WanaJF,
Tokea CDM ianzishwe mnamo mwaka 1992, sasa yapata miaka ipatayo 21.
Lakini katika kipindi chote hiki cha uwepo wa chama hicho katika uwanja wa siasa za ushindani, bado tija ya CDM haijaonekana kabisa, zaidi zaidi ni mambo ya ajabu ajabu tu ndio ambayo yamekuwa yakifanywa na chama hicho ambayo kimsingi mambo hayo ndio huitwa MAFANIKIO YA CDM. Baadhi ya MAFANIKIO ya CDM tangu kuanzishwa kwake ni:
i) Kuchochea mgawanyiko wa kikabila na kikanda nchini. Hapa wamefanikiwa ingawa sio kwa kiasi kikubwa kutokana na kudhibitiwa na serikali ya CCM.
ii) Kushushwa kwa hadhi kwa jiji la Arusha na kupelekea kupungua kwa idadi kubwa ya watalii na kushuka kwa mapato ya jiji hilo. Hapa pameratibiwa na Lema.
iii) Kuhamasisha vijana watumie mihadarati kama vile bangi, gomba, milungi, kuberi na viroba. Hapa wamefanikiwa sana hasa kwa vijana wa Arusha na Mbeya.
iv) Kuwekeza kwenye matusi na fujo. Hapa CDM imefanikiwa mno hasa ukizingatia chama kimemkabidhi hii sekta mtu aina ya Sugu (mb) ili kuweza kuiratibu. Katika historia ya nchi yetu, ni kwa mara ya kwanza tumeshuhudia ngumi kupigwa bungeni pamoja na kutukanwa kwa viongozi wa kitaifa.
v) Kutoa kafara Watanzania kwa kisingizio cha haki ya maandamano na mikusanyiko. Wote tunajua kuwa Mbowe ni mfanyabiashara na miaka ya hivi karibuni baada ya kumwaga damu ya kutosha ya Watanzania biashara yake imeonekana kustawi. Unaweza ku-connect dots hapo.
Haya ni baadhi tu ya mafanikio ya CDM ila ni imani yangu yapo mengine mengi ambayo yamefanywa na chama hicho cha kifamilia. Hivyo kuwa huru kujazia jazia mafanikio unayo yafahamu ya hiki chama
Tokea CDM ianzishwe mnamo mwaka 1992, sasa yapata miaka ipatayo 21.
Lakini katika kipindi chote hiki cha uwepo wa chama hicho katika uwanja wa siasa za ushindani, bado tija ya CDM haijaonekana kabisa, zaidi zaidi ni mambo ya ajabu ajabu tu ndio ambayo yamekuwa yakifanywa na chama hicho ambayo kimsingi mambo hayo ndio huitwa MAFANIKIO YA CDM. Baadhi ya MAFANIKIO ya CDM tangu kuanzishwa kwake ni:
i) Kuchochea mgawanyiko wa kikabila na kikanda nchini. Hapa wamefanikiwa ingawa sio kwa kiasi kikubwa kutokana na kudhibitiwa na serikali ya CCM.
ii) Kushushwa kwa hadhi kwa jiji la Arusha na kupelekea kupungua kwa idadi kubwa ya watalii na kushuka kwa mapato ya jiji hilo. Hapa pameratibiwa na Lema.
iii) Kuhamasisha vijana watumie mihadarati kama vile bangi, gomba, milungi, kuberi na viroba. Hapa wamefanikiwa sana hasa kwa vijana wa Arusha na Mbeya.
iv) Kuwekeza kwenye matusi na fujo. Hapa CDM imefanikiwa mno hasa ukizingatia chama kimemkabidhi hii sekta mtu aina ya Sugu (mb) ili kuweza kuiratibu. Katika historia ya nchi yetu, ni kwa mara ya kwanza tumeshuhudia ngumi kupigwa bungeni pamoja na kutukanwa kwa viongozi wa kitaifa.
v) Kutoa kafara Watanzania kwa kisingizio cha haki ya maandamano na mikusanyiko. Wote tunajua kuwa Mbowe ni mfanyabiashara na miaka ya hivi karibuni baada ya kumwaga damu ya kutosha ya Watanzania biashara yake imeonekana kustawi. Unaweza ku-connect dots hapo.
Haya ni baadhi tu ya mafanikio ya CDM ila ni imani yangu yapo mengine mengi ambayo yamefanywa na chama hicho cha kifamilia. Hivyo kuwa huru kujazia jazia mafanikio unayo yafahamu ya hiki chama