Haya ndio majibu ya Mh. Zitto ya kukosekana kwenye m4c

I rarery attack a personality of someone, it's wrong and uncivil; however, I subjectively excuse myself this time around.

Hivi huo u-smart na hiyo intelijensi kubwa ya Zitto ni upi? Watu wenye tongo tongo wanamwona Zitto bonge la intelligent guy (who is prbably closer to a super human). Well, that's their lot and choice of will

Zitto ni mtu wa kawaida sana. Kama angekuwa na smartness anayodhaniwa kuwa anayo hata 60% yake, basi asingekuwa anaingia kwenye skirmishes na silly controversies za aina yake, tena kwa kujirudia rudia. Na kama intelligence yake (kubwa) haimsadii kupambana na kuyashinda mazingira/changamoto zilizoko then anatofauti gani na mjomba wangu pale Iziba?

Ni afadhali ya JK dhaifu kuliko Zitto mnafiki. Kama ni kuchagua hata 2020 (suppose kapitishwa), siwezi mpa Zitto kura yangu ni afadhali iharibike; na kama NEC wakichakachua basi wampe JK.

The ego of Zitto is his undoing, it will never allow him to reach the potentials he once displayed. Ni individualist mkubwa, anashindwa kukubali kuwa sometime the best gain is to loose. Anavalue visakrifice mbuzi alivyotoa lakini wametoa damu na uhai wao na wala hawaitumii kama karata ya turufu kuhalalisha mapungufu yao.

With apology, that's my piece of mind
.

apology accepted.....your piece of mind!
 
MwanaHALISI limegundua.Taarifa zilizopatikana kutoka ndani ya idara hiyo zinaeleza kuwa vigogo hao wana mahusiano ya karibu na Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA, Zitto Kabwe.

Anayetajwa rasmi kuwa na mahusiano na Zitto ni Naibu Mkurugenzi wa TISS, Jack Zoka.
Kufichuka kwa taarifa za kuwapo “uswahiba” kati ya Zoka na Zitto kumekuja katika kipindi ambacho CHADEMA kimekuwa kikituhumu maofisa wa juu wa usalama wa taifa kuvuruga uchaguzi mkuu uliopita.

Aidha, kuibuka kwa tuhuma hizi kumekuja wiki moja baada ya gazeti hili kuchapisha taarifa mbalimbali za mawasiliano kati ya Zitto na Rais Jakaya Kikwete.

Baadhi ya mawasiliano hayo, ambayo Zitto ameyapeleka kwa rais, aliyapeleka pia kwa baadhi ya watuhumiwa ufisadi nchini.
Kwa mujibu wa mgombea urais wa CHADEMA, Dk. Willibrod Slaa ambaye alitangazwa kushika nafasi ya pili nyuma ya Rais Kikwete; viongozi wa TISS walihusika, kwa kiasi kikubwa, katika kile alichoita, “Kuchakachua matokeo ya uchaguzi.”

MwanaHALISI limefanikiwa kupata rekodi ya mshororo wa mawasiliano kati ya Zitto na Zoka.
Kuna mwingiliano wa simu za mdomo na maandishi (sms) kutoka kwa Zitto kwenda kwa baadhi ya vigogo wa ngazi ya juu serikalini na TISS, hasa Zoka.

Nyaraka za mawasiliano zinaonyesha kuwa Zitto amekuwa akiwasiliana na naibu mtendaji mkuu wa TISS huyo zaidi ya mara tatu kwa siku.

Kwa mfano, Zitto na Zoka walifanya mawasiliano ya simu mara tisa hapo tarehe 8 Agosti. Simu iliyotumika katika mawasilino hayo, ni Na. +255756809535 ambayo hutumiwa na Zitto na +255754787550 ambayo hutumiwa na Zoka.
Wakati mawasiliano hayo yanafanyika, Zitto alikuwa katika maeneo tofauti.

Mawasiliano ya kwanza kati ya Zitto na Zoka yalipokuwa yanafanyika, simu ya Zitto ilisomeka kuwa alikuwa katika maeneo mbalimbali.

Mathalani, wakati mwingine simu ilikuwa ikisomeka kuwa yuko Mtambani, Kinondoni Dar es Salaam, Kigoma Urban (Mjini), Kigoma Rural (Vijijini), Mtwara, Uwanja wa ndege-Ilala, Oyster Bay, Ukonga, Upanga na katikati ya mji.

Gazeti hili halikuweza kugundua mara moja undani wa mawasiliano ya Zitto na Zoka.
Kinachofanya baadhi ya wachunguzi wa mambo kujenga shaka ni kwamba mmoja ni mwanasiasa, tena kutoka chama kilichopo nje ya utawala; na mwingine ni mtumishi wa idara ya usalama inayolalamikiwa kukandamiza upinzani nchini.

Hata hivyo, taarifa zinaonyesha kuwa mawasiliano kati ya Zitto na Zoka yalianza kupamba moto kuanzia tarehe 6 Agosti 2010, siku moja baada ya CHADEMA kuzindua kampeni zake za urais.

Kulingana na uchunguzi, siku hiyo, tarehe 6 Agosti, simu ya Zitto ilisomeka kuwa yuko Kigoma Urban.
Katika mkutano wa ufunguzi wa kampeni, CHADEMA kupitia kada wake mashuhuri, Mabere Marando, iliibuka na lundo la tuhuma dhidi ya vigogo kadhaa wa serikali, CCM na idara ya usalama wa taifa.

Akizungumza na maelfu ya wananchi katika viwanja vya Jangwani, Dar es Salaam, Marando alisema wizi wa fedha katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA), ndani ya Benki Kuu ya taifa (BoT), ulifanywa na serikali na washirika wake.

Miongoni mwa vigogo aliodai kuwa walihusika kufanikisha wizi huo, ni rais wa sasa, Jakaya Kikwete, rais mstaafu Benjamin Mkapa, mbunge wa Igunga, Rostam Aziz na Edward Lowassa.

Akiongea kwa kujiamini, Marando alisema, “fedha za EPA ni wizi uliotiwa baraka na serikali ya CCM na ndio uliomsaidia rais Kikwete kuingia madarakani mwaka 2005.”

Kuanzia hapo hadi sasa, Zitto na Zoka wamekuwa na mawasilino ya mara kwa mara, na karibu kila siku huzungumza kwa simu.
Mawasiliano mengine ya mara kwa mara yalifanyika tarehe 7 Agosti 2010, siku mbili tangu hotuba kali ya Jangwani. Yalianza saa 10:17 na kuendelea tena saa 10:50, saa 10:51:31, saa 11:46:13, saa 12: 14:46, saa 12:26:48 na saa 13:50: 21.

Lakini Zitto alipoulizwa kuhusu sababu ya yeye kufanya mawasiliano ya mara kwa mara na vigogo wa TISS, alisema hajui na hakumbuki lolote kuhusu kuwapo mawasiliano hayo na Zoka au mkuu yeyote wa idara hiyo.

Zitto amesema yeye, akiwa mwanasiasa na kiongozi, anazungumza na watu wengi kutoka katika taasisi na mashirika mbalimbali ndani na nje ya nchi, lakini hajui kitu kuhusu usalama wa taifa.

Alipobanwa kuhusu mazungumzo yake na Zoka, hasa yale ya 3 Novemba 2010, saa nne na dakika 56 asubuhi, siku mbili baada ya uchaguzi kumalizika, Zitto alisema, “Siku hiyo nilizungumza na watu wengi sana. Siwakumbuki ni akina nani hasa.”

Alisema, “Hicho ndicho kipindi ambacho matokeo ya uchaguzi nchini kote yalikuwa yakizuiwa ikiwamo kwetu Kigoma. Na ukumbuke mimi nilipigwa mabomu na polisi na usalama wa taifa. Nakumbuka viongozi wengi wa vyombo vya ulinzi na usalama walinipigia simu kunijulia hali na kupata taarifa ya kilichotokea,” anaeleza.

“Sasa kama Zoka naye alinipigia siku hiyo sikumbuki; lakini nilipigiwa na wengi…Naomba uniambie kitu, hivi mnachokitafuta hasa ni nini?” aliuliza.

Katika njia ya kujitetea, Zitto aliuliza, “Mwanasiasa kuongea na wakuu wa vyombo vya usalama ni kosa? Maana, hata kama ningekuwa nimezungumza naye, kosa langu liko wapi?” alieleza mbunge huyo wa Kigoma Kaskazini.

Alipoelezwa kuwa haoni hiyo ni hujuma dhidi ya chama chake kwa kuzungumza na viongozi wa TISS na kile ambacho amekuwa akikizungumza kikiwa hakifahamiki kwa viongozi wake, Zitto alisema, “Sijawahi kukihujumu chama changu mahali popote, siku yoyote.”

Jitihada za gazeti hili kuzungumza na Zoka hazikufanikiwa katika kipindi chote
cha mwishoni mwa wiki, kwa vile kila alipopigiwa, simu yake ya mkononi ilikuwa haipokelewi.

Hata ujumbe mfupi wa maneno uliotumwa kwenye simu yake saa 2:53 asubuhi ya Jumapili; ukieleza sababu za gazeti kuzungumza naye, haukujibiwa.

Aidha, tarehe 2 Novemba, siku moja baada ya kuzungumza na Zitto, Zoka alinukuliwa akikana madai ya Dk. Slaa, kuwa TISS imesaidia kuvuruga uchaguzi.

Katika taarifa yake aliyoitoa mbele ya waandishi wa habari, ofisini kwake jijini Dar es Salaam, Zoka alisema, “Dk. Slaa amekuwa akidanganywa na watu wanaojiita maofisa wa usalama wa taifa.”

Hata hivyo, kuna meseji mbalimbali kuhusu udini na uamuzi wa CHADEMA kususia hotuba ya rais Kikwete ambazo zilitumwa na Zitto kwa baadhi ya wabunge wa CHADEMA ambazo zinadaiwa kuandaliwa na idara ya usalama wataifa.

Ujumbe huo unadaiwa kuandaliwa kwa ustadi mkubwa katika kukuza suala la udini na kuleta mtafaruku katika chama.

Mkuu Pompo,

Hii kitu nilikuwa nikiitafuta mda mrefu..

Mwanahalisi lilitakiwa kuwa mhimili mmojawapo wa dolla. Bunge, mahakama, serikali na mwanahalisi.
 
i concur...

unajua shida ipo wapi mkuu...ni hao wanaofikiri CDM ilianza 2010 baada ya wao kuingia......!

na unafiki wao upo wazi...akiongea wao wanafumba macho na akinyamaza wao wanafungua midomo...mfano majuzi hapa bungeni, aliitisha press conference na akatoa changamoto kuwa achunguzwe na ushahidi uwekwe wazi...umewaskia tena wakiongea, kama hawapo vile!!!

Siasa za bongo zinaangalia maslahi. Nafikiri ni vizuri kila mtu afanya yake, tuache kufocus kwenye maisha ya watu na kujenga hoja zisizo za msingi. Wana Jf tunaitwa viroporopo, hatuna kazi za kufanya, kutwa wangu wangu ku-discuss mambo yasiyotuhusu. Nahisi kila mtu ana mtazamo wake, huwezi kumzuia mtu kufikiri au kusema kile anachohisi kwamba ni sahihi. Mwisho wa siku ukweli anao mlengwa.
 
MKUBWA UKO SAHIHI, unajua tatizo kuna VIKARAGOSI vinavyotaka kugonganisha watu vichwa, na hivi vikaragosi ndivyo vilivyotufikisha hapa: vinataka kila siku ZITO, ZITO... ili watu tugonganishe vichwa vyetu... TUVIPUUZE VIKARAGOSI, tusonge mbele...
Mkuu ujumbe umefika!
 
cjayapenda majibu aliyotoa huyu kijana!cku zake kwene siasa na huo anaofikiri ni umaarufu alionao unahesabika!wait and see!
 
Zitto watanzania watakuhukumu kwa matendo yako sio hisia wala chuki kubali umekua tofauti urud kwenye mstari
 
Tweet to Zitto Zuberi Kabwe



9 Sep Abel Kaseko ‏@kaseko

Kuna maswali unatakiwa kuyajibu ili kufuta uongo wa kisiasa : kwamba haujawahi kuhudhuria Mikutano ya M4C.. @zittokabwe @omarilyas
9 Sep Zitto Zuberi Kabwe ‏@zittokabwe
@kaseko some of us rebranded the party and ensured its growth to now. Anybody knows CDM pre 2005? @omarilyas

9 Sep Fredrick Max ‏@Fredrickmax
@zittokabwe @kaseko @omarilyas kaseko hamna asiyetambua mchango wa Zitto kwa CDM..swali ni what works for now?
9 Sep Zitto Zuberi Kabwe ‏@zittokabwe
@MohamediMtoi kuna waliojali status quo, wakaendeleza kazi kujenga maisha yao kwanza na kisha kutufuata @Fredrickmax @kaseko @omarilyas

9 Sep Zitto Zuberi Kabwe ‏@zittokabwe
@MohamediMtoi hapana. Sitaki kusema chochote. Ninachosema ni kuwa 1) those who risked 2) those free riders (in public finance)....

9 Sep Zitto Zuberi Kabwe ‏@zittokabwe
@MohamediMtoi I am in Sri Lanka for a Commonwealth Parliamentary Association meeting. Also reading and writing - my favourites

9 Sep Fred Kavishe ‏@fredrooney
@zittokabwe all the best comrade

9 Sep Zitto Zuberi Kabwe ‏@zittokabwe
@Fredrickmax M4C is next level. We started with Sangara. Then Vua gamba Vaa gwanda na sasa M4C @MohamediMtoi @kaseko @omarilyas #M4C

9 Sep Zitto Zuberi Kabwe ‏@zittokabwe
@Fredrickmax don't pick up silly things. Triviality. Look the content of the subject matter @MohamediMtoi @kaseko @omarilyas #M4C

9 Sep Zitto Zuberi Kabwe ‏@zittokabwe
@MohamediMtoi hapana. Sitaki kusema chochote. Ninachosema ni kuwa 1) those who risked 2) those free riders (in public finance)....

9 Sep Zitto Zuberi Kabwe ‏@zittokabwe
@Fredrickmax ofcourse team work. I am proud to be part of the team which transformed the party. Sasa tupo wengi..... @kaseko @omarilyas

9 Sep Zitto Zuberi Kabwe ‏@zittokabwe
@MohamediMtoi I led the struggle from front when being chadema was old fashion. I am very happy now @Fredrickmax @kaseko @omarilyas

9 Sep Zitto Zuberi Kabwe ‏@zittokabwe
@MohamediMtoi kuna waliojali status quo, wakaendeleza kazi kujenga maisha yao kwanza na kisha kutufuata @Fredrickmax @kaseko @omarilyas

9 Sep Zitto Zuberi Kabwe ‏@zittokabwe
@MohamediMtoi kuna tulioona kwanza na kukataa status quo na kuingia kuweka msingi wa mabadiliko. @Fredrickmax @kaseko @omarilyas
9 Sep Zitto Zuberi Kabwe ‏@zittokabwe
@Fredrickmax what team spirit? Be specific @kaseko

9 Sep Zitto Zuberi Kabwe ‏@zittokabwe
@Fredrickmax Tunapokezana vijiti. Wengine tuli rebrand chama out of obscurity. Tumekuwa wengi. Tunasaidiana. No kelele @kaseko @omarilyas
9 Sep Zitto Zuberi Kabwe ‏@zittokabwe
@kaseko unapokuwa mwanasiasa kwenye nchi kama Tanzania ambapo principles and ideological orientation havina nafasi. Best, focus @omarilyas

9 Sep Zitto Zuberi Kabwe ‏@zittokabwe
@kaseko so achana na hao wanaoiona CHADEMA kwa jicho la M4C. Hata niwape utume watasema tu. I just move on with work, hardwork @omarilyas

9 Sep Zitto Zuberi Kabwe ‏@zittokabwe
@kaseko some of us rebranded the party and ensured its growth to now. Anybody knows CDM pre 2005? @omarilyas
9 Sep Zitto Zuberi Kabwe ‏@zittokabwe
@kaseko one thing, kuna watu wanataka kuaminisha umma kuwa CDM imeanza kujengwa after 2010. Wao walipoingia. Damn wrong @omarilyas
9 Sep Zitto Zuberi Kabwe ‏@zittokabwe
@kaseko when I do they close their eyes. When I don't they open their mouths @omarilyas

9 Sep Zitto Zuberi Kabwe ‏@zittokabwe
@kaseko nimefanya ziara Tanga. Nimefanya mikutano ya uchaguzi wa madiwani all over the country. Nimefanya Iringa. Tawi USA @omarilyas

9 Sep Zitto Zuberi Kabwe ‏@zittokabwe
@kaseko mikutano ya M4C...... It is very unfortunate. Ninafanya mikutano ya chama #CHADEMA ndani na nje ya nchi @omarilyas


Juzi Juzi alimsindikiza RAIS KIKWETE kilioni ETHIOPIA... PICHA CHINI ZITTO KABWE yuleeee... Anaangalia na kufurahi... SIO

YEYE Aliyetaka kulivunja BUNGE ? Naona wako kitini na SPIKA wa BARA MAKINDA na SPIKA wa NCHI ya ZANZIBAR...

3.JPG



Kula Maraha WABUNGE Wananchi Hawana Shida... Mnasafiri Kweli...

6.jpg
 
Siasa za bongo zinaangalia maslahi. Nafikiri ni vizuri kila mtu afanya yake, tuache kufocus kwenye maisha ya watu na kujenga hoja zisizo za msingi. Wana Jf tunaitwa viroporopo, hatuna kazi za kufanya, kutwa wangu wangu ku-discuss mambo yasiyotuhusu. Nahisi kila mtu ana mtazamo wake, huwezi kumzuia mtu kufikiri au kusema kile anachohisi kwamba ni sahihi. Mwisho wa siku ukweli anao mlengwa.

nakubaliana nawe Caroline...

....shida ni kuwa uongo unapokaririwa sana mwisho huonekana kama ni kweli vile na hapo kwa wenye ufahamu hugeuka kero na kushindwa kujizuia na kulazimika kuongea walau kuu-neutralise uongo huo.
 
Back
Top Bottom