Haya ndiyo maisha halisi ya takriban 70%; bado tunapigana na ujinga, maradhi na umasikini

Sky Eclat

JF-Expert Member
Oct 17, 2012
57,597
215,270
1640182738632.png

Haya ndiyo maisha ya takriban 70% ya Watanzania. Bado tunapigana na maadaui tuliowarithi kwa Wakoloni miaka 60 imiyopita Ujinga, maradhi na umasikini.

Mtoto anaezaliwa katika nyumba hii anategemewa akue salama, fikiria changamoto za kudhibiti mbu katika nyumba hii na uepukane na malaria.. Wakazi wa nyumba hii wanahitaji maji safi na salama ya kunywa.

Ukifanya utafiti ya wenye ajira za kudumu katika eneo hili atakua ni Mtendaji wa mtaa, na watu kama watano ofisini. Hakuna mradi ulioanzishwa karibu na hapa unaotoa ajira kwa vijana.

Hili si Tatizo la Tanzania tu, nchi nyingi za Afrika zimeshindwa kuzalisha ajira baada ya uhuru, matokeo yake vijana wengi wanapeleka nguvu kazi katika nchi zenye uchumi imara angalau waweze kuwa tumia wazazi wao mkate. Nguvu hizi zingetumika vyema Afrika zingeketa maendeleo kwetu.

Tusichekane tuangalie jinsi tunavyoweza kujinasua katika mtego huu.
 
Hatari sanaa, hapo kwenye elimu tunajitahidi kidogo, afya tunazidi kupiga hatua labda tutafika muda si mrefu, lakini kwenye hili suala la umasikini aseeeh! bado sana.

Umasikini ni mkubwa sana na unanuka, yaani sio wa kuukumbatia kabisa.

NB: kitu muhimu kabisa cha kufahamu, kama ilivyo minyororo ya thamani katika kilimo, pia kuna minyororo ya umasikini.
 
Hatari sanaa, hapo kwenye elimu tunajitahidi kidogo, afya tunazidi kupiga hatua labda tutafika muda si mrefu, lakini kwenye hili suala la umasikini aseeeh! bado sana.

Umasikini ni mkubwa sana na unanuka, yaani sio wa kuukumbatia kabisa.

NB: kitu muhimu kabisa cha kufahamu, kama ilivyo minyororo ya thamani katika kilimo, pia kuna minyororo ya umasikini.
Huu ukulima wa Jembe la mkono ni vigumu kututoa kiuchumi. Una Lima mazao Tanga tu hapo lakini huna uhakika wa soko.
 
View attachment 2053624
Haya ndiyo maisha ya takriban 70% ya Watanzania. Bado tunapigana na maadaui tuliowarithi kwa Wakoloni miaka 60 imiyopita Ujinga, maradhi na umasikini.

Mtoto anaezaliwa katika nyumba hii anategemewa akue salama, fikiria changamoto za kudhibiti mbu katika nyumba hii na uepukane na malaria.. Wakazi wa nyumba hii wanahitaji maji safi na salama ya kunywa.

Ukifanya utafiti ya wenye ajira za kudumu katika eneo hili atakua ni Mtendaji wa mtaa, na watu kama watano ofisini. Hakuna mradi ulioanzishwa karibu na hapa unaotoa ajira kwa vijana.

Hili si Tatizo la Tanzania tu, nchi nyingi za Afrika zimeshindwa kuzalisha ajira baada ya uhuru, matokeo yake vijana wengi wanapeleka nguvu kazi katika nchi zenye uchumi imara angalau waweze kuwa tumia wazazi wao mkate. Nguvu hizi zingetumika vyema Afrika zingeketa maendeleo kwetu.

Tusichekane tuangalie jinsi tunavyoweza kujinasua katika mtego huu.
Na hapo mti mjinga atasema hapo serikali inahusika , hii nafikiri ni DNA ya Africans wengi hawana akili za kuendelea, wanapata hela lakini hawafikirii kujiendeleza wao ni kuoa na kuzaa na kustarehe, mtu hafikirii kuboresha anapoishi kiwa miundo mbinu imara, safi, iliyopangwa vizuri!
Fikiria nyumba zinavyojengwa 'skwata' mru anavyojenga nyumba au anapoishi ndivyo alivyo pia kichwani...wanawaza uchawi, wivu, kulogana, kusengenyana, kutopendana, vijembe, lugha chafu nk...
Lakini bii bongo kuna maisha mazuri kweli pamoja na mjengo ulivyo, wanajitahidi kuvaa kulingana na udongo wenyewe, mtu avae suti kwenye dongo la vumbi si utachekesha....au mtu avae dela kwenye maeneo ya ofisi za serikali...
 
Hatari sanaa, hapo kwenye elimu tunajitahidi kidogo, afya tunazidi kupiga hatua labda tutafika muda si mrefu, lakini kwenye hili suala la umasikini aseeeh! bado sana.

Umasikini ni mkubwa sana na unanuka, yaani sio wa kuukumbatia kabisa.

NB: kitu muhimu kabisa cha kufahamu, kama ilivyo minyororo ya thamani katika kilimo, pia kuna minyororo ya umasikini.
Mkuu hebu tafakari vizuri!!! Kwenye kilimo kuna minyororo ya umasikini!!!
una maana gani mkuu, naona kama una jeuri fulani kwamba hulimi,, bila shaka unasubili kulimiwa ili ule kwa sababu una fursa ya pesa...
Siku wakulima wakiacha kilimo cha biashara na kujilimia vyakula tu; mlioko mjini mtakula hayo matofali ya nyumba zenu
 
Mkuu hebu tafakari vizuri!!! Kwenye kilimo kuna minyororo ya umasikini!!!
una maana gani mkuu, naona kama una jeuri fulani kwamba hulimi,, bila shaka unasubili kulimiwa ili ule kwa sababu una fursa ya pesa...
Siku wakulima wakiacha kilimo cha biashara na kujilimia vyakula tu; mlioko mjini mtakula hayo matofali ya nyumba zenu
Mkuu, hebu soma tena taratibu maana hujaelewa nilichoandika.

Na pia baada ya kuelewa nakuambia tu mimi pia ni mkulima, nalima nanasi pwani, mpunga ifakara, na nmazao mengine mingi.
 
Mkuu hebu tafakari vizuri!!! Kwenye kilimo kuna minyororo ya umasikini!!!
una maana gani mkuu, naona kama una jeuri fulani kwamba hulimi,, bila shaka unasubili kulimiwa ili ule kwa sababu una fursa ya pesa...
Siku wakulima wakiacha kilimo cha biashara na kujilimia vyakula tu; mlioko mjini mtakula hayo matofali ya nyumba zenu
Hujamuelewa
 
hapo ni kijijini kuwa na akili hata ya kuzaliwa unajua serikali haija base kuendeleza baadhi ya miji ilitupwa kitambo sana mfano moshi, Tanga,lindi na mengine
sasa we ulitaka hao wana kijiji wafanye nn na je wanapachukia au wanalala njaa kaa kwa kutulia
 
Tutawezaje kujiondoa kwenye hiyo vicious circle of poverty?
Huu ukulima wa jembe la mkono tusitegemee kuwa utatutoa katika umasikini.

Enzi za Ukoloni Waingereza walihamasisha wakulima wenye hela kuja kulima Tanganyika. Kabla hujaoa was Ardhi na lease ya miaka 99 inaonyesha kiasi cha pesa kinachotakiwa kama kigezo. A hadi kubwa ni wajibu wako W kiendeleza ardhi.

Baada ya miaka miwili kama hujafanya maendeleo unanyang’anywa ardhi. Wagiriki na Wazungu wengi walifanya kilimo cha biashara na kilizalisha ajira nyingi.
 
Hatari sanaa, hapo kwenye elimu tunajitahidi kidogo, afya tunazidi kupiga hatua labda tutafika muda si mrefu, lakini kwenye hili suala la umasikini aseeeh! bado sana.

Umasikini ni mkubwa sana na unanuka, yaani sio wa kuukumbatia kabisa.

NB: kitu muhimu kabisa cha kufahamu, kama ilivyo minyororo ya thamani katika kilimo, pia kuna minyororo ya umasikini.
Huu ni uandishi wa jf sasa.
Thanks
 
Huu ukulima wa jembe la mkono tusitegemee kuwa utatutoa katika umasikini.

Enzi za Ukoloni Waingereza walihamasisha wakulima wenye hela kuja kulima Tanganyika. Kabla hujaoa was Ardhi na lease ya miaka 99 inaonyesha kiasi cha pesa kinachotakiwa kama kigezo. A hadi kubwa ni wajibu wako W kiendeleza ardhi.

Baada ya miaka miwili kama hujafanya maendeleo unanyang’anywa ardhi. Wagiriki na Wazungu wengi walifanya kilimo cha biashara na kilizalisha ajira nyingi.
Upo sawa,Watanzania tuliowengi hatufikirii kuwa kilimo kinaweza kufanywa kwa njia za kisasa na kikifanywa kuwa biashara,asilimia kubwa tunaota kuwa na majumba ya kupangisha,au kumiliki mabasi ya abiria,ni waTanzania wachache sana wenye mwamko wa kufanya kilimo cha kisasa,matokeo yake kumekuwa na kilo cha ajira,na wimbi la vijana ambayo ni nguvu kazi kumiminika kuishi mijini huku wakitegemea shughuli za kimachinga.
 
Upo sawa,Watanzania tuliowengi hatufikirii kuwa kilimo kinaweza kufanywa kwa njia za kisasa na kikifanywa kuwa biashara,asilimia kubwa tunaota kuwa na majumba ya kupandisha,au kumiliki mabasi ya abiria,ni waTanzania wachache sana wenye mwamko wa kufanya kilimo cha kisasa,matokeo yake kumekuwa na kilo cha ajira,na wimbi la vijana ambayo ni nguvu kazi kumiminika kuishi mijini huku wakitegemea shughuli za kimachinga.
Watu watatu mkiweka milioni 20 kila mmoja, muwe na malori ya usafiri mawili mfano canter. Muamue kulima heka 100 za mihogo na kila siku kuna canter moja kwa kuanzia inapeleka mihogo Dar.
 
Mkuu, hebu soma tena taratibu maana hujaelewa nilichoandika.

Na pia baada ya kuelewa nakuambia tu mimi pia ni mkulima, nalima nanasi pwani, mpunga ifakara, na nmazao mengine mingi.
Ndo nilikuwa nataka ufafanue pale tu kwamba kwenye kilimo kuna mnyororo wa umasikini, hilo tu
 
Back
Top Bottom