Haya sasa, nani mkweli na nani anaihujumu Tanzania kati ya ADB na IMF?

Mpaka sasa inaonekana kunahujuma ilipangwa na IMF kuihujumu Tanzania dhidi ya takwimu za kiuchumi,

Naipongeza serikali kwa kushitukia mchezo huo mchafu,kwa kutoichapisha ripoti hiyo,IMF walitaka tujikaange kwa mafuta yetu wenyewe.

Hili limethibishwa leo ikulu na kiongozi mwandamizi kabisa wa bank ya ADB ,amesema uchumi wetu unakua vizuri na unatarajiwa kukua vizuri kwa asilimia 6 mpaka 7.

Nzuri zaidi ni mwafrika mwenzetu.

Nategemea Zitto ajitokeze na kundi lake kumpinga kiongozi huyu mbobezi wa masuala ya kiuchumi .

Mwisho, ni nani wako nyuma ya hujuma hii dhidi ya nchi yetu?,na nini lengo lao?
Aisee
Huku
1. Mafuta ya taa gali
2. Sukari juu
3.hakuna ajira
4. Hakuna nyongeza
5. Kila kitu juu mzee baba sujui hiyo 7 ni huo ujenzi Wa 4ways au ni hizo ndege kabda
 
Hiu
Mkuu nenda kwenye jumba la makumbusho pale London utaikuta. Hiyo yako ndiyo ya kuedit jaribu pia kumsearch huyo aliyekotiwa utajua alitembelea wapi mwaka 1835 mkuu.
Huyu jamaa hata Afrika hajawahi kufika.., kuna jamaa ka reply kuwa huyu lord hajawahi ku adress British Parliament 1835..

Sasa which is which, nani wa kumwamini..??
 

Btw; ni BET hiyo hiyo iliyokuwa funded na WB. And remember ni nani alietoa hilo tangazo kuwa "AfDB imeahidi/imekubali kutoa fedha za mradi...."? Msigwa, si ndio? Na ni the same guy alietutangazia kuwa WB wame-release USD 300m ya elimu (japo Magufuli alituambia hadharani mbele ya mwakilishi wa WB kuwa "asante sana kwa kuendelea kutufadhili japo kuna watu walisema hamtatupa"), right? Same Msigwa alietutangazia a few days later kupata fedha kutoka China (na Magufuli akasema "bora nyie hamtoi masharti...."), right?

Je, lipi kati ya hilo limeshatimizwa? Najua kuna uwezekano mkubwa tu wa kupata hizo fedha (maana makubaliano yake ni ya muda mrefu) ila LAZIMA MASHARTI YAO YATIMIZWE. Na aje hapa mtu yeyote yule aniambie kuwa tangu Magufuli aingie madarakani kuna ujumbe toka nchi yeyote umekuja kujadili miradi mipya. Please, do come.
 
Huyu Dr. Adesina hawezi kamwe kutoa kauli za kuwaudhi marais wa Afrika. Maana kuteuliwa kupata cheo chake kama Rais wa AfDB lazima marais wa Afrika waafiki hivyo akitoa kauli za kuwakwaza hawezi kuendelea kuwepo kazini.

23 Nov 2018
Known as Mr Development, Akinwumi Adesina is the president of the African Development Bank Group.
Exclusive interview of Forbes Africa My Worst Day with Peace Hyde.

Source : CNBCAfrica
 
Hiu

Huyu jamaa hata Afrika hajawahi kufika.., kuna jamaa ka reply kuwa huyu lord hajawahi ku adress British Parliament 1835..

Sasa which is which, nani wa kumwamini..??

Simple pal; usimuamini mtu bila kujiridhisha. Ccm ya Nyerere na Mwinyi na kidogo Mkapa waliweza kutuburuza maana kupata reference ilikuwa shida. People of a certain age watakumbuka concept ya "special reserve" kwenye maktaba ambako ilikuwa ni discretion ya librarian kukupa kitabu au la. Nilikuwa na hamu ya kusoma Jerusalem Bible (baada ya kuiona mara ya kwanza - and it is quite an expensive book even now), lakini mheshimiwa yule alininyima.

Leo hii unahitaji bundle tu na ku-google and presto! The fact is there.

Mnakumbuka dogo mmoja aliepost habari ya bricks game gadgets majuzi?
 
IMF inaweza kuhujumu nchi maskini kama hii Tanzania?
IMF ilifikia data yake kwa kushirikiana na wataalamu wetu lamina Serikali ikagona kuchapisha labda wakuu hawakupenda. Walirudi tena na kufika Ikulu baada ya majAdiliano waliahida kupitia upya. Makamu wa Rais wa WB na Rais wa AfDB walafika Ikulu kusalimia wakasema waliosema vinginevyo wasingetoka salama wasiojulikana wakiangalia.
 
Sasa hiyo taarifa ya ADB inatofauti gani na taarifa ingetolewa na polepole? Hujui kama ndege wanaofanana huruka pamoja!
Well, kujifariji kuwa uchumi unakua kwa 7% na zaidi ambayo zaidi haieleweki sijui ni points au 8% ni jambo LA muhimu otherwise unaweza kufa kwa kumeza piriton 1 tu! Wakati mwingine heri kuongopewa kuliko kuambiwa ukweli! Kuishi kwa matumaini kuna ni jambo jema sana kwa watanzania!
 
Mpaka sasa inaonekana kunahujuma ilipangwa na IMF kuihujumu Tanzania dhidi ya takwimu za kiuchumi,

Naipongeza serikali kwa kushitukia mchezo huo mchafu,kwa kutoichapisha ripoti hiyo,IMF walitaka tujikaange kwa mafuta yetu wenyewe.

Hili limethibishwa leo ikulu na kiongozi mwandamizi kabisa wa bank ya ADB ,amesema uchumi wetu unakua vizuri na unatarajiwa kukua vizuri kwa asilimia 6 mpaka 7.

Nzuri zaidi ni mwafrika mwenzetu.

Nategemea Zitto ajitokeze na kundi lake kumpinga kiongozi huyu mbobezi wa masuala ya kiuchumi .

Mwisho, ni nani wako nyuma ya hujuma hii dhidi ya nchi yetu?,na nini lengo lao?
You must be stupid kuamini kuwa uchumi unakua wakati wafanyabiashsra wanarudisha leseni kwa ukosefu wa biashara.

Hata mimi takwimu za IMF sizipendi.
 
You must be stupid kuamini kuwa uchumi unakua wakati wafanyabiashsra wanarudisha leseni kwa ukosefu wa biashara.

Hata mimi takwimu za IMF sizipendi.
Kurudisha lesen kunaambatana nansababu nyinyi

Unafanya biashara au umesoma kwa magezeti kuhusu kufanya biashara

Mfanya biashara wa kweli hubadilika na mazingira akitumia ubinifu kumuimarisha sokoni
 
17 Reactions
Reply
Back
Top Bottom