuate.

Unakuta mtu kachoka kutoka kazini na hawezi kwenda sokoni kwa hiyo machinga wapo karibu na alipo basi.
 
... kila mwaka maelfu ya vijana hu-migrate kutoka vijijini kwenda mijini kutafuta maisha na mitaji pekee wanayokuwa nayo sio kingine zaidi ya nguvu zao. Asilimia kubwa ya hawa huishia katika umachinga na kwa kuwa maelfu kwa maelfu ya watoto huzaliwa kila mwaka; bila sera madhubuti tatizo la ukosefu wa ajira na umachinga halitakoma na hali itakuwa mbaya sana siku za usoni.

Swali la msingi; tumefeli wapi? Sera? Sera ya elimu? Sera ya uzazi? Sera ya kilimo? Ni kwanini vijana wasitamani kubaki vijijini kuzalisha? Ni kwanini vijana wasihame mijini kwenda vijijini kuzalisha? Unapopandisha kwa mfano bei ya mbolea kutoka 50,000 hadi 120,000 ndani ya mwaka mmoja huku mazao ya wakulima yakikosa soko tutegemee nini? Kuna mahali sera zimefeli!
Sadly sitegemei Serikali au individual kama anaweza kusaidia hili suala; na tatizo hili ukiangalia kwa mbali ni global issue (tatizo la ajira) with automation, technology na machinery nguvu kazi haiitajiki tena kama zamani kwahio watu wasio na kazi wataongezeka na matabaka yatazidi kuwa makubwa siku baada ya siku na yataleta chuki kwa walionacho na wasionacho na mwishowe tutapigana bakora.

Lakini binafi naamini wa kuwasaidia hao machinga na masikini wengine ni wao wenyewe kwa kuchukua initiative na kufanya vitu sustainable, kwanini wahangaike kukimbizana mijini kwenye nchi kubwa na tajiri kama hii? Kwenda vijijini kulima pekee haisaidii kama hata waliopo kijijini sasa hivi wanalia mahindi yao hayana wateja, na kwanini mkulima akose wateja wakati kuna watu mjini wanakufa njaa ? Hapo utaona we need to get back to basics, something is fundamentally wrong somewhere and its solution is not a quick fix.

Anyway ngoja nikuache na hii work on progress ya mdau mmoja uburudike (though its idealistic and utopian might be the way forward

 
Tuliyasema haya wakati akiwa hai na tutayasema wakati huu ambao hatunaye.

Kwanza Wamachinga hawakuzi uchumi wa nchi hii kwa kiwango kikubwa bali wanaukuza uchumi wa China, India na Thailand maana huko ndiko zitokazo bidhaa wanazouza.

Serikali ya Magufuli iliwatumia wanyonge kama mtaji wake mkuu wa kufukia mashimo yake ya kisiasa.

Huwezi mtu kumwacha achafue mji eti kisa mnyonge asibughuziwe.

Aliyejenga Machinga complex nadhani ni Kikwete huyo ndiye unaweza kusema kuwa ana harufu ya huruma kwa wamachinga.

Dar es salaam ina wilaya tano kama sikosei. Kila wilaya ingepata soko la wamachinga lililojengwa kisasa na kugawa vizimba kwa wamachinga hiyo ndio huruma kwa wamachinga.

Kariakoo ingebaki na maduka ya Jumla tu.

Mji ungenoga, wananchi wangerahisishiwa huduma.

Mtu aweke banda lake kwenye mtaro umwache tu kisa mnyonge. No.
Nduli hakuwa na utu hata kidogo. Uganda nzima hatukumpenda, ila kwao alipendwa sana
 
Pia alifanya ni kichaka cha kuficha maovu yake hasa roho mbaya na ukatili wake wa kuzaliwa nao kwa kujifanya ni mtu wa watu na mwenye huruma lakini kiuhalisia alikuwa ni mtu mwenye roho mbaya.
 
Kimsingi hawaa machinga ndio nguvu kazi ya viwandani. Endapo viwanda vitashika kasi hawa vijana wote hawataonekana humo barabarani.
 
Back
Top Bottom