Haya mateso wanayopata abiria wa daladala ni makubwa. Serikali iwe na huruma!

mtotomtamuu

JF-Expert Member
Dec 4, 2016
602
1,454
Ifike mahali Serikali yetu iwe kitu kimoja linapokuja suala la msimamo halisi wa Nchi. Nchi nzima iegemee kwenye ukweli ili kama haya mateso tunayapata tujue tunayapata kwa usalama wetu au kwa ajili ya siasa

Nimetoka Ubungo leo kuelekea mbagala hadi sasa Serikali haijaruhusu magari kusimamisha abiria, sasa kitu kilichonisikitisha zaidi ni namna ya Abiria wabavyopangwa kama mafungu yani watu wanapata shida sana, sehemu ya kusimama ile kwenye mabasi makubwa yale ya Eicher watu wanachuchumaa kwa mstari kama wakimbizi, yote hayo askari asijue kama kuna watu wamesimama kuepuka faini, Na watu wengi wanakosa usafiri sababu gari ni chache na sheria ni level seat

Sasa kinachonishangaza mimi ni Serikali imetangaza kuwa kwa sasa kumesaliwa na wagonjwa wanne nchi nzima na kuaminisha watu kuwa hali ni shwari na watu kwa sasa barakoa washazitupa na wanajiachia, sasa kama mnachokisema ni kweli kwa nini muache watu wanateseka kwenye usafiri wa Daladala?

Ni muda muafaka wa Serikali kurudisha usafiri wa Dala dala kwenye hali yake kama kweli hali ni shwari la sivyo mtakuwa mnatudanganya,
 
Mapinduzi ya usafiri wa umma kwa Dar yanahitajika haraka sana. Serikali iliangalia kwa jicho la tatu hili suala.

Sishabikii kusimama ila nashabilia kuongezwa kwa mabasi na kuongeza flyover kila kona ili watu wasikae sana kwenye foleni
 
Yaani bado unawaza daladala zi simamishe aburia? Mkuu hata sheria za latra haziruhusu huu ujinga wewe omba serikali iongeze kasi kwenye usajili wa daladala.

Corona bado ipo vaa barakoa nawamikono na maji tiririka.
 
Yaani bado unawaza daladala zi simamishe aburia?mkuu hata sheria za latra haziruhusu huu ujinga wewe omba serikali iongeze kasi kwenye usajili wa daladala.
Corona bado ipo vaa barakoa nawamikono na maji tiririka.
kabla hujasema hivyo jiulize kuna magari ya kutosha kupandisha abiria level seat?

unaleta sheria wakati gari za kutosha hamna
 
wakazi wa Mbagala wanaumia sana kwenye suala la usafiri

Ila sasa hivi wakazi wa mbezi ya kimara,nadhani wanatamani

Huu utaratibu wa level seat uendelee hivi hivi maana akiwa na

buku anauhakika wa bus la direct from mbezi to k.koo kwenda

na kurudi ila mbagala mbagala huku nadhani Panahitaji kauli,twaafaa.
 
Mapinduzi ya usafiri wa umma kwa dar yanahitajika haraka sana. Serikali iliangalia kwa jicho la tatu hili suala.

Sishabikii kusimama ila nashabilia kuongezwa kwa mabasi na kuongeza flyover kila kona ili watu wasikae sana kwenye foleni
Umeona flyover Ubungo inachofanya kwa waendao Mbezi?
 
Yaani bado unawaza daladala zi simamishe aburia?mkuu hata sheria za latra haziruhusu huu ujinga wewe omba serikali iongeze kasi kwenye usajili wa daladala.
Corona bado ipo vaa barakoa nawamikono na maji tiririka.
Tulia uandike vizuri mkuu.
 
Levo siti imekuja na faida zake kama,gari kuwahi kufika kutokana na kutosimama kila kituo,foleni nazo zimepungua kiasi flani, at least unapata hewa safi kwasababu hakuna mbanano,ila changamoto ni nyingi zaidi gari ni chache kuliko abiria,kuchuchumaa ni adhabu kubwa asikwambie mtu,bila kutumia nguvu huwezi kupata gari kabisa.

Inakulazimu kuamka mapema kabla abiria hawajawa wengi kituoni, kwa kifupi ishu ya levo siti kwa nchi zetu za kiafrika bado hatuwezi waliweza Africa kusini ila huku kwingine bado sana,kwa kifupi kwa mji kama dar reli ndio ilikua suruhisho kubwa kuliko mwendokasi.
 
Kosa la serikali hapo ni Nini Sasa! Unachuta mwenyewe kwa hiari yako...unakuja ilaumu serikali! Unapangwa Kama matikiti kwa hiari yako badala ya kusubiri gari nyingine ukae kwenye seat, afu unailaumu serikali na kujisahau mwenyewe. Huu nao sijui tuuiteje!?
 
Kosa la serikali hapo ni Nini Sasa! Unachuta mwenyewe kwa hiari yako...unakuja ilaumu serikali! Unapangwa Kama matikiti kwa hiari yako badala ya kusubiri gari nyingine ukae kwenye seat, afu unailaumu serikali na kujisahau mwenyewe...huu nao sijui tuuiteje!?
Hata Mimi namshangaa huyo jamaa..kwani ulilazimishwa mtu kusimama!?
 
Yaani mpaka kuchuchumaa serikali waingilie? Unaona gari limejaa unapanda, acha uchuchumae.
 
Back
Top Bottom