Haya matangazo, Je wanatujengaje saikolojia zetu?.

Mringo

JF-Expert Member
Jun 23, 2010
320
100
Jamani mimi nimekua nakasirishwa sana na matangazo yanayotangazwa na vyombo vyetu vya habari ..halafu mwishoni mara unasikia linafadhiliwa na watu wa marekani....
1. Tangazo la kunawa mikono: Likiwa na story za karne ya 17 au nyuma.Eti mtu alipewa mali na mfalme fulani baada ya kumpikia chakula kitamu na siri kubwa eti alinawa mikono ktk kijito fulani...this is shame ktk karne hii ya digitali
2. Tangazo la dawa za malaria: Zikionyesha watu wenye hali mbaya kimaisha tena inayoonyesha mwanaume aliyekosa dira kimaisha anyewaza kwenda kijiweni tu, na jingine mwanaume anayegombezwa na mkewe.
3. Tangazo la ulevi ni noma: Likishawishi tunywe pombe mpaka tukibakiwa na funda moja la mwisho kuwa taabani. Huku waigizaji ambao ndio wametumika kama kielelzo cha karibia na "full tank" wakionyesha kulewaa mbaya..

Hivi haya matangazo yana malengo gani na sisi watanzania?? Hvi wanajenga saikolojia gani kwa vizazi vinavyokua kwa sasa??..kuamini tu kunawa mikono kunatosha kupata mambo makubwa..wameshindwa nini kueleza maradhi yatokanayon na kutokunawa mikono badala yake wanazidi kutupotosha watanzania??
Hivi watawala wanatuchukuliaje sisi watawaliwa..nadhani sisi sio mambumbu kihivyo
 
Mkuu umesahau kionjo wanachomalizanacho "... kwa hisani ya watu wa Marekani". Jaman hata kampeni ya kunawa mikono!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom