Utani wa Makabila: Ijue Historia ya utani wa Makabila Tanzania

Sikonge,

Big up mkuu, sasa watu waelewe haya mambo ndo yaliyoleta utani, someni historia ya nchi yenu jamani mjue mambo yaliendaje?
 
Nakumbuka rafiki yangu mmoja aligombana na mtani wake kwani utani ulivuka mipaka. Alimtania mpaka akawa anamshika wife wake akidai ni wife wake (huyo mtani). Sometimes watu wanaleta utani msibani au harusini mpaka kusababisha watani wao kukasirika. Je utani una kikomo?
 
Eh Bwana mdogo msingi wa utani wa makabila ni vita hapo zamani wakati makabila yalipokuwa yanahama. kulitokea uhasama kati ya makabila mbayo ni watani wenye nguvu waliahama sehemu walipokuwa wakiwaachia wageni au wageni walishindwa na kuendelea na safari, hivyo kuleta hisia za kudharauliana na kuanza kutaniana, aidha makabila mengine ilikuwa ni dhuluma za biashara mfanao wasumbwa na wahaya- hawa wasumbwa walikuwa wanasafirisha chumvi na kuwauzia ila kwa kuangalia tofauti ya tamaduni zao wakaanza kutaniana. makabila mengine ni majirani walitaniana kwa kudharau baadhi ya tamaduni na mila tofauti. kwa kifupi ni hayo
 
Eh Bwana mdogo. msingi wa utani wa makabila ni vita hapo zamani wakati makabila yalipokuwa yanahama. kulitokea uhasama kati ya makabila mbayo ni watani wenye nguvu waliahama sehemu walipokuwa wakiwaachia wageni au wageni walishindwa na kuendelea na safari, hivyo kuleta hisia za kudharauliana na kuanza kutaniana, aidha makabila mengine ilikuwa ni dhuluma za biashara mfanao wasumbwa na wahaya- hawa wasumbwa walikuwa wanasafirisha chumvi na kuwauzia ila kwa kuangalia tofauti ya tamaduni zao wakaanza kutaniana. makabila mengine ni majirani walitaniana kwa kudharau baadhi ya tamaduni na mila tofauti. kwa kifupi ni hayo

Mkuu,
Ahsante sana kwa kunipa mwangaza huo, nathamini ulichonieleza.
 
Mfano wa utani wa Mgogo na Mnyamwezi, ilikuwa hivi: Wanyamwezi walikuwa Wafanya biashara na walikuwa wanaenda Pwani kuchukua bidhaa wakirudi wanapitia Dodoma. Wakifika Dodoma wanawakuta Wagogo, na Wagogo wanawaomba Wanyamwezi bidhaa zao ili waaangalie wakijifanya kushangaa, wakiwapa tu wanakimbia nazo kwenye majani yenye miba na mbigili na Wanyamwezi wanashindwa kuwafuata wakiogopa kujichoma na miba.
 
Hii ilitokana na vita vya enzi hizo za mababu zetu, mfano wangoni walipoingia Bongo toka South, waliingia Sumbawanga wakapiga kule, wakapita Tabora wakatwanga wanyamwezi na wasukuma, Iringa furusha wahehe, na wabena halafu ndo waka settle SONGEA/RUVUMA. sasa huko walikopita kote hawa sasa hivi ni watani wa WANGONI- Wafipa, wasukuma, wanyamwezi, wahehe, na kuna makabila menine madogo madogo na si strategy ya Nyerere wala mtu binafsi hii ni HISTORIA.
Mngekuwa na ubavu wa kuwapiga wahehe si mngelinga? wahehe ndo kabila lenye nguvu kushinda Yote kusini mwatanzania na tanzania kwa ujumla na ndo kabila pekee lenye historia ya kumpiga mjerumani, na ndo maana wangoni mkaungana na mjerumani kuja kupigana na wahehe.
 
Wakuu naomba kuuliza swali hilo hapo kwenye heading. Kwa dharau na majivuno waliyonayo wahaya wanawezaje kuwa marafiki(mtani) wa wakurya kabila ambalo siku zote watu wake wanasisitiza kuwa dharau kwao ni mwiko?
Nimeuliza hivi kutokana na tabia za wahaya wengi niliokaa nao kuonekana ni watu wenye dharau iliyopitiliza. Naomba kuujuzwa utani wao ulivyo.
kumbuka;
Ni vigumu sana kwa mkurya kuwa na uhusiano wowote na mtu yeyote mwenye dharau ama majigambo.
Cc:mad:excel
charminglady
Molemo@mwitamaranya nk.
 
Last edited by a moderator:
Wakurya ni wajukuu wa wahaya, kwa hiyo hata iwe vipi babu / bibi hawezi mdharau mjukuu. Na mjukuu hawezi chukizwa na utani wa babu/bibi.
 
Huo ujukuu ulianzaje? na kwanini wakurya hawana dharau na majivuno kama wahaya?

Thibitisha hitimisho lako la kuwa wahaya wanadharau na majivuno. Je wajua kuwa babu /bibi na mjukuu wanaweza kuwa na tabia tofauti kulingana na mazingira?
 
Msaidieni ajue historia,huo utani ulianzaje! Hii inaweza kuwa faida hata kwa wengine

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Thibitisha hitimisho lako la kuwa wahaya wanadharau na majivuno. Je wajua kuwa babu /bibi na mjukuu wanaweza kuwa na tabia tofauti kulingana na mazingira?

Najua wanaweza kuwa na tofauti ila siyo ya asili! mfano wakurya ni watata toka enzi za enzi na bado wanasomeka hivyo siku zote, je kusema hivyo ni vizazi vingapi vimepita?
 
Mleta mada hii unatakiwa ujue makabila na asili, mila na tamaduni zao ndipo uje kuuliza la Wakurya na wahaya. Pili napenda nikusahihishe kidogo, ni kwamba wahaya na Wanyambo wanataniana na Wakerewe, Wajita, Wajaluo na Wakurya amabao katika wakurya kuna vikabila au koo kama Wasimbiti, wangorome, Wasweta, Waruri, Wazanaki, Wakabwa, wakiroba, Wakwaya, Waikoma, Wanata, Waisenye, Waikizu etc Vile Vile Wahaya na Wanyambo wanataniana na Waha wa Kigoma
Ukishajua hivyo ndipo uje na swali lako
 
Mleta mada tambua kwamba there is no one who can make you inferior without your permission. Kwahiyo suala kwamba wahaya wana dharau ni kutojiamini kwako kutako kufanya ujisikie unadharaulika.
 
Mleta mada tambua kwamba there is no one who can make you inferior without your permission. Kwahiyo suala kwamba wahaya wana dharau ni kutojiamini kwako kutako kufanya ujisikie unadharaulika.

Hayo mambo ya inferior yanahusianaje na swali nililouliza?
"Kuelewa swali ni nusu ya jibu".
 
Kuna jamaa angu mhaya alikuwa anaoa basi rafiki yetu mkurya akaenda pale kwenye kiti cha bwana harusi akakaa anagoma kutoka mpaka pesa itolewe
 
Back
Top Bottom