Mvaa Tai
JF-Expert Member
- Aug 11, 2009
- 6,159
- 4,442
Katika vuta nikuvute ya Serikali na madaktari inahusisha makundi matatu. Kuna 1(Rais), 2(Madaktari) na 3(Mawaziri yaani Nkya, Mponda).
Ninaamini mgomo uliotishiwa kuanza leo ukitekelezwa utapelekea vifo vya watu wengi kama uliopita. Kwasababu hivi vifo vinaweza kuzuilika iwapo kundi moja litawaonea huruma wagonjwa wasio na hatia. Kwa mfano Madaktari wakisitisha mgomo wao watu wataendelea na matibabu kama kawaida, lakini wakiendelea na msimamo wao Rais anaweza kuwasimamisha hawa mawaziri watu waendelee na matibabu kama kawaida, lakini pia Rais akiendelea na msimamo wa kuwalinda hawa mawaziri, Waziri Mponda na Nkya kwa kuwaonea huruma binaadam watakaokufa kutokana na mvutano huu wanaweza wakaacha kazi ili waokoe uhai wa binaadam kwani uwaziri kitu gani mbele ya uhai wa binaadamu??. Sasa Ninaamini katika haya makundi matatu siyo wote wana roho ya kiuaji, Sisi binaadamu naturally ni wabinafsi lakini katika hili ninaamini hatakufa mtu kwani sidhani kama Madaktari,Kikwete, Mponda na Nkya watakubali watu wafe ili wao washinde katika mvutano huu.
Ninaamini mgomo uliotishiwa kuanza leo ukitekelezwa utapelekea vifo vya watu wengi kama uliopita. Kwasababu hivi vifo vinaweza kuzuilika iwapo kundi moja litawaonea huruma wagonjwa wasio na hatia. Kwa mfano Madaktari wakisitisha mgomo wao watu wataendelea na matibabu kama kawaida, lakini wakiendelea na msimamo wao Rais anaweza kuwasimamisha hawa mawaziri watu waendelee na matibabu kama kawaida, lakini pia Rais akiendelea na msimamo wa kuwalinda hawa mawaziri, Waziri Mponda na Nkya kwa kuwaonea huruma binaadam watakaokufa kutokana na mvutano huu wanaweza wakaacha kazi ili waokoe uhai wa binaadam kwani uwaziri kitu gani mbele ya uhai wa binaadamu??. Sasa Ninaamini katika haya makundi matatu siyo wote wana roho ya kiuaji, Sisi binaadamu naturally ni wabinafsi lakini katika hili ninaamini hatakufa mtu kwani sidhani kama Madaktari,Kikwete, Mponda na Nkya watakubali watu wafe ili wao washinde katika mvutano huu.