AlP0L0
JF-Expert Member
- Apr 23, 2011
- 6,053
- 4,279
Jambo hili halihitaji IMF wala ADB waje watuambie, kama mwaka wa nne sasa mishahara inashindikana kuongezwa, maana yake uchumi uko ICU.Mpaka sasa inaonekana kunahujuma ilipangwa na IMF kuihujumu Tanzania dhidi ya takwimu za kiuchumi,
Naipongeza serikali kwa kushitukia mchezo huo mchafu,kwa kutoichapisha ripoti hiyo,IMF walitaka tujikaange kwa mafuta yetu wenyewe.
Hili limethibishwa leo ikulu na kiongozi mwandamizi kabisa wa bank ya ADB ,amesema uchumi wetu unakua vizuri na unatarajiwa kukua vizuri kwa asilimia 6 mpaka 7.
Nzuri zaidi ni mwafrika mwenzetu.
Nategemea Zitto ajitokeze na kundi lake kumpinga kiongozi huyu mbobezi wa masuala ya kiuchumi .
Mwisho, ni nani wako nyuma ya hujuma hii dhidi ya nchi yetu?,na nini lengo lao?