Ntemi Kazwile
JF-Expert Member
- May 14, 2010
- 2,182
- 307
Uingereza kuna waziri wa elimu alilazimishwa kujiuzuru baada ya kugundulika kuwa watoto wake wote walikuwa wanasoma shule za binafsi huku yeye akiliambia taifa kuwa hali ya elimu kwenye shule za umma ilikuwa ni nzuri kuliko wapinzani walivyokuwa wanadai.
Kwa wenzetu ukiwa mtumishi wa umma (hasa wakisiasa kama waziri) na ukakwepa kutumia huduma wanazotumia wananchi wengine ni tiketi inayokuondolea uhalali wa kuendelea kushika huo wadhifa, hapa kwetu ukipata uwaziri unasahau shida kwa kupata huduma kwenye hospitali za binafsi (nje ya nchi), kusomesha watoto wako kwenye shule za binafsi zinatoa huduma bora (au hata nje ya nchi), n.k,.nk.
Taifa likiwa limegubikwa na mizengwe isiyoisha kwenye sekta ya nishati viongozi wetu hawajui hata hali ilivyo pale mtu unapokosa umeme (wao hawana mgao wa umeme na wana majenerata pale unapokatika), kwa maana hiyo hawana hata haraka ya kuona kuwa changamoto ya kukosa umeme inapatiwa ufumbuzi wa haraka na wa kudumu wao wanachoangalia ni namna gani watajaza mifuko yao kwa kuingia mikataba ya kilaghai.
Je tutafika?
Kwa wenzetu ukiwa mtumishi wa umma (hasa wakisiasa kama waziri) na ukakwepa kutumia huduma wanazotumia wananchi wengine ni tiketi inayokuondolea uhalali wa kuendelea kushika huo wadhifa, hapa kwetu ukipata uwaziri unasahau shida kwa kupata huduma kwenye hospitali za binafsi (nje ya nchi), kusomesha watoto wako kwenye shule za binafsi zinatoa huduma bora (au hata nje ya nchi), n.k,.nk.
Taifa likiwa limegubikwa na mizengwe isiyoisha kwenye sekta ya nishati viongozi wetu hawajui hata hali ilivyo pale mtu unapokosa umeme (wao hawana mgao wa umeme na wana majenerata pale unapokatika), kwa maana hiyo hawana hata haraka ya kuona kuwa changamoto ya kukosa umeme inapatiwa ufumbuzi wa haraka na wa kudumu wao wanachoangalia ni namna gani watajaza mifuko yao kwa kuingia mikataba ya kilaghai.
Je tutafika?