Haya ndio madai taslimu ya Tundu Lissu!

Freyzem

JF-Expert Member
Jun 29, 2013
10,049
24,428
Baada ya lile tukio baya kabisa lililompata mbunge, T. Lissu la sept 7, 2017 na kukimbizwa Nairobi kwa matibabu yaliyookoa uhai wake na hatimae Ubelgiji, basi kumekuwa na sintofahamu juu ya stahiki zake alizopaswa kulipwa na bunge!
...Stahiki alizotakiwa kulipwa ni posho ya siku ya kwake yeye binafsi, pamoja na 20% ya posho yake kwa msaidizi mmoja ambapo gharama hizi ni nje ya gharama za matibabu!
..Kwa mujibu wa sheria Lissu alipaswa kulipwa posho takribani dola 450 kwa siku pamoja na dola 90 za msaidizi wake( ambaye ni mkewe) kwa siku na kufanya jumla ya dola 540 kwa siku!
..Hivyo, basi hadi hivi sasa ambapo ni takribani miezi 17 imeisha tokea aumizwe, ni kuwa anapaswa kulipwa si chini ya dola 275,000.
Ikumbukwe pia kiwango hiki kinazidi kupanda kadiri siku zinavyozidi kuendelea!
..zaidi ni kuwa kiwango hiki kililipwa kwa spika ndugu, J. Ndungai aliyekuwa amelazwa india kwa matibabu yaliyokuwa si chini ya miezi mitano, na pia hata aliyekuwa spika mstaafu Ndugu, S. Sitta baada ya kumaliza muda wake wa ubunge alilazwa nchini uingereza na bunge liliwajibika kumlipa japokuwa hakuwa mbunge!
..hivyo, basi kwenye hili suala la Lissu, ni vyema zaidi busara ikatumika kuliko kuingiza siasa na viroja, ili aweze kupata stahiki zake!
Wabunge wote, waungane wamtetee, mbunge mwenzao bila kujali itikadi, maana kama watashindwa kumtetea mbunge mwenzao, vipi kuhusu raia/ wananchi ambao ndio wapiga kura waliowapa dhamana..!? Watatetewa na nani...
Hakika, TAML usinyamaze kamwe...

Sent using Vertu Signature Cobra
 
Watakuambia kwanini mlikataa asitibiwe Muhimbili kwa gharama ya serikali?

Kwamba Lissu ambae alikuwa fatally injured angefaa kutibiwa Muhimbili ila wenye obesity wanaenda kutibiwa nje ya nchi kwa kodi ya wanachi na vitambi vyao vilivyojaa mangurunyi.
 
Watakuambia kwanini mlikataa asitibiwe Muhimbili kwa gharama ya serikali
Hiyo, hoja mkuu namna wanavyoitetea haina mashiko..
Kwani sitta alikuwa na rufaa ya muhimbil?
Halafu kama ambavyo, ilishakwisha elezwa kwenye yale mazingira ya tukio kulikuwa hamna njia nyingine ya kuokoa uhai wake zaidi ya kumpeleka nje ya nchi!
Imagine kama jamaa, waliweza kufanya ule uhuni namna ile mchana kweupe, wangeshindwaje kuingia muhi2 na kufanya yao, wakahakikisha wamemaliza kazi kabisa..?!

Sent using Vertu Signature Cobra
 
Mungu akubariki Mkuu umeongea ukweli mtupu ila ngoja vijana wa Chakubanga waje maana wapo ktk foleni za kuingiziwa bando
 
Hiyo, hoja mkuu namna wanavyoitetea haina mashiko..
Kwani sitta alikuwa na rufaa ya muhimbil?
Halafu kama ambavyo, ilishakwisha elezwa kwenye yale mazingira ya tukio kulikuwa hamna njia nyingine ya kuokoa uhai wake zaidi ya kumpeleka nje ya nchi!
Imagine kama jamaa, waliweza kufanya ule uhuni namna ile mchana kweupe, wangeshindwaje kuingia muhi2 na kufanya yao, wakahakikisha wamemaliza kazi kabisa..?!

Sent using Vertu Signature Cobra
Lengo lau linafahamika, walitaka wammalize kwa njia ya kimya kimya baada ya kushindwa kwa risasi.

Napongeza sana viongozi wa CHADEMA na wote waliopigana kumpeleka Lissu nje ya hii nchi.

Lissu will come back even stronger than when he left.
 
Si ajabu aliyrandika Uzi huu hata dola hajawahi ishika, anadhani dola ni kama sarafu za kuchezea machine za betting za kichina
 
Lengo lau linafahamika, walitaka wammalize kwa njia ya kimya kimya baada ya kushindwa kwa risasi.

Napongeza sana viongozi wa CHADEMA na wote waliopigana kumpeleka Lissu nje ya hii nchi.

Lissu will come back even stronger than when he left.
For sure mkuu...
Zaidi ni kwamba, hata huko alipo inabidi awe makini sana maana adui anaweza kujichanganya, maadui ni lazima watakuwa wamegeuzia dish pande za europe na marekani!

Sent using Vertu Signature Cobra
 
Huo ni Ujinga sasa mtu kashapona saivi anadhurura tu Ulaya huko bado aendelee kulipwa!? Afu kama mgonjwa mpaka kuamua kutofata taratibu za rufaa ni kuwa hao waliomkimbiza Nairobi ni walijua fika mshiko wanao wakumtibu huko sasa acheni kulia lia, Ikiwa kila mbuge ataumwa na kutaka kukimbilia nje na alipwe huoni pesa zetu za kodi zitatumika tu ovyo.
 
Baada ya lile tukio baya kabisa lililompata mbunge, T. Lissu la sept 7, 2017 na kukimbizwa Nairobi kwa matibabu yaliyookoa uhai wake na hatimae Ubelgiji, basi kumekuwa na sintofahamu juu ya stahiki zake alizopaswa kulipwa na bunge!
...Stahiki alizotakiwa kulipwa ni posho ya siku ya kwake yeye binafsi, pamoja na 20% ya posho yake kwa msaidizi mmoja ambapo gharama hizi ni nje ya gharama za matibabu!
..Kwa mujibu wa sheria Lissu alipaswa kulipwa posho takribani dola 450 kwa siku pamoja na dola 90 za msaidizi wake( ambaye ni mkewe) kwa siku na kufanya jumla ya dola 540 kwa siku!
..Hivyo, basi hadi hivi sasa ambapo ni takribani miezi 17 imeisha tokea aumizwe, ni kuwa anapaswa kulipwa si chini ya dola 275,000.
Ikumbukwe pia kiwango hiki kinazidi kupanda kadiri siku zinavyozidi kuendelea!
..zaidi ni kuwa kiwango hiki kililipwa kwa spika ndugu, J. Ndungai aliyekuwa amelazwa india kwa matibabu yaliyokuwa si chini ya miezi mitano, na pia hata aliyekuwa spika mstaafu Ndugu, S. Sitta baada ya kumaliza muda wake wa ubunge alilazwa nchini uingereza na bunge liliwajibika kumlipa japokuwa hakuwa mbunge!
..hivyo, basi kwenye hili suala la Lissu, ni vyema zaidi busara ikatumika kuliko kuingiza siasa na viroja, ili aweze kupata stahiki zake!
Wabunge wote, waungane wamtetee, mbunge mwenzao bila kujali itikadi, maana kama watashindwa kumtetea mbunge mwenzao, vipi kuhusu raia/ wananchi ambao ndio wapiga kura waliowapa dhamana..!? Watatetewa na nani...
Hakika, TAML usinyamaze kamwe...

Sent using Vertu Signature Cobra
Nani kakudanganya kwamba Wabunge wapo kwa ajili ya kutetea maslahi wa Wananchi? Iweje Wabunge hawalipi kodi, mafao yao wanachukua yote baada ya kila miaka mitano lkn wananchi tunayasotea,halafu useme eti Mbunge akutetee,acha mashala basi.....!!!!
 
Back
Top Bottom