Haya ndiyo Makosa 11 anayotuhumiwa Zitto Kabwe na chama chake cha CHADEMA...

hahahaahaha...kwa speech ya lisu tayari zitto anahujumiwa...eti hatutaki kuweka tuhuma wazi ila si alizozisema zitto na dk.mkumbo...eti ukiwa na nia ya kugombea unaandka barua kwa katibu mkuu hivi kweli kuna kitu kama hicho dunia ipi..et ohh zito ajawahi kuhoji pesa za sabodo na ruzuku kwenye vikao vya chama..sasa atahoji ili nani atekeleze? Mbowe au mkwe wake au vibaraka wa mbowe? Na watueleze ni kwa nini zitto alijitoa kuwa signatory kama si ufisadi wa mbowe na kufanya chama mali yake ikiwemo kukiuzia chama magari chakavu..kukikopesha chama ruzuku kama pesa yake..etc chadema ni saccos ya mbowe na mtei full stop vbaraka wengne wa mbowe njaa zinawasumbua mwsho umefka go zito go zito toa uozo chadema si mama yako wala baba yako..mvuto wa zitto kisiasa na uwezo wake wa kujenga hoja ndio umeifksha chadema pale ilipo toka enzi za buzwagi saga adi leo...chadema masalia wanaoshinda ufipa ni waganga njaa ndio maana mbowe anawawin kirahisi...mbowe si mwanasiasa ni bussines man na silaha anatafta pensheni kwa hili mnyka na umeonyesha udhaifu sana kwa sababu silaha tunajua alishakuwa mtumwa wa mbowe na mtei wewe nawe umeingia uko mnyka kuwa saccos member?
Umendika mengi lakin sijaona kama uko informed. Pia ni kosa kumispell Jina la mtu!
 
Mungi Mkuu nikiunganisha vifungu 2,3,4 kuweka wazi ni kushirikiana na CCM kuihujumu
CHADEMA, pamoja na kugawa pesa kujenga uchochezi kudhoofisha chama!! Hizo mbinu za kuwashambulia viongozi wa juu
tukiwa kwenye mapambano ni kudhoofisha chama!!
Piga chini wasaliti tusonge mbele na Ukombozi wa wanyonge!!
 
Last edited by a moderator:
Kufanya maamuzi magumu ndiyo kitu kinachokosekana serikalini na kuharibu nchi.Kwa hili naipongeza cdm wanaweza kutawala na kutomfumbia macho yeyote yule akivurunda.
 
@ Chamviga hiyo project Wasira ikiasisiwa Ikulu imefeli! Hivi hujiulizi zile namba za kutuma fedha kwa M-Pesa kwa mamluki kama sio za ZZK???
CDM wana akili huyu jamaa anatapatapa amekwisha!!
 
hahahaahaha...kwa speech ya lisu tayari zitto anahujumiwa...eti hatutaki kuweka tuhuma wazi ila si alizozisema zitto na dk.mkumbo...eti ukiwa na nia ya kugombea unaandka barua kwa katibu mkuu hivi kweli kuna kitu kama hicho dunia ipi..et ohh zito ajawahi kuhoji pesa za sabodo na ruzuku kwenye vikao vya chama..sasa atahoji ili nani atekeleze? Mbowe au mkwe wake au vibaraka wa mbowe? Na watueleze ni kwa nini zitto alijitoa kuwa signatory kama si ufisadi wa mbowe na kufanya chama mali yake ikiwemo kukiuzia chama magari chakavu..kukikopesha chama ruzuku kama pesa yake..etc chadema ni saccos ya mbowe na mtei full stop vbaraka wengne wa mbowe njaa zinawasumbua mwsho umefka go zito go zito toa uozo chadema si mama yako wala baba yako..mvuto wa zitto kisiasa na uwezo wake wa kujenga hoja ndio umeifksha chadema pale ilipo toka enzi za buzwagi saga adi leo...chadema masalia wanaoshinda ufipa ni waganga njaa ndio maana mbowe anawawin kirahisi...mbowe si mwanasiasa ni bussines man na silaha anatafta pensheni kwa hili mnyka na umeonyesha udhaifu sana kwa sababu silaha tunajua alishakuwa mtumwa wa mbowe na mtei wewe nawe umeingia uko mnyka kuwa saccos member?


kama zitto ni bora kwa nini msimchukue ninyi kwenye chama chenu, mtuachie sisi na saccos yetu ili 2015 watanzania waamue kati ya saccos au mafisadi/wanafiki/wezi
 
Afrika nzima na hasa huku Tanzania njaa, choyo na ubinafsi utatuponza sana ni nadra sana kupata viongozi wakawa na msimamo mmoja ili kuzikwamua jamii zetu na umaskini uliokithiri.,
 

Katika kosa la tatu, wanadaiwa kutoa tuhuma juu ya viongozi wenzao bila kupitia vikao halali na utaratibu wa ngazi zilizowekwa, kinyume na kanuni ya 10.1 (X).

mimi kidogo ninashida na eneo hili, hivi muheshimiwa LEMA alivyotoa tuhuma hapa JF dhidi ya ZZK ilikuwa kwenye kikao? na hatua zipi amechukuliwa juu ya hilo? na hapa ndipo tunapotoa nafasi ya lugha za "ubaguzi", "vibaraka wa Mbowe" na mengi mengineyo, kuna wakati tunapaswa kuwa critical na tuweke mapenzi kando.
 
Hata wakiwafukuza sawa almuradi siye Watanzania tumeshajua uozo wa ufisadi unaofanywa Chadema ngazi ya taifa inatosha.JISAFISHENI KWA KUTENDA MEMA.
 
Mungi Mkuu nikiunganisha vifungu 2,3,4 kuweka wazi ni kushirikiana na CCM kuihujumu
CHADEMA, pamoja na kugawa pesa kujenga uchochezi kudhoofisha chama!! Hizo mbinu za kuwashambulia viongozi wa juu
tukiwa kwenye mapambano ni kudhoofisha chama!!
Piga chini wasaliti tusonge mbele na Ukombozi wa wanyonge!!

Salama ya CHADEMA ni kumfukuza Zitto Kabwe
Salama ya CCM ni kumchagua Zitto Kabwe awe Mwenyekiti wa Taifa
 
sipati picha ndugu mbowe angekuwa ndio mheshimiwa rais wa jamhuri ya muungano.kwa majina ya kejeli anayopewa kikwete,nadhani nusu ya CCM ingekuwa imefukuzwa chama.

hapa chadema wakubali wamechanganya mambo.hata ZITTO na KITILA wangemponda vipi mwenyekiti,hizi sio firm grounds za dismissal.sasa kama ZITTO anaona mwenyekiti ana elimu ndogo asemeje?aseme mwenyekiti ni PhD holder?hapa chadema wanajaribu kujenga chama cha ndio mzee all the way.

sikubaliani na ukosaji ustaarabu wa zitto na mwenzie kama wamewaita hivyo,lakini kuna sababu ya msingi kwa nini wameufanya waraka ule uwe siri,sidhani kila mmoja wetu hapa angeambiwa aweke hadharani jinsi anavyomfikiria kikwete mbele yake kuna ambaye angeikosa jela kwa kosa la kumdhalilisha mkuu wa nchi.

MBOWE hakutakiwa kupekenyua kufahamu zitto anamchukuliaje,yeye kama kiongozi alitakiwa alifahamu hilo mapema.kuhusu-ku-conspire kuweza kum-replace mbowe kuwa mwenyekiti,hapa naona chadema wamehamaki.kwani kilichokuwa kinafanywa na ZITTO na wenzie ni power consolidation.

kwa siasa zetu za kibongo hii bado sana,lakini sidhani kama inastahili kufukuzana uongozi.yeye mbowe alitakiwa afahamu natural ascendance ya katibu mkuu msaidizi ni aidha katibu mkuu kamili,makamu mwenyekiti au mwenyekiti
sasa kama alikuwa anadhania ZITTO anampango wakutoka katibu mkuu msaidizi kwenda kuwa mjumbe wa shina la chadema,basi si vibaya akikubali kuitwa akili ndogo
acheni kujitoa ufahamu kwa makusudi, hivi unataka kusema kama akina Nape na Mwigulu wakipanga mapinduzi ya kumng‘oa Kikwete kwenye uenyekiti kwa madai kwamba ana akili ndogo waataachwa waendelee kuwa viongozi wa Ccm kwa kuwa kikwete ni mvumilivu? msitulishe ujinga, nampenda sana Zitto na nisingependa afukuzwa Chadema lakini ni ukweli kwamba Zitto ni mwiba kwenye miguu ya Chadema anapaswa abadilike sana kama anataka kukubalika na wanamageuzi wenzake
 
Na furahishwa sana na siasa za hawa watu, kwani ukisema kiongozi wa chama chetu ni mzito, na akili ndogo sioni kama hapo akisema ana kipenda chama ni kosa kwa kuwa yeye ana penda chama ila hafurahishi na mtawala kwenye chama anaona hana sifa za kuongoza, hilo haliondoi mapenzi yake kwenye chama hebu tusiwe tuna sifia hoja mfu kwa madai kuwa fulani amesema, hata Lisu na yeye uchambuzi wake mara nyininge huwa haupo sawa .

Unaweza sema nchi yangu ni masikini sana tena umasikini wake ni wa kutisha na sifurahishwi nao ila naipenda nchi yangu huwezi kuwa umefanya kosa kwa kuwa ulicho kisema ndio sahihi, kwahiyo ni kweli mwenyekiti wa chama si msomi, pia hawezi kujieleza vizuri na ni mzito kufanya maamuzi then kwanini mfiche jambo hili wakati ndio ukweli halisi.
kama kiongozi hata kama nikweli kiongozi mwenzako Ana madhaifu sio busara, sio hekima, sio uungwa na si UTARATIBU sahihi kuandika hekaya za hovyo zenye kupanda chuki na utovu wa nidhamu kwa uongozi na matabaka flani flani ndani ya chombo au jamii husika. Mh. Zitto na wenzake hapa WALIKOSEA! Na hakuna mjadala kuhusu hilo. Hapa wange fuata taratibu zote walizo pewa na CC, ilikufunga mjadala huu,. Kwa Mh. Zitto mtu wa kazi aliyo ifanyia Tanzania na Chadema hii ni AIBU!!!!
Usitetee hii kabisa hii haifai., wala haiwezi kukubalika!
 
Naona kama kuna jambo limejificha ktk hiki chama,ukiangalia kwa makini makosa hayo utaona jinsi yanavyo onyesha kuwa kuna jambo limejificha.
Bado Tnzania kuna safari ndefu sana na kamwe hatuwezi kufikia malengo ya kupata ukombozi wa 2 tunaoufikilia,
safari ni ndefu watanzania na bado hakuna GARI la kutufikisha huko tunako kutaka.hili nina imani nalo na sina shaka nalo kuwa Tanzania bado tunahitaji GARI lenye uwezo wa kutufikisha pale tunako taka kufika.
Tanzania wabunge wake ndio wanaopokea pesa nyingi ukilinganisha na maisha ya watu wake-hakuna chama chenye kupigania hili
Tanzania watu wake wanaishi chini ya dola moja-lakini viongozi vya vyama mbali mbali na wabunge wanapokea mabilioni ya pesa-bado hakuna chama kinachopigania haya.
Tanzania bado wakulima wanategemea mvua na bado wanategemea sana kilimo cha jembe la mkono-hakuna chama chenye kupigania hili na tukumbuke 80% ya watanzania wanategemea kilimo.


Hii nchi bado inahitaji Gari la kutufikisha tupatakapo.
 
Zitto anaonekana ''kuonewa'' na CDM.CCM wameona ivo,na wamekubali utendaji kazi wake,ndani na nje ya chama.Sasa ninaona kwa kuwa CCM ni werevu na wanyenyekevu ni bora Zitto akaenda huko
 
Ndiyo tatizo la watanzania mtu anaelimu ndogo anataka kuitwa anaelimu kubwa mambo gani haya.

......Pazuri hapoooo, kumbe umeliona hilooooo.

Eti anataka kuwa RAIS WA TANZANIA!!!!!!!!!

Tutapomsema anaelimu ndogo TUTAFUNGWA. Ondoeni balaaa hili....
 
Nimegundua ni vigumu kwa Zitto na Kitilla kusalimika baada ya kusoma kauli hii iliyotolewa na Lissu kwa waandishi jana.

Habarileo limemnukuu Lissu kama ifuatavyo:

"Waraka huu umetoa matusi mazito dhidi ya Mwenyekiti wetu,ikiwamo kuitwa kuwa ana elimu ya chini na ana akili ndogo na nzito,halafu mtu huyo huyo alietoa matusi hayo dhidi ya kiongozi wake wa chama anadai eti anakiheshimu chama,kwa hili tumewashitukia,"alisema.

Ndugu mwana JF kama kweli hii ndio kauli kwenye waraka huo kuna kusalimika hapa?

Ni vigumu kwa Zitto na Kitila kusalimika kuliko ilivyo vigumu kwa Ngamia kupenya kwenye tundu la sindano.

kwa upande wa kitila sijui, lakini kwa zitto mbona rahisi sana? Zitto amekataa kuhusika na waraka kwa namna yoyote ile, kitila na mwenzie waliouandika wamekanusha zitto kuhusika, na CC haina ushahidi wowote wa kudhibitisha uhusika wa zitto katika waraka.
 
Back
Top Bottom