Display Name
JF-Expert Member
- Feb 11, 2014
- 423
- 451
Wakuu habari za muda huu, hongereni kwa mapambano dhidi mdudu huyu mchafu Corona.
Wacha twende moja kwa moja kwenye mada yetu, dada yangu ana watoto wake wa kiume mwenye miaka 15 (nataja umri ili huu ushauri uone kama umri ndio chanzo au la)
Sababu ya kuleta mada hii hapa ni hii, huyu mtoto amekuwa na tabia ya kupendelea kumwita mama yake Mama Amani (yeye jina lake ndio Amani) au wakati mwingine hata cheo chake cha kazini (Chief Accountant wa kampuni ******) au dadake Display Name au vyovyote tu atakavyojisikia aiki hiyo
Mama yake amekuwa na wasiwasi flani labda mtoto hampendi au heshima imepungua kwenye jinsi mtoto wake amekuwa akimwita, mimi nimemwambia ni kawaida maana nimeshuhudia watu wengi wakiwapa mama zao/baba zao majina flani hivi, dada ameonekana kama kaelewa ila ka wasiwasi nakaona kwa mbaali bado kapo.
Je, hili ni jambo la kuwa na wasiwasi nalo au tumuache dogo aendelee na maisha?
Wacha twende moja kwa moja kwenye mada yetu, dada yangu ana watoto wake wa kiume mwenye miaka 15 (nataja umri ili huu ushauri uone kama umri ndio chanzo au la)
Sababu ya kuleta mada hii hapa ni hii, huyu mtoto amekuwa na tabia ya kupendelea kumwita mama yake Mama Amani (yeye jina lake ndio Amani) au wakati mwingine hata cheo chake cha kazini (Chief Accountant wa kampuni ******) au dadake Display Name au vyovyote tu atakavyojisikia aiki hiyo
Mama yake amekuwa na wasiwasi flani labda mtoto hampendi au heshima imepungua kwenye jinsi mtoto wake amekuwa akimwita, mimi nimemwambia ni kawaida maana nimeshuhudia watu wengi wakiwapa mama zao/baba zao majina flani hivi, dada ameonekana kama kaelewa ila ka wasiwasi nakaona kwa mbaali bado kapo.
Je, hili ni jambo la kuwa na wasiwasi nalo au tumuache dogo aendelee na maisha?