Haya ndiyo makundi ya watanzania ambao ambao hawataipigia kura CCM mwaka 2020

Tofauti ya wajima wa CCM na mwenendo wa kileo wa CHADEMA hupimwa kwa aina ya lugha wanazotumia,kwa mwenendu huu mtaendelea kushangaa matokeo ya vijijini kwa wasioathirika na bangi wala wavaa miregezo wa kimarekani tunaodhani kuwaiga ni usasa.

Hoja hujibiwa kwa hoja ukiona jibu lako ni mlipuko wa matusi maana yake huna jibu,ni bora kunyamaza.
=mwenendo
=milegezo
Kajifunze kuandika kisha ndio uje.
Halafu hivi utawezaje kumwambia mtu anyamaze angali katiba ina mruhusu kuwa na uhuru wa kutoa maoni yake?
Wewe hapa umekuja na hoja gani?
Naona pia Ulimwengu amekuingia kichwani maana neno "milipuko" limekukolea, unalipuka kama ilivyo kwa jeuri ya pombe mataputapu (j.p.m)
 
Watanzania tulio wengi tunamuelewa sana JPM..kila kitu kina gharama yake....funga mkanda, kaza na kamba..kurudisha nidham kutoka pale tulipofikia sio mchezo
Tumia nafsi ya umoja kujielezea wewe na usiseme "watanzania tulio wengi tunamuelewa" kwani wewe ni msemaji wa hao watanzania?
 
Tanzania ina majinga mengi dom.,sing,shiny,mwan, simi,Moro,tab yakilambishwa sukari miezi mitatu pamoja na ubabe wa mtukufu wa kuilazimisha tume ya uchaguzi.
 
Ukisema wanafunzi wa vyuo vikuu vyote kuwa makini, kuna shirikisho la vyuo vikuu ccm na tawi kila chuo
 
Kinacho nisikitisha kunawanaichi ambao ambao pamoja na yote hayo bado wanaikubali NYINYIEM
 
01: watumishi wa umma wote ,sababu mpaka sasa hawajapandishwa madaraja ,vyeo na mishahara wananyanyasika kazini bila hatia wanateseka uhakiki wa kila siku ambayo unawapa gharama kila kukicha.

02: wanafunzi wote wa vyuo vikuuu ,maana wamekoswa mikopo hivyo wengi wao kubaki nyumbani bila kazi yeyote ile hivyo hawatamani tena kuichagua ccm.

03: vijana 3000 walioajiriwa mwezi June 2016 na kusimamishwa kazi huku wamepewa mikataba ya kazi na kuanza kufanya kazi mfano walioajiriwa mahakamani ,mikoani nk mpaka sasa imepita miezi sita hawajui hatima yao kabisa hivyo ni jambo gumu kuwapigia ccm kura.

04: wahanga wa watetemeko la ardhi kagera .

05 : wamachinga wote wa kwenye majiji makubwa mfano Mwanza nk .

06: wakulima wanalia njaa lakini serikali haitoi hata misaada ya chakula .

07: wahitimu wa vyuo mbalimbali kwa sababu wamekoswa ajira kutokana na serikali kutoajiri na kusimamisha ajira mpaka sasa hakuna idara yeyote iliyeyote iliyotangaza ajira serikalini toka zisimamishwa zaidi ya kutoa matamko.

08: wahitimu wa ualimu kwa masomo ya Sanaa na walimu waliohitimu kwa ajili ya shule za msingi kubaguliwa kwenye ajira kutoajiriwa serikalini .

09: wananchi waliobomolewa nyumba zao na tanroad bila taarifa yeyote.

10: waandishi wa habari wote kutokana na kunyimwa Uhuru wa kuandika habari kwa ukombozi wa taifa letu.

11: wafanyabishara wote kutoka na kodi kupanda kiholela na mzunguko wa hela kuwa mgumu mtaani .

12: watumishi wa umma waliotumbuliwa wote hawatakuwa tayari kuwapigia ccm kura tena .

Ukweli uchaguzi wa 2020 ni mgumu zaidi ya ule wa mwaka juzi utakuwa mgumu kuliko chaguzi zote toka tupate Uhuru.
serikali imejitengenezea upinzani ndani ya chama chake yenyewe baba nanihii itabidi aanze kumnoa darasa mapeema ili akanengue ,jukwaani 2020 kutoboa kwakwe itakuwa ngumu kama ngamia kuingia kwenye tundu la sindano
 
Serikali yetu waga inajisafisha kipindi cha uchaguzi hivyo kuwaaminisha wananchi wake kuwa itafanya mabadiliko. Shida ya binadamu tunasahau yale tuliyo tendewa ndani ya miaka 5 na kuaminishwa kwenye kipindi cha kampeni kuwa we have hope.
na shigongo kanyimwa tenda ya tsht za 95000 hehehee wapinzani ni wengi kuliko pombe anavyodhani
 
Back
Top Bottom