Haya sio Mapenzi bali Uroda

Black BackUp

JF-Expert Member
Aug 5, 2019
683
618
Ebwana eheee nimeoa miaka Saba iliyopita lakini cha kushangaza sasa kila siku unaambiwa mapenzi yazidi kuongezeka na sasa si mapenzi tena Mwanaume mwenzenu napata uroda.

Asubui nikiamka nakuta maji bafuni zamani maji ya kuoga alikua anayaunga na karafuu Ila sasaivi ameongeza anaweka majani ya mdarasini na mchaichai, katika mapishi ndo usigusee kabisaa Kila siku nakula radha mpyaa katika chakula binzari haikosii.

Kitandani Kila siku twalalia shuka jeupee na kabla sijalala nafanyiwa masaji ya buree na mafuta ya tende. Kila siku napewa mtindo mpyaaa Sio ya mbuzi kagoma tu, Kuna ile popo kanyea mbingu bhana,nikilala hoiii unaambiwa Kama mbeba viroba kariakoo shimoni.

Jamani kuoa raha nyiee.
 
Kama na mambo mengine yanaenda sawa, basi fresh.Yani madogo wako na wazee kama unawazingatia basi vizuri. Mwaka wa saba halafu uje kuandika hivi, kuna kitu kidogo kinatupa wasi wasi.

Uko sawa kwelikweli mkuu, hebu tupigie simu home kwanza utuulize tunakuchukuliaje...
 
14 Reactions
Reply
Back
Top Bottom