Haya huyo wenu wa CIA mnayemuami kwamba ni mkweli, aletwe sakata la Tundu Lisu!

Kwanza tuwekane sawa; CIA hawafanyi kazi ya uchunguzi wa matukio ya kihalifu kama ya kushambuliwa kwa risasi kwa bwana Tundu Lissu

Barbosa,
Kwanza jambo moja inabidi lifahamike wazi kwamba CIA hawafanyi uchunguzi wa matukio ya kijinai kama ya kutekwa, mauaji, ubakaji au ujambazi, iwe huko kwao America,au nje ya America.
Wanaohusika na uchunguzi wa matukio ya kihalifu kama hayo huko America ni polisi ambao nao wakizidiwa wanaomba msaada kwa FBI ambayo ni taasisi bobezi kwa mambo hayo.
CIA ni taasisi ya kijasusi kama ilivyo MI6 ya Uingereza, au Mossad ya Israeli ,au FSB ya Russia,na au ilivyo Tiss hapa kwetu.
Kwa hiyo kama serikali ingeomba msaada wa kiuchunguzi wa matukio ya kijinai kutoka America, watakaokuja ni FBI, siyo CIA. Vivyo hivyo ikitokea serikali imeomba msaada wa kiuchunguzi toka Uingereza, watakao kuja kufanya kazi hiyo ni Scotland Yard, na siyo MI6.
Matokeo ya uchunguzi unaofanywa na taasisi hizi za aina ya Scotland yard na FBI au kama polisi wetu,ndiyo huo huja kutumika mahakamani. Na kwa vile matokeo ya kazi zao hizi za kiuchunguzi baadaye huja kutumika mahakamani, hivyo basi kazi nzima ya kiuchunguzi huwa ya kisayansi zaidi ili kupata ushahidi thabiti. Mathalan, kwa sasa kutokana na matumizi ya kiuchunguzi yanayohusisha vinasaba (DNA) yamerahisisha kuwakamata wahalifu wa ubakaji au hata wauaji na kutiwa hatiani bila ya shaka.
Ni kweli CIA na hata taasisi nyingine za kijasusi wanaweza kudanganya kama sehemu ya propaganda. Hata taasisi yetu ya kijasusi ya TISS inaweza kudanganya katika propaganda zake kwa maslahi ya nchi.
Lakini kama jeshi letu la polisi likasema sasa limeshindwa, na kwamba wakaomba msaada wa taasisi ya Scotland yard au FBI katika uchunguzi juu ya matukio ya kihalifu,au kama ulivyosema tukio la kupigwa risasi Tundu Lissu ,taasisi hizo zikija hapa kufanya uchunguzi,zitafanya kazi kisayansi kwa sababu mwisho wa siku matokeo ya uchunguzi wao ndiyo yatakayotumika kwa ushahidi mahakamani.
Taasisi ya kiuchunguzi ikidanganya au kufanya propaganda, inashindaje kesi mahakamani? Hata kama CIA wangehusika na uchunguzi kama ulivyodhani mwanzo, unafikiri baada ya hapo wakisema wao wangekuwa na jukumu la kutueleza waliohusika tu na kisha sisi tukawakamata waliotajwa na kuwapeleka jela bila waliotajwa kujitetea mahakamani?
Sasa kama wanadanganya au kufanya propaganda katika uchunguzi wao, wanashindaje mahakamani?
Miaka ya 80 jengo la BOT,liliungua. Serikali baada ya muda kidogo tu ikaomba msaada wa Scotland Yard. Baada ya wiki 2 za uchunguzi,sababu ya moto ilijulikana.

Huko Kenya pia, baada ya kuuawa kwa Waziri wa mambo ya nje bwana Robert Ouko, serikali iliomba msaada wa Scotland yard,wakiongozwa na kachero John Troon. Wakiwa katikati ya uchunguzi, serikali ya Kenya iliwafukuza baada ya kugundua kuwa Nicholaus Biwott ambaye alikuwa mtendaji Ikulu na pia mpwa wa rais Moi, kwamba alionekana kuwa ni mmoja kati ya watu muhimu waliotakiwa kuhojiwa baada ya uchunguzi wa kimazingira, kuona, na kisayansi.
WACHUNGUZI WA NJE HAWAJI KUFANYA PROPAGANDA UKIWAHITAJI.
ILA UNA MOYO,MAANA ISIJE IKAONEKANA MUHALIFU AKAWA MWANAO.
Asante kwa maelezo mazuri,
Wenzetu linapokuja swala la investigation wapo vizuri Sana,
Nakumbuka bbc walimwelezea FBI director aliyekuja Kushughulika na shambulio la Nairobi, Alisema haikuwahi kuijua Kenya kiu jumla, na hata haikuwahi kusikia neno Nairobi,

Ila siku mbili baada ya jamaa KuingiaNairobi, tayari alikuwa amefanikisha kumkamata key suspect akiwa amelazwa hospitali Moja jijini hapo,
Na alikuwa, peke yake 'team solo'

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Walichotuzidi wenzetu si tu akili, Bali ni u smart wao katika kuchakata mambo.

Unaweza hata hiyo kauli ya Pompeo inatolewa kimkakati Sana ila kwa kuwa hatupo smart tunaichukulia kirahisi kama Mtoa Mada anavyoainisha,
Kwamba Cia director anakiri ,waliiba, na kudanganya!! Na Mtoa Mada anakuja kuitoa huku kama reference ya bad conduct, bila hata kujiuliza waliiba nini na kudanganya nini,!!!

Pengine, Cia walidangaya maadui ili kufanikisha jambo la ki usalama? Au labda waliiba nyaraka zilizofanikisha jambo flani muhimu kwao?



Sent using Jamii Forums mobile app


Kipendacho roho, chongo huita kengeza ndo wewe, uko so brainwashed kuwa Muzungu ni superior kwako na kwamba Muzungu can do no wrong huo ni ugonjwa wa akili kafanye therapy, siyo mimi niliyoichukuwa na kuisambaza hiyo Video Clip ni hao hao Wazungu unaowasifia na hata wao ukisoma comments zao wanashangaa pia sasa iweje uje na matusi na kejeli dhidi yetu Waafrika kwa kitu ambacho hata Muzungu anafanya?
 
Asante kwa maelezo mazuri,
Wenzetu linapokuja swala la investigation wapo vizuri Sana,
Nakumbuka bbc walimwelezea FBI director aliyekuja Kushughulika na shambulio la Nairobi, Alisema haikuwahi kuijua Kenya kiu jumla, na hata haikuwahi kusikia neno Nairobi,

Ila siku mbili baada ya jamaa KuingiaNairobi, tayari alikuwa amefanikisha kumkamata key suspect akiwa amelazwa hospitali Moja jijini hapo,
Na alikuwa, peke yake 'team solo'

Sent using Jamii Forums mobile app
Asante pia kwa kusoma maelezo yangu.
Tunajaribu kuelekezana kupitia mada zinazojitokeza katika JF kwa kwa lengo la kupeana taarifa sahihi ili kukuza ufahamu wetu.
Labda kwa nyongeza ya kile nilichosema awali huku nikichukua mwelekeo wa mwanzisha mada Barbarosa,ni kwamba Mike Pompeo anaposema wakati akiwa mkurugenzi wa taasisi ya Ujasusi ya America,CIA kuwa walikuwa wakiiba na pia kudanganya, taarifa hiyo haikutakiwa kumshangaza mwanzisha mada hata kidogo, kwani tunajua nyuma ya pazia hiyo ndiyo kazi ya taasisi ya ujasusi ya nchi yoyote hasa pale inapobidi.
Mfano halisi wa wizi wa CIA ulikuwa hivi;
Shirika la ndege la Saudi Arabia wakati fulani miaka ya 90 waliingia mkataba na kampuni ya Airbus kampuni la Ulaya ili watengenezewe ndege. Marekani, ambayo ni washirika wa karibu wa Saudia wakaja kusikia habari hiyo, wakashangaa kwa nini Saudia hawakuingia mkataba na kampuni ya Boeing ya America.
America walipowauliza Saudia imekuwaje, Saudia wakasema hawezi tena kuingia mkataba na Boeing kwa vile wao walishabadilishana mikataba na Airbus, kwa hiyo kama wangekataa ina maana wangeingia hasara kuvunja mkataba.
Cha kushangaza ile biashara ya Airbus kuiuzia ndege Saudia haikuendelea, na badala yake Boeing wakaonekana wameingia mkataba na Saudia na baadaye Boeing wakaanza kutengeneza ndege huku wakiwaacha Airbus wakilalamika kichinichini. Ilibidi walalamike kimyakimya kwa sababu wangelalamika rasmi kwa sauti kubwa mahakamani, wangeambiwa waoneshe mkataba wa mauziano waliongia.
Kumbe, kwa mujibu wa waandishi wa habari za kiuchunguzi, mkataba ambao Airbus walikuwa nao uliibwa katika ofisi yao kuu, tena katika eneo lenye usalama mkubwa. Na ikatajwa wizi huo ilikuwa ni kazi ya CIA,na ndiyo maana Boeing na Saudia wakawa na jeuri ya kuingia mkataba mpya.

Kichekesho ni kwamba linapokuja suala la kudanganya kwa taasisi za kijasusi,wanaweza kumdanganya hata rais aliyeko madarakani kama wataona inafaa kwa maslahi ya nchi au pengine yao.
Mathalan, rais anaweza kuambiwa na taasisi ya kijasusi ya nchi yake kwamba kuna mtu mmoja mwenye ushawishi katika jamii inaonekana anashirikiana au anatoa siri nyeti za nchi nje kitendo ambacho ni hatari kwa ustawi na usalama wa taifa. Na kwamba wao wameona kuwa kutokana na mwenendo wa mtu huyo, wameona ni bora AONDOLEWE KABISA. Namna watayomueleza watatumia ujanja wa kushawishi ili yeye rais aunge mkono hoja yao bila kupinga. Nyuma ya pazi asichokijua rais ni kwamba huyo mtu aliyetajwa kumbe hafanyi kabisa hayo mambo ambayo kwayo anatuhumiwa. Na kumbe taasisi ya ujasusi kumbe wanamwona huyo mtu atakuwa kikwazo kwa muundo au sera ambayo wao wanataka rais mpya atekeleze au aisimamie kwa maslahi ya nchi.
Haya mambo yanatokea nchi zote, ni ajabu lakini ni kweli.
Ahlan Wasaalan.
 
Damu ya hedhi Ni useless, haitengenezi watoto
Mkuu bila mzunguko wa hedhi mtu anaweza kuzaliwa kweli? Au kama mwanamke hatoi Hizo damu anauwezo wa kushika Mimba kweli..

Damu ya hedhi Ni uthibitisho tosha wa ovary ya Mwanamke kuwa active.
 
Mkuu!

Simultaneous USA bombings za Dar Es Salaam na Nairobi, unafahamu kuwa walikuja FBI?

Sent using Jamii Forums mobile app
Hawezi kujua hilo. Nimejaribu kuwaelewesha hilo naona imeshindikana. FBI wameshaombwa kwenda nchi mbalimbali kusaidia uchunguzi wa matukio ya kihalifu especially ugaidi. Naona yanang'ang'ania tu, "FBI ndani, CIA nje" "wote wanafanya investigation blah blah ". There is a reason FBI wapo chini ya Justice Dept.
 
Watu wazima hawajui tofauti ya investigation ya kawaida na espionage. Shule zetu siku hizi zinatengeneza madudu, Google ndio inaharibu kabisa, siku hizi wagonjwa wanaenda hospitali wakiwa tayari wanajifanya wanajua wanaugua nini na dosage pia. Utasikia mgonjwa anambishia daktari, "mbona Google inasema hivi na hivi" nasikia na madaktari nao wanawambia " haya kajitibu according to hiyo Google"
 
Kipendacho roho, chongo huita kengeza ndo wewe, uko so brainwashed kuwa Muzungu ni superior kwako na kwamba Muzungu can do no wrong huo ni ugonjwa wa akili kafanye therapy, siyo mimi niliyoichukuwa na kuisambaza hiyo Video Clip ni hao hao Wazungu unaowasifia na hata wao ukisoma comments zao wanashangaa pia sasa iweje uje na matusi na kejeli dhidi yetu Waafrika kwa kitu ambacho hata Muzungu anafanya?
Bado narudia Tena jamaa ni smart vichwani mwao!, Sina lengo la kujikekejeli au kujidharau kama unavosema, Bali ni katika tu kukubali Hali halisi

Kuna mdau hapo juu ameelezea Mkataba wa Saudi Arabia ulioibiwa na Cia, ili kuinusuru boeing, kwa maslahi mapana ya USA, wizi kama huo unausemeaje?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
sio lazima iwe ndani tu,hata ubalozi wao ulipolipuliwa walikuja hadi hapa,wao wana deal na matukio ambayo yashatokea kuchunguza,CIA ni intelijensia ya future events
Asante,sikutaka kumkumbusha Jambo Hilo,pengine hajui ama alikua bado mdogo pale Ale Qaida walipolipua US Embassy in Dar and Nairobi,waliokuja kuchunguza tukio Hilo ni FBI Wala sio CIA.
watu wa Lumumba wote wanafanana kuanzia mkubwa Hadi mdogo.
 
Back
Top Bottom