Sasa hapo ndg yangu linaboreka au linakufa? Imefikia hadi viongozi wa serikali hawalitumii kabisa kwasababu wanajua halina watazamaji, wanaenda clouds au TV nyinginePamoja na watu wengi kumsifia Tido Mhando akiwa TBC ni kweli alifanya mkubwa kwa utashi wake lakini kumbuka TBC ina msingi yake ktk uendeshaji wake kama taasisi ya umma.
Dr Rioba ni mzuri lakini kwa TBC ataendesha kwa kufuata msingi ya TBC na si nje ya hapo.
TBC iko makini na kazi zake na INA vyombo vya kisasa na vya gharama sana na kamwe haitafanya Fanya kazi kwa kufuata matakwa ya MTU Bali taratibu za taasisi.
Mkurugenzi Dr Rioba amepewa dhamana na Rais na anajua anachokifanya ili kuboresha shirika na maslahi ya watumishi tumwache afanye kazi.